Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 12/15 kur. 575-576
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Habari Zinazolingana
  • Unaweza Kuyavunja Mazoea ya Tumbako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Mungu ana maoni gani kuhusu Kuhusu Kuvuta Sigara?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Sigareti—Je, Wewe Huzikataa?
    Amkeni!—1996
  • Imarisha Azimio Lako
    Amkeni!—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 12/15 kur. 575-576

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Kwa kuwa mashahidi wa Yehova wanaona kuvuta sigara kama kwenye kutofautiana na mazoea ya Kikristo, je! wao wanazuia watu wengine wasivute sigara wanapokuja nyumbani kwao au biasharani?​—U.S.A.

Lo lote Mashahidi mmoja mmoja watakaloamua katika habari hii ni shauri la kipekee litakaloongozwa na dhamiri yao iliyozoezwa na Biblia.

Walakini, kwa ujumla mashahidi wa Yehova wanapendelea mtu ye yote asivute sigara katika nyumba zao. Kwa njia hii wanalinda afya ya jamaa zao na kuzuia nyumba zao zisichafuliwe na mnuko wa tumbako. Halafu, tena, kwa kuwa mashahidi wa Yehova wanahangaikia kusaidia wengine ‘wajitakase nafsi zao na uchafu wote wa mwili na roho,’ je! ingepatana kwao kuruhusu uvutaji wa ovyo ovyo katika nyumba zao? (2 Kor. 7:1) Wakifanya hivyo, je! isingeonyesha wengine kwamba hawaoni kuvuta sigara kama jambo baya sana?

Wageni wanapopashwa habari kwa upole juu ya maoni ya mashahidi wa Yehova, kwa kawaida wanaheshimu matakwa ya mwenye nyumba. Lakini ikiwa wamezoelea tumbako mno hata wanaona lazima kabisa wavute sigara, wanaweza kuvutia sigara mahali pasipoudhi na kudhuru wengine sana. Ni juu ya Mashahidi mmoja mmoja kuamua watapanga au kuruhusu nini katika habari hiyo, na hii ingeongozwa na kama kichwa cha jamaa ni Shahidi.

Katika mahali pa biashara ni jambo la kawaida kuona vibao vya kusema “Usivute Sigara.” Bila shaka, inawezekana sheria ya nchi isikataze kuvuta sigara waziwazi mahali fulani pa biashara, na wavuta sigara wanaweza kutazamia kufanya zoea lao wanapongoja watumikiwe. Kwa kuwa Mkristo anatoa utumishi wa kipekee kwa wote wanaoweza kumjia, hawezi kujiona kwamba yumo katika hali ya kuweka sheria kwa wenye kumfikia. Yeye anajua kwamba yumo ulimwenguni na kwa hiyo hawezi kuepuka asikutane na watu wenye mazoea asiyoyakubali. (1 Kor. 5:9, 10) Kwa sababu hii, wengine wa mashahidi wa Yehova wanaweza kuamua kwamba hali zinawazuia wasikataze kuvuta sigara mahali pao pa biashara. Kwa hiyo, wanaweza kujiona wanalazimika kuweka vyombo vya kutilia majivu ya sigara kwa watu wavutao wanaowafikia, Walakini, Mashahidi wengine wanaweza kuamua kuweka kibao kinachoomba kusiwe na kuvuta sigara ko kote. Wanaweza kuwaza kwamba hii itafanya mambo yawe yenye kupendeza zaidi kwao wenyewe na watu wengi wasiovuta sigara wanaokuja mahali pao pa biashara mara kwa mara.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki