Kutumia Kanuni za Biblia Kuliokoa Ndoa
MKE wa afisa wa polisi katika Massachusetts alianza kujifunza Biblia na mashahidi wa Yehova, lakini mumewe alianza kupinga. Walakini, baada ya kupindi cha kutengana alikubali kujifunza Biblia akitumainia kuiokoa ndoa yake. Lakini maafisa aliokuwa akifanya kazi nao wakaanza kumfanyia mzaha. Kwa sababu hii na mikazo mingine aliacha kujifunza. Karibuni alizirudia njia zake za zamani—kunywa kupindukia na kuwa na magumu mengi nyumbani. Hii ilileta mtengano mwingine.
Juu ya lililotokea baadaye, yeye anasimulia hivi: “Baada ya muda fulani mke wangu alinipasha habari kwamba alikuwa akitaka kuomba talaka, naye alikuwa na sababu za Maandiko na za halali kufanya hivyo. Kwa kuwa nilikuwa na watoto sita nami nilipendezwa sana nao na mke wangu, sikutaka talaka. Nilimwita Shahidi aliyejifunza nami Biblia hapo kwanza nikamwuliza kama angejifunza nami tena.”
Kwa sababu ya mwanamume huyu kutumia aliyokuwa akijifunza, mkewe alianza kuona kwamba yeye alikuwa akibadili njia zake kweli. Kwa hiyo, alipoulizwa na mumewe kama wangeweza kujaribu tena, alimkubali tena. Wote wawili wameungana sasa katika kujenga maisha yenye furaha ya jamaa kulingana na kanuni zipatikanazo katika Neno la Mungu