Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lmd somo la 8
  • Subira

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Subira
  • Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Alifanya Nini?
  • Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?
  • Mwige Yesu
  • Endelea Kuwa Mwenye Subira
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Tumia Video Kufundisha
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
  • Nufaika Kutokana na Dhabihu ya Yesu
    Habari Zaidi
  • Kupendezwa na Watu
    Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
Pata Habari Zaidi
Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
lmd somo la 8

KUFUATIA UPENDEZI

Yesu akimkaribia ndugu yake Yakobo akiwa kazini. Yakobo anashangaa kumwona Yesu.

Yohana 7:​3-5; 1 Kor. 15:​3, 4, 7

SOMO LA 8

Subira

Kanuni: “Upendo ni wenye subira.”—1 Kor. 13:4.

Yesu Alifanya Nini?

Yesu akimkaribia ndugu yake Yakobo akiwa kazini. Yakobo anashangaa kumwona Yesu.

VIDEO: Yesu Anamsaidia Ndugu Yake kwa Subira

1. Tazama VIDEO, au soma Yohana 7:​3-5 na 1 Wakorintho 15:​3, 4, 7. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1. Mwanzoni, ndugu za Yesu waliitikiaje alipowahubiria?

  2. Ni nini kinachoonyesha kwamba Yesu aliendelea kumsaidia ndugu yake Yakobo?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?

2. Tunahitaji kuwa na subira kwa sababu baadhi ya watu hawakubali haraka habari njema.

Mwige Yesu

3. Jaribu kutumia njia nyingine. Ikiwa mtu hakubali mara moja kujifunza Biblia, usimlazimishe. Inapofaa, tumia video au makala fulani kumsaidia aelewe kinachotendeka kwenye funzo la Biblia na jinsi atakavyonufaika.

4. Usimlinganishe na wengine. Watu wanatofautiana. Ikiwa mshiriki wa familia au mtu unayemrudia anasita kujifunza Biblia au kukubali fundisho la Biblia, fikiria kwa nini anafanya hivyo. Je, kuna fundisho la dini analopenda sana? Je, anashinikizwa na watu wa ukoo au majirani? Mpe muda wa kufikiria mambo uliyomwambia na kuthamini mafundisho ya Biblia.

5. Sali kwa ajili ya watu wanaopendezwa. Mwombe Yehova akusaidie uwe na busara na mtazamo mzuri. Sali ili utambue ni wakati gani unapaswa kuacha kumtembelea tena mtu ambaye hapendezwi.—1 Kor. 9:26.

SOMA PIA

Marko 4:​26-28; 1 Kor. 3:​5-9; 2 Pet. 3:9

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki