Nani Awezaye Kusaidia?
◆ Ikiwa moyo wa mtu umevutwa na habari njema kwa kweli zinazopatikana katika Biblia, yeye anataka kuwasaidia wengine wawe na tumaini la ajabu la kuishi katika paradiso iliyorudishwa duniani. Si lazima ayajue yote yaliyomo katika Biblia kusudi awasaidie wengine. Wala si lazima awe na kila kitu kama mwalimu. Vizuizi vya namna zote na magumu vyaweza kushindwa ikiwa mtu anataka kusaidia kwa kweli.
Hii inaonyeshwa na maono ya mwanamke mwenye kuzungumza Kispania anayeshirikiana na kundi la mashahidi wa Yehova katika mji wa New York. Ebu angalia ni akina nani waliotaka kumsaidia na wakafanya hivyo:
“Mimi nilikuwa mshiriki wa Christian Spirit Church. Mume wangu ndiye ‘Kiongozi’ wa kanisa hili. Mara nyingi mashahidi wa Yehova walinifikia mlangoni pangu wazungumze Biblia nami. Mara nyingi nilikataa kabisa kuzungumza nao. Ama nisingefungua mlango.
“Siku moja akaja mwanamume mzee mmoja mlangoni pangu anishuhudie kutoka kwa Biblia. Kwa wazi asiyeelimishwa na alisoma kwa shida. Nilipomwona akijitahidi na Biblia yake, nilivutwa na unyofu wake nami nikamkaribisha ndani. Alinieleza kwamba ndio sasa alikuwa anaanza kujifunza kusoma; alikuwa ameanza kushirikiana na mashahidi wa Yehova nao walikuwa wakimfunza kusoma na kuandika. Kwa unyenyekevu akaomba radhi kwa kutoweza kusoma vizuri zaidi. Hata hivyo alieleza kwamba alijua namna lilivyo jambo la haraka kuuhubiri ujumbe unaoenezwa duniani pote na mashahidi wa Yehova na kwa hiyo akaamua kuhubiri kwa njia bora kama alivyoweza. Kwa kuwa hakujua kusoma sana, nilimsaidia kuyatafuta maandiko nami niliyasoma kwa sauti. Kisha alitoa maelezo juu yake kama alivyoweza.
“Alinikaribisha nijifunze Biblia pamoja naye. Kwa kuwa nilivutwa na unyofu aliouonyesha katika kuhubiri kwake, nilikubali. Lakini, nyuma ya ziara moja au mbili hivi ilikuwa wazi kwamba alikuwa hajajua bado kusoma vya kutosha kuweza kufanya funzo la kawaida la Biblia pamoja nami. Alipanga kwamba mkewe aliongoze funzo.
“Wakati wa ziara yake ya kwanza ilionekana wazi kwamba ulikuwako ugumu bado. Alikuwa mzee sana na alisikia kwa shida. Funzo liliendelea polepole nami nikajifunza mambo fulani juu ya ufalme wa Mungu. Lakini kilikuwapo kizuizi kikubwa kwa maana kidogo alikuwa kiziwi. Mwishowe mipango ikafanywa kwamba Shahidi mwingine anitembelee na kujifunza nami. “Mbele ya muda mwingi kupita niliuona ubatili na kutofuatana kwa mazoea ya uchawi na Maandiko. Nikaamua kwamba, kusudi nimpendeze Mungu, ilinipasa niliache kanisa nililokuwa nikihudhuria. Mume wangu akakataa, lakini kwa kimya nikauliza sababu gani yeye kama ‘Kiongozi’ hakuweza kunipa msingi imara katika kweli. Hali mwanamume mzee, anayeanza tu kujifunza kusoma, na mkewe mzee, kidogo kiziwi, walikuwa wameweza kuniarifu kile ambacho mume wangu alikuwa ameshindwa kufanya kwa muda huo wote.
“Sasa nimekwisha weka maisha yangu wakf kwa Mungu nami nawasaidia wengine wajifunze njia ya kweli kutoka kwa Neno lake lililoongozwa na roho yake.”
Ikiwa nawe umekuwa ukijifunza Biblia na mashahidi wa Yehova au unajifunza makusudi ya Mungu kwa kutumia vitabu vyao, je! unaiona haraka ya kuwasaidia wengine wajifunze uliyokwisha jifunza? Uzee, kutoweza kusoma kwa ufasaha, uziwi ujana, madaraka ya jamaa—hakuna mojawapo la haya lililo kizuizi kisichoweza kushindika. Je! wewe utalijibu ulizo “Nani awezaye kusaidia?” kihodari, ukisema “Mimi naweza”?