Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 68 uku. 162-uku. 163 fu. 1
  • Elisabeti Apata Mtoto

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Elisabeti Apata Mtoto
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Yule Atakayetayarisha Njia Azaliwa
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Walithawabishwa kwa Kutembea Bila Lawama
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Wapokea Ujumbe Kutoka kwa Mungu
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Mtayarishaji wa Njia Azaliwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 68 uku. 162-uku. 163 fu. 1
Zekaria anawaambia marafiki na watu wa ukoo kwamba mwana wake ataitwa Yohana

SOMO LA 68

Elisabeti Apata Mtoto

Miaka zaidi ya 400 baada ya kuta za Yerusalemu kujengwa upya, kuhani anayeitwa Zekaria na mke wake Elisabeti, waliishi karibu na jiji hilo. Walikuwa wamefunga ndoa kwa miaka mingi lakini hawakuwa na watoto. Siku moja Zekaria alipokuwa akifukiza uvumba katika patakatifu pa hekalu, malaika Gabrieli alimtokea. Zekaria akaogopa sana, lakini Gabrieli akamwambia: ‘Usiogope. Ninakuletea habari njema kutoka kwa Yehova. Mke wako, Elisabeti, atakuzalia mwana nawe utamwita jina lake Yohana. Yehova amemchagua Yohana afanye kazi ya pekee.’ Zekaria akauliza: ‘Ninawezaje kukuamini? Mimi na mke wangu ni wazee sana tusiweze kupata mtoto.’ Gabrieli akamwambia: ‘Nilitumwa na Mungu kukupatia habari hizi. Lakini kwa sababu hukuniamini, hutaweza kuzungumza mpaka mtoto huyo azaliwe.’

Zekaria alikaa katika patakatifu kwa muda mrefu kuliko kawaida. Hivyo, mwishowe alipotoka nje, watu waliokuwa wakingoja walitaka kujua kilichotokea. Lakini Zekaria hakuweza kuzungumza. Angeweza tu kutoa ishara kwa mikono yake. Kisha watu wakatambua kwamba Zekaria alikuwa amepata ujumbe kutoka kwa Mungu.

Baada ya muda, Elisabeti akapata mimba na kuzaa mwana, kama malaika alivyosema. Rafiki zake na watu wa ukoo walikuja kumwona mtoto. Walifurahi sana. Elisabeti akasema: ‘Ataitwa Yohana.’ Wakamwambia: ‘Hakuna yeyote katika familia yenu anayeitwa kwa jina hilo. Mwite Zekaria, jina la baba yake.’ Lakini Zekaria akaandika maneno haya: ‘Yohana ndilo jina lake.’ Wakati huohuo, Zekaria akaanza kuzungumza tena! Habari kuhusu mtoto huyo zikaenea kotekote katika Yudea, na watu wakajiuliza hivi: ‘Mtoto huyu atakuwa mtu wa aina gani?’

Kisha Zekaria akajazwa roho takatifu. Akatoa unabii huu: ‘Na abarikiwe Yehova. Alimwahidi Abrahamu kwamba angemtuma mwokozi, Masihi ili kutuokoa. Yohana atakuwa nabii, naye atatayarisha njia kwa ajili ya Masihi.’

Maria, mtu wa ukoo wa Elisabeti pia alipata tukio la pekee. Acheni tuchunguze jambo hilo katika somo linalofuata.

“Kwa wanadamu jambo hilo haliwezekani, lakini kwa Mungu mambo yote yanawezekana.”​—Mathayo 19:26

Maswali: Gabrieli alimwambia Zekaria nini? Yohana angefanya kazi gani ya pekee?

Mathayo 11:7-14; Luka 1:5-25, 57-79; Isaya 40:3; Malaki 3:1

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki