Utangulizi wa Sehemu ya Pili 2
Kwa nini Yehova alileta gharika na kuharibu ulimwengu wa wakati huo? Mwanzoni mwa historia ya wanadamu, kulitokea ushindani kati ya wema na uovu. Baadhi ya watu, kama vile Adamu, Hawa, na mtoto wao Kaini, walichagua kufanya mambo mabaya. Watu wachache kama vile Abeli na Noa, walichagua kufanya mema. Watu wengi walikuwa wabaya sana hivi kwamba Yehova aliamua kuleta mwisho wa ulimwengu huo mwovu. Sehemu hii itatusaidia kujifunza jinsi Yehova anavyohisi kuhusu maamuzi tunayofanya na kwamba hataruhusu kamwe uovu ushinde wema.