Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 3/1 kur. 119-120
  • Uzee Si Kizuizi cha Kujifunza Kweli ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uzee Si Kizuizi cha Kujifunza Kweli ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Habari Zinazolingana
  • Mwishowe Mbegu Ilichipuka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Aliazimia Aishi Kulingana na Viwango vya Adili za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kondoo wa Yesu Husikiliza Sauti Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • ‘Kutokana na Yaujazayo Moyo’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 3/1 kur. 119-120

Uzee Si Kizuizi cha Kujifunza Kweli ya Biblia

MARA nyingi watu wazee wanatoa maoni ya kwamba wao ni wazee mno wasiweze kujifunza mambo mapya. Lakini, hata watu wenye umri wa miaka 80 wamefanya mageuzi katika jambo lililo la maana zaidi la maisha yao, yaani, katika ibada yao ya Mungu. Uzee, pamoja na vizuizi, haukuwazuia wasijifunze kweli ya Biblia kama inavyofundishwa na mashahidi wa Yehova wa Kikristo.

Kwa mfano, kunacho kisa cha mwanamke mzee wa Yugoslavia anayeishi katika Austria. Hakuzungumza Kijeremani safi na aliisoma lugha hii kwa shida. Nyumba yake ilijaa picha za “watakatifu.” Lakini yeye alikuwa mnyofu sana na akakubali kujifunza Biblia na mmoja wa mashahidi wa Yehova. Kwanza ilichukua nusu saa kumaliza fungu moja tu katika kitabu kilichotumiwa kwa funzo, kwa maana ilikuwa lazima afunzwe kusoma Kijeremani.

Ijapokuwa si habari nyingi iliyomalizwa wakati wa kila funzo, mwanamke huyu mzee kwa wazi alikuwa akifaidika. Kupendezwa kwake kuliamshwa vya kutosha kuweza kumsukuma ahudhurie mikutano ya mashahidi wa Yehova. Hii ilitaka jitihada nyingi kwa upande wake. Ilimpasa atembee kwa saa moja na nusu kusudi afikie kituo cha bas kilichoko karibu zaidi na kutoka hapo asafiri karibu maili tano kwenye Jumba la Ufalme. Aliyojifunza mwanamke huyu mzee kutoka kwa Biblia vile vile yalimharakisha awaharibu “watakatifu” wake, aachane na ukamatano wake na siasa na ushirikiano wote na Kanisa la Kirumi la Katoliki, vile vile kuacha kuvuta sigareti. Ijapokuwa mwenye umri wa miaka 82, ameufanya uamuzi wake kushiriki kweli ya Biblia na wengine na kubatizwa.

Katika Bolivia, mke wa mmojawapo wa wahudumu wanaosafiri wa mashahidi wa Yehova alimtembelea mwanamke mwenye umri wa miaka 81 aliyekuwa anasoma Biblia yake ya Kikatoliki. Alipoulizwa kama angependa kuifahamu Biblia, mwanamke huyu mzee alijibu: ‘Kabisa. Kwa miaka mingi nimekuwa nikiisoma Biblia kama kasuku. Ningependa kufahamu inachosema.’

Funzo la nyumbani la Biblia likaanzwa. Wakati wa kipindi cha siku tatu mafunzo yaliongozwa na mke wa mhudumu anayesafiri. Nyuma ya kuondoka kwake pamoja na mumewe kuelekea mahali pengine, mtu mwingine aliendelea kuliongoza funzo. Siku nane tu nyumaye yule mwanamke mzee alizichoma picha zake zote za kidini, akaziharibu sanamu zake, na akamwarifu padre wa mahali pake kwamba yeye alikuwa mmoja wa mashahidi wa Yehova sasa na hakutaka tena ajulikane kama Mkatoliki. Ameanza kuwasimulia wengine mambo aliyojifunza naye anaihudhuria mikutano yote ya mashahidi wa Yehova.

Mwanamke mwenye umri wa miaka 81 katika Ufaransa alifanya maendeleo ya kasi kasi yanayofanana na hayo. Wakati wa mwezi wake wa kwanza wa kujifunza Biblia na mashahidi wa Yehova alichoma kibweta cha vitabu vyenye habari ya mazoea ya kichawi. Vile vile aliharibu nishani 34 za kidini, sanamu, tasbihi yake na msalaba, aliokuwa anajiwekelea hapo kwanza kusudi umlinde na ulozi. Miezi mitano nyuma ya funzo la kwanza alianza kuhudhuria mikutano yote ya mashahidi wa Yehova. Kisha akaanza kushiriki katika huduma ya mlango kwa mlango na nyumaye akabatizwa.

Katika nchi ya Amerika ya Kati Shahidi alipanga kujifunza Biblia na mwanamke mwenye umri wa miaka 84. Shahidi akajisemea mwenyewe. ‘Ni faida gani itakayotokana na hili? Yeye hawezi hata kusoma naye mkwewe anapinga.’ Lakini, penye funzo la pili watu watatu zaidi walikuwapo na nyumaye walihudhuria kufikia kumi na wanne. Kwa sababu ya kupinga kwa mkwewe, mwanamke huyo alijikodishia chumba na kumwambia Shahidi: ‘Sasa mkwe wangu aweza kukasirika kama atakavyo, lakini hawezi kuzuia funzo letu katika nyumba yangu.’ Alipoulizwa alilofanya hata watu wengi namna hiyo wakajiunga katika funzo, alijibu: ‘Basi, tunalojifunza ni zuri sana hivyo kwamba, kusudi nisilisahau, nawafikia jirani zangu mara tu uondokapo na kuwaambia nilichojifunza.’

Tangu funzo la tatu mwanamke huyu mzee alianza kuhudhuria mikutano ya mashahidi wa Yehova kwa kawaida, sikuzote akienda pamoja na wanaopendezwa. Ijapokuwa ilimpasa ajitegemeze mwenyewe kwa habari ya fedha, yeye ni mtangazaji mwenye bidii wa ujumbe wa Biblia. Sasa, kama Shahidi aliyebatizwa wa Yehova, yeye, katika umri wa miaka 86, anasema: ‘Mimi najifunza kusoma na kuandika. Tamaa yangu iliyo kubwa zaidi ni kujisomea mwenyewe Neno la Mungu kusudi niwaambie watu mengi zaidi juu ya Baba yetu, Yehova.’

Lo! maneno ya Yesu ni ya kweli kama nini: “Kondoo wangu waisikia sauti yangu”! (Yohana 10:27) Kwa kweli uzee hauwazuii watu wenye mioyo ya haki kutoiitikia kweli iliyowekwa katika Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki