Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 9/1 kur. 387-388
  • Kitabu cha Wanadamu Wote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kitabu cha Wanadamu Wote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Habari Zinazolingana
  • Unaweza Kupata Amani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Unaweza Kupata Wapi Uongozi?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Je, Biblia Ni Kitabu cha Wazungu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Ulimwengu Usio na Vita U Karibu
    Amkeni!—1996
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 9/1 kur. 387-388

Kitabu cha Wanadamu Wote

WEWE ungetazamia nini kwa kitabu ambacho ni cha wanadamu wote? Bila shaka ingekipasa kipatikane katika lugha zote kuu. Ujumbe wacho wapaswa uwe wenye maana kwako, kukuwezesha ufaidike na maisha hata sasa. Je! kuna kitabu kama hicho kweli?

Ndiyo, kiko. Ni kitabu cha kale sana ambacho kimefika kwenye kila nchi na hata kwenye visiwa vya mbali. Chaweza kupatikana katika nyumba za kawaida za kienyeji na katika nyumba za kisasa. Kitabu chenyewe kimetafsiriwa, chote au nusu, katika lugha kubwa na ndogo zaidi ya 1,525, hivyo karibu kila mtu aweza kukisoma katika lugha yake mwenyewe. Hakuna hata kitabu kingine kiwezacho kuenezwa pote kama hicho. Kila mwaka mamilioni na mamilioni ya nakala yanaenezwa duniani pote. Kitabu hicho ndicho Biblia.

Lakini je! kitabu hiki chaweza kweli kukusaidia ufaidike na maisha sasa? Mamilioni ya watu leo wanasadiki kwamba hii haingeweza kuwa hivyo. Wanaihukumu Biblia kwa wanavyojua juu ya wale wanaodai kuifuata. Wanashangazwa na matendo yenye aibu ambayo Jumuiya ya Wakristo imefanya kwa namna ya vita vyenye kuogofya, kupendelea, chuki, kuonea na kutumia wengine kwa faida yao. Wanawaza kwamba, ikiwa hivi ndivyo watu na mataifa yaliyo na Biblia wanafanya, hawataki kuwa sehemu yake.

Walakini, kama ujuavyo, kuwa na kitabu tu hakumaanishi kwamba mtu aliye nacho anafuata kanuni zilizomo. Watu wengi wanavyo vitabu katika maktaba zao vinavyofundisha mawazo ambayo wao hawaungi mkono. Je! hivi sivyo ingeweza kuwa pia na mamilioni yaliyo na Biblia?

Matengenezo mengi ya kidini yanayojidai kuwakilisha Biblia yaliunga mkono sana vita vikali vya karne hii ya 20. Je! yaliungwa mkono na Biblia katika kufanya hivi? Huenda wengine wakajaribu kutetea mwendo wao, wakielekeza kwenye vita vinavyotajwa katika Biblia. Kweli, Mungu alitumia watu na mataifa fulani wafanye vita juu ya mataifa mengine ili kutekeleza hukumu yake juu yao kwa sababu ya uovu wao. Lakini hakuna watu au mataifa leo yawezayo kudai kwamba wametumiwa katika njia hiyo.

Biblia inalaumu vikali wale wanaofanya vita vya kichoyo. Tunasoma hivi:

“Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu? Mwatamani, wala hamna kitu; mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi! Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.”​—Yak. 4:1-3.

Kwa habari ya kufanya vita, mara nyingi yanayosababisha ni maoni ya kwamba taifa au kabila fulani ndilo bora kuliko mengine. Je’ Biblia inaunga mkono maoni hayo? Hata, inaonyesha kwamba jambo ambalo Mungu anaona kuwa lenye maana si cheo cha mtu, taifa au kabila la mtu, bali namna mmoja alivyo kama mtu. Ebu angalia maneno haya ya waziwazi ambayo Biblia inasema: “Mungu hana upendeleo; bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.” (Matendo 10:34, 35) “Alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja.”​—Matendo 17:26.

Vile vile, Biblia haiungi mkono wale ambao wameonea na kutumia wanadamu wenzao kwa faida yao wenyewe. Tunaona maneno haya wakiambiwa waonezi na wenye kunyonya wengine hivi:

“Lieni na kuombolezea msiba unaoshuka juu yenu. Mali zenu zimeoza; mavazi yenu mazuri yameliwa na nondo; fedha yenu na dhahabu yenu zimeota kutu, na kutu yazo yenyewe itakuwa ushuhuda juu yenu na kula nyama yenu kama moto. Mmelundika mali kwa wingi katika kizazi kinachokaribia mwisho wake. Ile mishahara ambayo hamkuwalipa kamwe watu waliokata majani ya mashamba yenu inawapazieni sauti, nacho kilio cha wavunaji kimeyafikia masikio ya Bwana wa Majeshi. Mmeishi duniani kwa anasa isiyozuiwa, mkijinenepesha kama ng’ombe​—na siku ya kuchinjwa imekuja.”​—Yak. 5:1-6, New English Bible.

Njia ya maisha inayoshauriwa katika Biblia ni ile ya upendo, kupendezwa bila choyo na hali njema ya wanadamu wenzetu. “Msimkope mtu cho chote,” inashauri, “isipokuwa wajibu wa kupendana, kwa maana ye yote anayependa wanadamu wenzake ameitosheleza sana Sheria. Kwa maana amri hizi, ‘Haikupasi ufanye uzinzi, Haikupasi uue, Haikupasi uibe, Haikupasi utamani, na amri nyingine zo zote zilizoko, zote zajumlishwa katika usemi mmoja, ‘Inakupasa umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’”​—Rum. 13:8-10, An American Translation.

Bila shaka ungefaidika ikiwa watu walio katika mtaa wako, kijiji au mji wako wangejitahidi kufuata shauri hili bora. Je! wewe hungejiona salama zaidi sana katika nyumba yako? Je! isingekuwa faraja kuweza kuishi katikati ya watu wasioshiriki katika udanganyifu, unyang’anyi, wizi au kuharibu mali za watu? Halafu, tena, wale wanaoonyesha upendo wa kweli kwa jirani ni wenye furaha zaidi wenyewe. Hawana husuda na wivu unaotokana na kutaka mali za wengine. Hawapatwi na masikitiko na maumivu ya watu wasiooa au wasioolewa na wale waliooana wanaojaribu kutosheleza nyege zao bila mpango wa ndoa. Wanaepuka magonjwa yenye kuchukiza sana ya kaswende na kisonono, mimba zinazochukuliwa pasipo mpango wa ndoa, na jamaa zenye kufarakana.

Ijapokuwa faida za wazi zinazotokana na kuonyesha upendo ambao Biblia inashauri, watu wengi hawataki wabadili njia zao. Hili laweza kukutatiza na huenda kukushawishi ufuate maoni yao ya kichoyo. Lakini huko kusingefanya mambo yawe mazuri zaidi, sivyo?

Ingawaje, huenda wengine wakawaza hivi: “Sababu gani nijifunze Biblia? Mimi simwumizi ye yote. Najaribu kufanya yaliyo mema.”

Labda umewasikia wengine wakisema sawasawa kama hivyo. Lakini je! isingekuwa bora kuchunguza kama Biblia ingeweza kukusaidia uone furaha kubwa zaidi katika maisha? Mamilioni ya wanaume na wanawake wenye akili wanasadiki kwamba Biblia inatoa uongozi ulio bora kwa maisha. Je! wanasema kweli? Je! Biblia ni kitabu kilichotungwa tu na watu wa kale wenye hekima, au yatokana na chanzo cha juu zaidi kuliko wanadamu? Je! yaweza kukusaidia ufaidike na maisha sasa na kujipatia mwenyewe na wapendwa wako wakati ujao ulio salama?

[Blabu katika ukurasa wa 388]

Biblia yafundisha hivi: “Mungu hana upendeleo; bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.”​—Matendo 10:34, 35.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki