Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 1/1 kur. 20-24
  • Je! Afya Kamili Katika Mazingira Yaliyokamilika Yaweza Kuwapo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Afya Kamili Katika Mazingira Yaliyokamilika Yaweza Kuwapo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • CHANZO CHA AFYA YA KWELI
  • KUPONYWA KWA MWUJIZA
  • WENGINE HAWATAPONYWA
  • MAZINGIRA YA PARADISO
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 1/1 kur. 20-24

Je! Afya Kamili Katika Mazingira Yaliyokamilika Yaweza Kuwapo?

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1-3. Toa ushuhuda wa kwamba afya ya watu kwa jumla inaharibika.

AFYA ya watu kwa ujumla inaharibika kila siku. Ilishtua serikali ya United States miaka fulani iliyopita wakati kadiri ya juu kwa kila vijana 100 walipopatikana wasiofaa kwa utumishi wa kijeshi kwa kimwili. Ripoti iliyotolewa nyumaye na aliyekuwa rais wakati huo John F. Kennedy ilisema kwa habari ya programu yake ya kufaa kimwili: “Kadiri ya 20 kwa 100 ya shule zote za nchi hawana programu ya kawaidi ya kufaa, na kadiri ya 20 kwa 100 ya watoto wetu wa shule hawawezi kupita jaribio dogo sana. 80 kwa 100 hawawezi kupita sehemu zote za mtihani wenye mambo mengi zaidi. . . . Nasi kwa shida tumeanza kushughulikia ugumu ulio mkubwa mno wa kufaa kwa watu wazima.”

2 Hali hii iliyomo katika mojawapo la yanayoitwa kwa kawaida mataifa ‘yenye maendeleo’ kupita yote ya ulimwengu yaonyesha kwamba jamii iliyohakikishwa kwa kisayansi haiwaleti watu karibu zaidi na afya kamili. Kwa kweli, mazingira yaliyo ya lazima kwa afya njema yanazidi kuchafuliwa.

3 Hata hivyo, kuna tumaini hakika, lenye msingi imara la afya kamili katika mazingira yaliyokamilika. Hii yawezekanaje?

CHANZO CHA AFYA YA KWELI

4. Ili kufurahia afya ya kweli, kwa sababu gani kuna mengi zaidi ya lazima kuliko utabibu na mazingira mazuri?

4 Ili kupata afya ya kweli, jambo fulani zaidi ya utabibu na mazingira linahitajiwa. Kama vile mtu ye yote aliyemwendea daktari awezavyo kukuambia, utabibu, ijapokuwa ni wenye msaada nyakati nyingine, hauleti afya kamili. Wala watu wanaoishi nje mashambani, mbali na uchafu mwingi wa miji, hawako huru na uharibifu wa uzee. Wanadamu leo wanajikokota chini ya mzigo uliorithiwa wa dhambi, na hii ndiyo iletayo ugonjwa na mwishowe kutokeza mauti. Hakuna mwanadamu asiyekamilika awezaye kujikomboa mwenyewe ama mtu mwingine ye yote katika hali hii. (Rum. 5:12; Zab. 49:7-9) Lakini Mungu ametoa njia ambayo kwayo ukombozi huo wawezekana. Amefanya hivi kupitia kwa Mwanawe Yesu Kristo.

5. (a) Afya ya kweli inaweza kupatikana kwa njia gani, naye Yesu alionyeshaje hivi? (b) Yesu alifanya ahadi gani kwa habari ya mazingira mazuri kwa wanadamu?

5 Alipokuwa duniani, Yesu alionyesha kwamba wale waliotumia imani katika yeye wangeweza kusamehewa dhambi zao na kwa njia hii wangeweza kurudishwa kwenye afya njema. Hivyo alipomwambia mtu aliyepooza, “Umesamehewa dhambi zako,” mtu huyo aliponywa. (Marko 2:1-12) Vile vile Yesu alionyesha kwamba atakapopewa ufalme wa wanadamu kama milki yake, paradiso ambayo wanadamu walikuwa wamefurahia katika Edeni itarudishwa. Mtu aliyekuwa anakufa kando ya Yesu ndiye aliyemwambia: “Yesu, unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.” Hii ilimvuta Yesu kujibu: “Kweli nakwambia leo, Wewe utakuwa pamoja nami katika Paradiso.”​—Luka 23:42, 43, NW.

6. Nani watakaoishi katika paradiso iliyorudishwa?

6 “Paradiso” maana yake “shamba lenye mfano wa bustani.” Makao ya paradiso ambayo Mungu aliwapa wanadamu wawili wa kwanza yalipotezwa kwa kutokutii. (Mwa. 3:1-7, 17-24) Wale watakaopata uzima katika mazingira yaliyokamilika ya paradiso iliyorudishwa lazima waonyeshe kwamba wao si kama Adamu, lakini kwamba wao wanafanya mapenzi ya Mungu, wakimtii kwa moyo.

KUPONYWA KWA MWUJIZA

7. Mungu alionyeshaje kale kwamba aliijua hali yenye shida ya mwanadamu na kwamba angefanya jambo fulani kusudi aiondoe hali hii?

7 Zamani sana Mungu alionyesha kwamba alijua hali ya mwanadamu yenye shida na kwamba yeye anajali naye ataiondoa hali hii. Kwa nabii wake Ezekieli alitoa njozi ambayo katika hiyo Ezekieli aliona “mto wa maji ya uzima” ukitiririka kutoka patakatifu pa Yehova, Patakatifu Zaidi Sana pa hekalu, ambapo Yehova kwa kufananishwa alikuwapo. Maji haya yalitokeza kama kijito, lakini yakawa bubujiko lenye nguvu yalipotiririka kuelekea mashariki kwenye bonde liitwalo Araba, nayo yakatiririka moja kwa moja kuingia katika Bahari ya Chumvi. Matokeo yaliyoletwa yalitabiri utimizo wa ajabu wenye kufurahisha, mmoja ambao hakuna ye yote kati ya wanadamu astahiliye kutopendezwa nao. Ezekieli anatoa habari juu ya njozi yake:

8, 9. Ezekieli aliona mwujiza gani?

8 “[Malaika wa Mungu] akaniambia, Mwanadamu, je! umeona haya? Kisha akanichukua, akanirudisha mpaka ukingo wa mto. Basi nikiisha kurudi, tazama, kando ya ukingo wa mto ilikuwapo miti mingi sana, upande huu na upande huu. Ndipo akaniambia, Maji haya yanatoka kwenda pande za nchi ya mashariki, nayo yanashuka mpaka Araba, na kuingia katika bahari; maji yatokezwayo yataingia baharini, na maji yake yataponyeka. Tena itakuwa, kila kiumbe hai kisongamanacho, kila mahali itakapofika mito hiyo, kitaishi; kutakuwapo wingi mkubwa wa samaki, kwa sababu maji haya yamefika huko; maana maji yale yataponyeka, na kila kitu kitaishi po pote utakapofikilia mto huo.”​—Eze. 47:6-9.

9 Humo, katika maji haya yenye chumvi, yasiyo na uhai na yenye uso ulio chini zaidi duniani, Ezekieli aliona mwujiza ukitukia. Bahari ilianza kujawa na samaki wenye uhai! Bubujiko lilikuwa limeyakoleza maji ili kwamba yaweze kuchukua uzima!

10-13. Nini kilichofananishwa kwa unabii na uhakika wa kwamba wavuvi walikuwa wakitenda kwa bidii katika pwani ya magharibi ya Bahari ya Chumvi?

10 Ezekieli alipewa ushuhuda wa kweli kwamba iliyokuwa Bahari ya Chumvi sasa ilikuwa imejaa uhai​—kwamba kijito kutoka katika hekalu la Yehova kilikuwa “maji ya uzima” kweli kweli. Malaika anaendelea na masimulizi:

11 “Tena itakuwa, wavuvi watasimama karibu nao; toka Engedi [“Chemchemi ya Mwana-mbuzi”] mpaka En-eglaimu [“Chemchemi ya Ndama Wawili,” karibu maili kumi na nane kaskazini ya Engedi, katika pwani ya magharibi ya Bahari ya Chumvi], patakuwa ni mahali pa kutandazia nyavu; samaki wao watakuwa wa namna zao mbalimbali, kama samaki wa bahari kubwa [Bahari ya Kati], wengi sana.”​—⁠Eze. 47:10.

12 Kwa wazi sana njozi hii ni moja iliyo juu ya utawala wa Kristo wa miaka 1,000. Kwa hiyo wavuvi wa unabii huu sio “wavuvi wa watu” ambao Kristo alisema wanafunzi wake wangekuwa. (Mt. 4:19) Kwa maana, katika “nchi mpya” iliyoahidiwa, hakutakuwako kushika watu kama samaki ili wawe wanafunzi wa Yesu.​—2 Pet. 3:13.

13 Kwa hiyo kuonekana kwa wavuvi katika njozi ya Ezekieli kunafananisha tu kwa unabii ya kwamba “maji ya uzima,” mipango ya Mungu ya uzima kupitia kwa dhabihu ya ukombozi ya Kristo na utumishi wa kikuhani, yatatoa afya ya kweli, yenye nguvu na uzima kwa wanadamu.

14-16. Ni mambo gani lazima yaondolewe mbele ya wanadamu kupata afya yote?

14 Leo hali zinazowapata wanadamu ni zenye kufisha, kama vile mazingira ya Bahari ya Chumvi. Hii ni kweli si kwa habari ya mazingira ya kisasa yaliyochafuliwa ya asili tu, ambayo kidogo kidogo mwanadamu anazidi kuyaharibu. (Ufu. 11:18) La maana zaidi, vile vile inatia na kutokamilika, matokeo yaliyorithiwa ya dhambi ya babu yetu Adamu, yanayoleta kifo.

15 Lakini, liko jambo jingine linalofanya afya kamili katika dunia ya paradiso isiweze kuwapo chini ya hali zilizopo. Jambo hili linaonyeshwa katika maneno ya mtume Yohana, “Ulimwengu wote unakaa katika uwezo wa yule mwovu.” (1 Yohana 5:19, NW; 2 Kor. 4:4) Shetani Ibilisi anaongoza wingi wa wanadamu kwa kutoonekana, naye ndiye chanzo kikubwa cha ole za mwanadamu. Zaidi hii ndivyo ilivyo sasa katika huu wakati wa mwisho wa ulimwengu.​—Ufu. 12:3, 4, 7-13.

16 Kwa hiyo, ‘maji yenye kutoa uzima’ yaliyotabiriwa hayatatiririka yarudishe afya kamili kwa wanadamu mpaka Malaika Mkuu mwenye nguvu wa Mungu, Yesu Kristo, amewaondoa Shetani na mashetani zake kwa kuwatupa ndani ya “shimo” kusudi kwamba wasiisumbue dunia. Ndipo waokokaji wa uharibifu wa ulimwengu huu watakapokuwa wa kwanza kunywa kwa uhuru maji ya uzima. Lakini hawatakuwa peke yao. Wingi wa mto utatoa ya kutosha kwa wanadamu wote watakaofufuliwa.​—Ufu. 20:1-3, NW.

WENGINE HAWATAPONYWA

17, 18. Nini kitakachotokea kwa wale watakaokataa kunywa katika maji ya uzima kwa imani na utii?

17 Samaki waliofananishwa kama walioshikwa katika maji yaliyokolezwa kwa mwujiza ya bahari ya chumvi walikuwa samaki “safi,” wawezao kuliwa chini ya sheria ya Musa, si viumbe vichafu vya baharini. Vivyo hivyo wale watakaoponywa na maji yenye kutoa uzima watakuwa ni wale wanaotumia imani na utii katika ibada safi. Lakini je! nini kitakachotukia mtu akiwa mwasi na asiyetii sheria na mipango ya hiyo taratibu ya mambo chini ya utawala wa “mbingu mpya” za Kimasihi?​—Ufu. 21:1.

18 Kwa kujibu, njozi ya Ezekieli inasema juu ya maeneo fulani yasiyofikiwa na maji yenye kuponya: “Bali mahali penye matope, na maziwa yake, hayataponywa; yataachwa yawe ya chumvi.” (Eze. 47:11) Kwa usemi wa mfano, hii ingeonyesha kwamba ye yote atakeyakataa “maji” yenye kuponya ya Yehova kwa makusudi hatapata uzima wa milele. Imeandikwa juu ya waliofufuliwa chini ya Ufalme wa Yehova wa Kimasihi: “Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.” Hao wasio na imani, wasiotii wataondolewa katika jamii yenye haki ya kibinadamu ya wale watakaopokea “maji” ya uzima.​—Ufu. 20:14, 15.

MAZINGIRA YA PARADISO

19. Yehova alionyeshaje kwamba ni kusudi lake kwa wanadamu wakamilifu wawe na mazingira ya paradiso?

19 Yehova alionyesha kusudi lake kwamba wanadamu wakamilifu wawe na mazingira yaliyokamilika ya paradiso wakati alipowaweka Adamu na Hawa wakamilifu katika bustani ya Edeni. Walipoasi walifukuzwa, kwa maana kubaki katika bustani kungekuwa pendeleo la watu wakamilifu, wenye haki peke yao.​—Mwa. 3:24.

20, 21. Ni njozi gani ya mazingira ya paradiso aliyopewa Ezekieli?

20 Kwa kulingana, njozi ya Ezekieli haiachi sehemu hii ya mazingira iliyo muhimu kwa furaha kamili. Malaika aliendelea kusema:

21 “Na karibu na mto, juu ya ukingo wake, upande huu na upande huu, utamea kila mti wa chakula, ambao majani yake hayatanyauka, wala matunda yake hayatatindika kamwe; utatoa matunda mapya kila mwezi, kwa sababu maji yake yanatoka mahali patakatifu; na matunda yake yatakuwa ni chakula; na majani yake yatakuwa ni dawa.”​—⁠Eze. 47:12.

22, 23. Yehova alihakikishaje kabisa juu ya mazingira ya paradiso, “katika kinywa cha mashahidi wawili”?

22 Yehova anatuhakikishia ukweli wa makao ya paradiso kwa kutoa ushuhuda kwa kinywa cha mashahidi wawili. (2 Kor. 13:1) Namna gani? Zaidi ya miaka 600 nyuma ya unabii wa Ezekieli, Kristo alituma malaika wake kwa mtume Yohana akiwa na njozi yenye kuhakikisha, ikihakikisha kwamba Yehova ndiye Mungu ambaye hageuki na ambaye makusudi yake ni yenye uhakika wa kutimizwa. Yohana anatoa habari juu ya njozi yake ya “Yerusalemu Mpya” wa kimbinguni:

23 “Na njia ya mji ni dhahabu safi kama kioo kiangavu. Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung’aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo, katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa.”​—Ufu. 21:21; 22:1, 2.

24, 25. Nini kinachofananishwa na matunda ya “kila mwezi,” na majani?

24 Njozi ya Yohana iliweka utimizo wa njozi penye wakati ambapo Yehova anatawala kupitia kwa ufalme wa Masihi wake, “Mwana-Kondoo.” Njozi za Yohana na Ezekieli zinashuhudia habari njema zenye kufariji kwamba bubujiko la maji yenye kutoa uzima litafuatana na ukuzi wa mimea kwa ajili ya uzuri na chakula kizuri, kama ilivyokuwa kwa bustani ya kwanza ya Edeni. Msaada unaoendelea wa vitu vyenye kuendeleza uzima kwa wingi, usioharibiwa na ukosefu wa mvua, ugonjwa ama balaa, utakuwako ili wanadamu waufurahie, kana kwamba kwa njia ya miti ya matunda inayozaa matunda mapya “kila mwezi.”

25 “Majani” ya miti hiyo yatakuwa “ya kuwaponya mataifa.” Hii inatuhakikishia kwamba kutakuwako afya kamili bila kikomo, kwa wanadamu watiifu.

26. Hali zote zitakuwako kwa njia gani kwa furaha yote?

26 Hali zote zitakuwako basi kwa ajili ya afya kamili na furaha. Wanadamu wataweza kushukuru kwa uzima kabisa, nayo mazingira yenye afya, yaliyo safi yataikamilisha furaha yao. Hakutakuwako woga kwamba maji yatakauka, kwa kuwa Chanzo chake ni kisichoishika. Lo! ni nguvu kama nini wale wanaokunywa humo watakazokuwa nazo kwa ajili ya kazi katika kuitunza paradiso, kama Adamu na Hawa walivyoagizwa kufanya lakini wakashindwa!

27. Hali itakuwa nini kwa habari ya ukamatano wa mwanadamu na wanyama?

27 Yehova, katika kubariki watu wake, vile vile ataleta elimu ya tabia za vitu vilivyo hai kama vile alivyofanya katika bustani ya Edeni. Ndiyo, kama vile alivyofanya “agano na wanyama wa mashamba” kwa ajili ya faida na usalama wa watu wake walio wakf wa kale katika Israeli, zaidi sana ulinzi wake utakuwa wenye kuendelea chini ya utawala wa Ufalme, kuelekea hatari zote kwa uhai na afya.​—Hos. 2:18.

28, 29. (a) Imetupasa tuvutweje na elimu tunayopewa na njozi ya Ezekieli? (b) Wanadamu waaminifu watasikia tangazo gani lenye kuchangamsha, katika “nchi mpya” ya Mungu?

28 Ujuzi wa fadhili zisizostahili za Yehova kupitia kwa Kristo umepaswa uwavute wote wanaoziona wamsifu. Kusifu huku kunafanywa kwa njia nzuri zaidi kwa kupatanisha maisha zetu na matakwa yaliyowekwa katika Neno lake Biblia na kwa kulitangaza tumaini hili la ajabu kwa wengine. (Ufu. 22:17; Rum. 10:10) Hakuna jambo liwezalo kuwa zuri zaidi kupita, katika hali ya afya kamili na katika mazingira mazuri, yenye amani, yasiyo na uhalifu na yasiyochafuliwa, kusikia maneno:

29 “Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”​—Ufu. 21:3, 4.

​—Kutoka Kitabu “The Nations Shall Know That I Am Jehovah”​—How?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki