Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 6/1 kur. 261-262
  • ‘Kutokana na Yaujazayo Moyo’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Kutokana na Yaujazayo Moyo’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Habari Zinazolingana
  • Mwishowe Mbegu Ilichipuka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Uzee Si Kizuizi cha Kujifunza Kweli ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Kutoka Mshuko wa Moyo Hadi Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Waambie Unawapenda
    Masimulizi ya Mashahidi wa Yehova
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 6/1 kur. 261-262

‘Kutokana na Yaujazayo Moyo’

KWA kawaida wanadamu hawawezi kujiwekea habari njema wenyewe bila kuwaambia wengine, sivyo? Wanajiona kulazimika kuwaambia wengine. Hii ndivyo ilivyo hasa wakati ambapo habari njema zinaweza kuwa baraka ya kweli kwa wasikiaji. Ndiyo sababu mashahidi wa Yehova wa Kikristo wanavutwa washiriki kweli ya Biblia na wengine, mioyo yao ikiwa imejawa na shukrani kwa ahadi bora za Mungu. Ni sawa na Yesu Kristo alivyosema: ‘Kutokana na yaujazayo moyo kinywa husema.’​—Luka 6:45.

Kwa sababu ya kutumia vema nafasi zinazojitoa katika maisha ya kila siku kuzungumza Maandiko, Mashahidi wengi wamepata furaha ya kuona wengine wakisimama upande wa ibada ya kweli.

Kwa mfano, Shahidi mmoja alikuwa akinunua vitu katika soko lenye kusongamana na watu katika California. Katika meza ya nyama mwanamke aliyekuwa karibu naye akasema hivi: “Lo! bei ya nyama imepanda sana. Sioni mtu mwenye jamaa awezaje kununua nyama.” Shahidi akajibu: “Jamaa nyingi sana haziwezi. Wengi wana njaa leo.” Mwanamke huyo akakubali akasema kwamba mambo yalikuwa yanaharibika sana hata hakujua mwisho wayo ungekuwa wakati gani. Akieleza juu ya lililotukia baadaye, Shahidi huyo anaandika hivi:

“Nilimwambia watu wengi wanaona ivyo hivyo nao wana wasiwasi sana juu ya wakati ujao. Tulizungumza uhakika wa kwamba zijapokuwa jitihada za wanadamu mambo hayawi mazuri zaidi bali yanaendelea kuharibika.

“Nikaendelea kusema hivi: ‘Sijui kama wewe wasoma Biblia yako sana, lakini mimi nasoma yangu wakati wote. Kulingana na maneno ya Yesu, nyakati hizi zenye hatari zinatimiza unabii wa Biblia. Hali hazitakuwa nzuri zaidi, bali zitaharibika hata zaidi.’ Akawaza kidogo, kisha akasema, ‘Mimi nimejaribu kusoma Biblia yangu, lakini siwezi kuifahamu hata.’ Nikamwambia pengine ni kwa sababu Biblia nyingi zimeandikwa kwa Kiingereza cha kale nasi hatuzungumzi namna hiyo siku hizi. Ndiyo sababu mimi nimejipatia Biblia iliyoandikwa katika Kiingereza cha kisasa.

“Akauliza kama mtu ye yote angeweza kuinunua Biblia hiyo. Nikamwambia kama angependa kupata moja, mimi nilikuwa na moja ya ziada katika gari langu na kwamba ningemruhusu aipate. Akapendezwa sana na kusema angengoja ninapokwenda garini nikaichukue. Nilipofika garini nikakuta nilikuwa nimekwisha angusha nakala yangu ya mwisho.

“Nikakumbuka kwamba Shahidi mwingine aliishi karibu majumba matatu hivi kutoka duka hilo. Kwa hiyo mwendo wote nilipokuwa nikielekea nyumbani kwake nikawa nikisali awe na Biblia. Naye alikuwa nayo.

“Kwa kuwa ilichukua muda mrefu zaidi kuliko nilivyotazamia, kwa kweli sikudhani mwanamke huyo angekuwa dukani bado niliporudi. Lakini yeye alikuwa akingoja pale pale nilipokuwa nimemwacha. Nikamsomea 2 Timotheo 3, Mathayo 24 na Luka 21. Watu walikuwa wakisukuma mikokoteni hapa na hapa tulipokuwa tunaisoma Biblia. Kisha akasema anatamani angejua Biblia yake kama mimi. Kwa hiyo nikamwuliza kama angependa kuniruhusu nije nyumbani kwake nimsaidie kuifahamu Biblia. Akanipa anwani yake, nami nikapanga mipango kufika nyumbani kwake.”

Funzo la nyumbani la Biblia lilianzwa na mwanamke huyu. Leo, akiwa shahidi aliyebatizwa wa Yehova, yeye mwenyewe anasema kwa wengine juu ya tumaini lake lenye msingi wa Biblia. Kwa kweli kuna sababu nzuri kutumia kila nafasi kushiriki ujumbe wenye kufariji wa Biblia pamoja na wengine. Je! moyo wako unakuvuta ufanye hivyo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki