Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • hf seh. ya 9 kur. 29-31
  • Mwabuduni Yehova Mkiwa Familia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwabuduni Yehova Mkiwa Familia
  • Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • 1 IMARISHA UHUSIANO WAKO NA YEHOVA
  • 2 FURAHIENI IBADA YENU YA FAMILIA
  • Msaada kwa Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Ibada ya Familia Ni Nini?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Ibada ya Familia​—Je, Mnaweza Kuifanya Ifurahishe Zaidi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Kujenga Pamoja Kijamaa kwa Ajili ya Wakati Ujao wa Milele
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
Pata Habari Zaidi
Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
hf seh. ya 9 kur. 29-31
Wenzi wa ndoa wakijifunza Biblia pamoja

SEHEMU YA 9

Mwabuduni Yehova Mkiwa Familia

“Mwabuduni Yeye aliyezifanya mbingu na dunia.”​—Ufunuo 14:7

Kama ulivyojifunza katika broshua hii, Biblia ina kanuni nyingi zinazoweza kukusaidia wewe na familia yako. Yehova anataka uwe na furaha. Anaahidi kwamba ukimtanguliza, ‘atakuongezea hivi vitu vingine vyote.’ (Mathayo 6:33) Yehova anataka uwe rafiki yake. Tumia kila fursa kusitawisha urafiki pamoja na Mungu. Hiyo ndiyo heshima kubwa zaidi ambayo mwanadamu anaweza kupata. ​—Mathayo 22:37, 38.

1 IMARISHA UHUSIANO WAKO NA YEHOVA

Mume na mke wakihubiri pamoja

BIBLIA INASEMA HIVI: “‘Nitakuwa baba kwenu, nanyi mtakuwa wana na mabinti kwangu,’ asema Yehova.” (2 Wakorintho 6:18) Mungu anataka uwe rafiki yake wa karibu. Sala ni njia moja ya kufanya hivyo. Yehova anakualika ‘usali bila kuacha.’ (1 Wathesalonike 5:17) Yeye yuko tayari kusikiliza mambo yanayokuhangaisha. (Wafilipi 4:6) Unaposali pamoja na familia yako, wataona jinsi unavyompenda Mungu.

Zaidi ya kuongea na Mungu unahitaji kumsikiliza. Unaweza kumsikiliza kwa kusoma Neno lake na machapisho yanayotegemea Biblia. (Zaburi 1:1, 2) Tafakari mambo unayojifunza. (Zaburi 77:11, 12) Kumsikiliza Mungu kunamaanisha pia kuhudhuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida.​—Zaburi 122:1-4.

Kuwaeleza wengine kumhusu Yehova ni njia nyingine muhimu ya kuimarisha uhusiano wako naye. Kadiri unavyozidi kuwaeleza wengine kumhusu ndivyo unavyomkaribia zaidi Yehova.​—Mathayo 28:19, 20.

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Tenga muda wa kusoma Biblia na kusali kila siku

  • Mkiwa familia, tangulizeni mambo ya kiroho badala ya burudani na vitumbuizo

2 FURAHIENI IBADA YENU YA FAMILIA

Baba akijitayarisha kwa ajili ya kujifunza na familia yake na baadaye wanafurahia ibada ya familia

BIBLIA INASEMA HIVI: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yakobo 4:8) Mnahitaji kupanga ratiba ya ibada ya familia na kuifuata. (Mwanzo 18:19) Lakini mengi yanahusika. Mungu anapaswa kuwa sehemu ya maisha yako ya kila siku. Imarisha uhusiano wa familia yako na Mungu kwa kuzungumza kumhusu “unapoketi katika nyumba yako na unapotembea barabarani na unapolala na unapoamka.” (Kumbukumbu la Torati 6:6, 7) Uwe na lengo la kuiga mfano wa Yoshua, aliyesema hivi: “Mimi na nyumba yangu, tutamtumikia Yehova.”​—Yoshua 24:15.

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Panga ratiba ya kuendelea ambayo inazingatia mahitaji ya kila mshiriki wa familia

Mama akijifunza na kijana wake mdogo ; familia ikicheza mchezo wa kuigiza;baba akijifunza na binti yake

WATUMISHI WA YEHOVA WENYE FURAHA

Hakuna jambo bora kuliko kumwabudu Yehova Mungu. Yeye anafurahi kukuona wewe na familia yako mkimtumikia kwa uaminifu. Kadiri mnavyoendelea kufanya hivyo, ndivyo mtakavyomkaribia zaidi Yehova. (Marko 12:30; Waefeso 5:1) Kumhusisha Mungu katika ndoa yenu kutaimarisha uhusiano wenu. (Mhubiri 4:12; Isaya 48:17) Wewe na familia yako mnaweza kuwa na furaha milele, kwa kujua kwamba “Yehova Mungu wako amekubariki.”​—Kumbukumbu la Torati 12:7.

JIULIZE . . .

  • Ni lini mara ya mwisho mimi na mwenzi wangu tuliposali pamoja?

  • Ninaweza kujifunza habari gani pamoja na familia yangu ili kuimarisha uhusiano wetu na Yehova?

TAARIFA KWA VICHWA VYA FAMILIA

  • Usiruhusu chochote kivuruge ibada yenu ya familia

  • Kabla ya ibada, waambie washiriki wa familia mambo mtakayozungumzia ili wajitayarishe

  • Hakikisha kila mshiriki wa familia yupo

  • Hakikisha kila mmoja atajihisi amestarehe

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki