Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 24 uku. 62-uku. 63 fu. 2
  • Walivunja Ahadi Yao

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Walivunja Ahadi Yao
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Ndama ya Dhahabu 36
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Kuzijua Njia za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Musa—Jinsi Maisha Yake Yanavyokuhusu
    Amkeni!—2004
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 24 uku. 62-uku. 63 fu. 2
Waisraeli wakiimba na kucheza kuzunguka ndama wa dhahabu

SOMO LA 24

Walivunja Ahadi Yao

Yehova alimwambia Musa hivi: ‘Njoo kwangu juu mlimani. Nitaandika sheria yangu juu ya mabamba ya mawe halafu nitakupa.’ Musa akapanda juu mlimani na kukaa huko kwa siku 40. Alipokuwa huko, Yehova akaandika zile Amri Kumi juu ya mabamba mawili ya mawe na kumpa Musa mabamba hayo.

Musa akitupa chini mabamba ya mawe

Baada ya muda, Waisraeli wakafikiri kwamba Musa alikuwa amewaacha. Wakamwambia Haruni hivi: ‘Tunataka mtu wa kutuongoza. Tutengenezee mungu!’ Haruni akasema: ‘Nipeni dhahabu yenu.’ Akaiyeyusha dhahabu na kuifanya kuwa sanamu ya ndama. Watu wakasema hivi: ‘Huyu ndiye Mungu aliyetutoa Misri.’ Wakaanza kuabudu ndama huyo wa dhahabu na wakafanya sherehe. Je, hilo lilikuwa kosa? Ndiyo, kwa kuwa watu hao walikuwa wameahidi kumtumikia Yehova peke yake. Lakini sasa walikuwa wanavunja ahadi hiyo.

Yehova aliona kilichokuwa kikitendeka, naye akamwambia Musa hivi: ‘Shuka urudi kwa watu. Wameacha kunitii na wanaabudu mungu wa uwongo.’ Musa akashuka haraka kutoka mlimani, akiwa amebeba yale mabamba mawili.

Alipoikaribia kambi, Musa akawasikia watu wakiimba. Kisha akawaona wakicheza dansi na kuiinamia sanamu ya ndama. Musa akakasirika sana. Akatupa yale mabamba mawili chini, nayo yakavunjika vipande-vipande. Akaiharibu sanamu hiyo mara moja. Kisha akamuuliza Haruni hivi: ‘Watu hawa walikuambia nini ili ukubali kufanya jambo hili baya?’ Haruni akasema: ‘Usikasirike. Wewe unajua jinsi watu hawa walivyo. Walitaka niwatengenezee mungu, kwa hiyo nikatupa dhahabu yao ndani ya moto na sanamu hiyo ya ndama ikatokea!’ Haruni hakupaswa kufanya hivyo. Musa akarudi juu mlimani na kumsihi Yehova awasamehe watu hao.

Yehova aliwasamehe wale waliokuwa tayari kumtii. Je, umeona kwa nini ilikuwa muhimu kwa Waisraeli kufuata uongozi wa Musa?

“Wakati wowote unapoweka nadhiri kwa Mungu, usikawie kuitimiza, kwa maana hapendezwi na wapumbavu. Unapoweka nadhiri, itimize.”​—Mhubiri 5:4

Maswali: Waisraeli walifanya nini Musa alipokuwa ameondoka? Musa alifanya nini aliporudi?

Kutoka 24:12-18; 32:1-30

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki