Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 29 uku. 74-uku. 75 fu. 2
  • Yehova Amchagua Yoshua

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yehova Amchagua Yoshua
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Yoshua Anakuwa Kiongozi
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Aliyokumbuka Yoshua
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • “Uwe Hodari Tu na Ushujaa Mwingi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kitabu Cha Biblia Namba 6—Yoshua
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 29 uku. 74-uku. 75 fu. 2
Makuhani wakiwa wamebeba sanduku la agano wakipita kwenye Mto Yordani

SOMO LA 29

Yehova Amchagua Yoshua

Yoshua akisoma Sheria

Baada ya kuongoza taifa la Israeli kwa miaka mingi, Musa alikuwa anakaribia kufa. Yehova akamwambia hivi: ‘Si wewe utakayewaingiza Waisraeli kwenye Nchi ya Ahadi. Lakini nitakuruhusu uione nchi hiyo.’ Kisha Musa akamwomba Yehova achague kiongozi mpya wa kuwaongoza watu. Yehova akamwambia hivi: ‘Nenda kwa Yoshua umwambie yeye ndiye atakayekuwa kiongozi.’

Musa akaliambia taifa lote kwamba angekufa hivi karibuni na kwamba Yehova amemchagua Yoshua awe kiongozi wa kuwaingiza katika Nchi ya Ahadi. Kisha Musa akamwambia Yoshua hivi: ‘Usiogope. Yehova atakusaidia.’ Muda mfupi baada ya hapo, Musa akapanda kwenda juu ya Mlima Nebo, na akiwa huko Yehova akamwonyesha nchi ambayo Yeye alikuwa ameahidi kuwapa Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Musa alikuwa na umri wa miaka 120 alipokufa.

Musa akimweka rasmi Yoshua mbele ya kuhani na wanaume wengine

Yehova akamwambia Yoshua hivi: ‘Vuka Mto Yordani, na uingie Kanaani. Nitakusadia kama tu nilivyomsaidia Musa. Hakikisha kwamba unasoma Sheria yangu kila siku. Usiogope. Uwe hodari. Nenda, na ufanye yote ambayo nimekuamuru.’

Yoshua akatuma wapelelezi wawili waende katika jiji la Yeriko. Katika hadithi inayofuata, tutaona ni nini kilichotukia huko. Waliporudi, walisema kwamba ulikuwa wakati unaofaa kuingia Kanaani. Siku iliyofuata, Yoshua akaliambia taifa lote livunje kambi. Kisha akawaambia makuhani waliokuwa wakibeba sanduku la agano watangulie kuingia katika Mto Yordani. Mto ulikuwa umefurika. Lakini mara tu miguu ya makuhani ilipokanyaga maji, mto ukaacha kutiririka, na maji yakakauka! Makuhani wakatembea mpaka katikati ya mto na kusimama hapo hadi taifa lote la Israeli lilipovuka upande ule mwingine. Unafikiri kwamba muujiza huo uliwakumbusha kile ambacho Yehova alikuwa amefanya kwenye Bahari Nyekundu?

Hatimaye, baada ya miaka hiyo yote, Waisraeli walikuwa wameingia katika Nchi ya Ahadi. Wangeweza kujenga nyumba na majiji. Wangeweza kupanda mashamba ya chakula, ya mizabibu, na ya matunda. Nchi hiyo ilikuwa ikitiririka maziwa na asali.

“Yehova atakuongoza daima na kukushibisha hata katika nchi iliyokauka.”​—Isaya 58:11

Maswali: Ni nani aliyewaongoza Waisraeli baada ya Musa kufa? Ni nini kilichotendeka kwenye Mto Yordani?

Hesabu 27:12-23; Kumbukumbu la Torati 31:1-8; 34:1-12; Yoshua 1:1–3:17

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki