Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 1/15 kur. 47-48
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Habari Zinazolingana
  • Tumaini la Ufufuo Lina Nguvu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Dhambi
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Kuondoa Doa la Dhambi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Kitabu Kinachotegemeka—Sehemu ya 7
    Amkeni!—2011
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 1/15 kur. 47-48

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Kwa sababu gani vitabu vya Watch Tower vinataja mamlaka saba za ulimwengu tu, hali kwa wazi zilikuwako falme nyingine zenye uwezo mwingi karne zote?​—U.S.A.

Vitabu vya Watch Tower havikosi kufuata kanuni kwa kutaja mamlaka saba tu za ulimwengu. Vinafanya hivyo kulingana kabisa na habari zinazozunguka za Biblia wala si kwa njia ya juujuu tu au ya kilimwengu. Kitabu cha Biblia cha Ufunuo kinataja waziwazi “wafalme saba.” Katika Ufunuo 17:10 twasoma hivi: “Navyo ni wafalme saba. Watano wamekwisha kuanguka, na mmoja yupo, na mwingine hajaja bado.”

Kwa wazi, katika karne zote wametawala zaidi ya “wafalme” halisi saba. Kwa hiyo “wafalme” saba wanaotajwa hapa bila shaka wanasimamia falme fulani au milki, ya sita ikiwa ilitawala wakati mtume Yohana alipoyaandika maneno hayo. Kitabu cha Danieli chafunua majina ya tatu za milki hizi​—Babeli, mamlaka ya mwungano ya Umedi na Uajemi, na Ugiriki. (Linganisha Danieli 2:37-45; 7:1-7; 8:20, 21.) Mamlaka zote tatu hizi zilizo kuu zilishughulika moja kwa moja na watu wa kale wa Mungu wa agano, Waisraeli.

Tukiwa na dokezo hili kutoka katika kitabu cha Danieli, twaweza kuwatambua wale “wafalme” wengine kati ya saba waliotajwa katika Ufunuo 17:10. Bila shaka ni falme kuu zilizokuwa na shughuli za moja kwa moja ama na watu wa Mungu wa kale wa agano au na taifa lake mpya la Israeli wa kiroho, lililofanyizwa na wanafunzi waaminifu wa Yesu Kristo. (Rum. 2:28, 29; Gal. 6:16) Kabla Babeli haijauharibu Yerusalemu na kuiacha ukiwa nchi ya Yuda, falme nyingine mbili zilizo kuu zilitumia maongozi yenye nguvu juu ya Waisraeli. Wa kwanza, Misri, uliwatumikisha miaka mingi, na wa pili, Ashuru, uliuharibu ufalme wa makabila kumi wa Israeli na pia ukaacha miji mingi ya Uyahudi ukiwa. Baada ya Babeli, Uajemi ulitawala Uyahudi mpaka utawala wa Kigiriki ulipouondoa ule wa Uajemi; na baadaye Rumi ukawatawala Wayahudi.

Kwa hiyo, wafalme watano waliokuwa ‘wameanguka’ wakati mtume Yohana alipouandika Ufunuo (karibu 96 C.E.) walikuwa: Misri, Ashuru, Babeli, Umedi-Uajemi na Ugiriki. Mamlaka ya ulimwengu iliyokuwa ikitawala wakati huo ilikuwa ile ya Rumi. Kwa habari ya yeye ambaye angekuja, Mamlaka ya Ulimwengu ya Waingereza na Waamerika inatokeza zaidi sana kati ya zile zilizotumia uwezo mkuu tangu siku za Rumi ya kale. Nayo historia yashuhudia kwamba, wakati wa Vita za Ulimwengu za Kwanza na Pili, Mamlaka ya Ulimwengu ya Waingereza na Waamerika iliwapinga sana walio Waisraeli wa kiroho.a

[Maelezo ya Chini]

a Kwa maelezo mengi, tazama kitabu “Your Will Be Done on Earth,” kurasa 179 mpaka 182, na Awake! la Desemba 8, 1970, kurasa 20-23.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki