Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 7/15 uku. 336
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Mungu Ameruusu Uovu Yetu ya Leo?
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Mjue Adui Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Watawala Katika Makao ya Roho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Shetani
    Amkeni!—2013
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 7/15 uku. 336

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Zaburi 5:4 (NW) inasema hivi juu ya Yehova, “Hakuna mtu mbaya ye yote anayeweza kukaa wakati wo wote pamoja na wewe.” Basi, sababu gani Yehova alimruhusu Shetani abaki mbinguni kwa maelfu ya miaka na hata kuingia katika kuwapo Kwake wakati fulani?​—U.S.A.

Maneno yanayozunguka mstari huo yanaonyesha wazi kwamba Shetani ‘hakukaa’ pamoja na Yehova Mungu katika maana inayomaanishwa na mtunga zaburi Daudi. Katika zaburi ya tano, Daudi alionyesha matumaini kwamba Yehova alikuwa na nia ya kusikiliza sala yake. Halafu, akitoa sababu yake ya matumaini haya, Daudi anaonyesha haki ya Mungu, akisema hivi: “Kwa maana wewe si Mungu anayefurahia uovu; hakuna mtu mbaya ye yote anayeweza kukaa wakati wo wote pamoja na wewe.” (Zab. 5:3, 4, NW) “Kukaa” hivyo na Mungu kuna maana ya kuwa mgeni anayekubaliwa katika nyumba yake au hekalu lake takatifu. (Linganisha Zaburi 15:1-5.) Hii ni wazi kutokana na maneno ya Daudi ya baadaye. Akitofautisha hali yake mwenyewe na wazoeao mabaya, wasioruhusiwa “kukaa” pamoja na Yehova, yeye anasema hivi: “Kwa habari yangu mimi, katika wingi wa fadhili zako za upendo nitaingia nyumbani mwako, nitainama kuelekea hekalu lako takatifu kwa kukuogopa wewe.”​—Zab. 5:7, NW.

Shetani Ibilisi aliruhusiwa aendelee kuwako mbinguni kwa maelfu ya miaka na nyakati nyingine (kwa wazi kwa sababu fulani) aliruhusiwa aweko katika kusanyiko la wana wa Mungu. (Ayubu 1:6, 7; 2:1) Lakini ni kwa sababu tu ya ulizo la adili lililopaswa litatuliwe kwamba Yehova Mungu alimvumilia Shetani aweko mbinguni. Kama inavyoonekana wazi kutokana na kitabu cha Ayubu, Shetani alishikilia kwamba viumbe vyote vyenye akili vilikuwa vikijitafutia faida yao vyenyewe navyo vingekuwa visivyoaminika kwa Mungu kama visingepata faida tena ya kimwili au ya kipekee kutokana na kumtii Yeye. (Ayubu 2:4, 5) Ili ulizo hili la maana katika ulimwengu wote litatuliwe, Yehova Mungu alimruhusu Shetani ajaribu kuhakikisha dai lake. Hii ilimruhusu Shetani atumie maongozi yake kujaribu kushawishi wana wengine wa kimalaika wadai wawe wenye kujitegemea, kwa njia hiyo akiwatia katika jaribu la uaminifu wao kwa Mungu.

Malaika wengi wakawa wasioaminika. Lakini wasioaminika hao wote walipoteza vyeo vyao vya amana na madaraka, ingawa bado walikuwa na ruhusa kuingia mbinguni. Wakashushwa, wakawekwa chini ya kizuizi na kunyimwa mwangaza zaidi wa kimungu. Hali hii inazungumzwa kwa usemi wa mfano katika Yuda katika Yuda 6: “Malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.”

Hivyo malaika hawa wasioaminika walifukuzwa watoke katika jamaa ya Mungu ya viumbe vya kiroho vilivyo viaminifu. Wao wala mtawala wao, Shetani, hawakuendelea kukaa pamoja na Yehova Mungu kwa njia ambayo walikuwa wamefurahia wakiwa wana wake watiifu. Ingawa walikuwa na ruhusa ya kuingia katika makao ya kimbinguni, sasa walikuwa watupwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki