Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 10/15 uku. 476
  • Kupata Mali Yenye Thamani Zaidi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kupata Mali Yenye Thamani Zaidi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • “Umtazame Mtu Mnyofu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Sisi Hatukuahirisha Mambo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Faida Zenye Kudumu Kutokana na Kuifuata Biblia Kama Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Je, Mashahidi wa Yehova Wanavunja Ndoa za Watu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 10/15 uku. 476

Kupata Mali Yenye Thamani Zaidi

WANAUME na wanawake wengi sana wanaona kwamba kuna mali yenye thamani zaidi kuliko mali zote za kimwili. Wanapoipata mali hiyo maisha zao zinakuwa nzuri, wanapata furaha na uradhi usioweza kununuliwa na pesa. Mali hiyo ni nini?

Ni uhusiano mwema na Muumba, unaotegemea kuwa na maarifa sahihi ya mapenzi yake na kuishi kupatana nayo. Wale ambao wameupata uhusiano huo wanaufurahia sana hata wanatia bidii kuwapa wengine maarifa ambayo wamepata.

Wengine hata wameacha faida za kimwili ili kuwa na wakati zaidi na kufahamisha wanadamu wenzao mali ambayo wameona ndiyo yenye thamani zaidi. Ndivyo alivyofanya fundi wa umeme aliyekuwa akifanyia kazi Hitachi Manufacturing Company katika Japan. Asimulia jinsi jambo hilo lilivyotukia:

“Nilisafiri Japan yote nikiwa kazini, na mara nyingi nilikwenda nchi za ng’ambo, Iran na United States. Katika safari moja nilikwenda na mke wangu, tukakaa katika chumba kimoja katika Placerville, karibu na Sacramento, California. Hapo ndipo mmoja wa Mashahidi wa Yehova alipotutembelea, nasi tukakubali kuchukua nakala za magazeti Mnara na Mlinzi na Awake! Kwa sababu hatukujua Kiingereza kingi, hatukuyasoma sana.

“Muda mfupi baadaye tulirudi kuishi katika chumba cha shirika katika Mji wa Hitachi, Japan. Muda mfupi tu baada ya kufika nyumbani mke wangu alitembelewa na mtu akamwonyesha magazeti yale yale mawili​—yaani, jalada za magazeti zilikuwa zile zile, lakini vichwa vya habari viliandikwa katika Kijapan. Jambo hilo lilimwonyesha mke wangu papo hapo kwamba Mashahidi wa Yehova wanafanya kazi yao katika mataifa yote. Mke wangu alikubali kwa furaha kuyachukua magazeti hayo. Shahidi huyo Mjapan alitutembelea mara nyingi, na karibuni mke wangu akawa akijifunza Biblia kwa kawaida na Shahidi huyo mwanamke.”

Baadaye, mume pia alianza kujifunza akawa mwenye shauku kama mkewe. Wote wawili waliendelea kufanya maendeleo hata wakabatizwa katika kusanyiko la mzunguko la Mashahidi wa Yehova katika Adachi, Tokyo.

Kwa sababu ya kuthamini jinsi maarifa sahihi ya Biblia yalivyokuwa yamewafaidi, mume pamoja na mkewe walitaka kutumia wakati mwingi iwezekanavyo wakisaidia wengine wapate maarifa hayo. Walitaka kuwa “mapainia,”wakitumia saa zisizopungua 100 kila mwezi kuhubiri wengine na kuwafundisha kweli za Biblia, zaidi ya kutunza kivulana wao mdogo. Lakini, mume alijua kwamba akiendelea na kazi yake ya wakati wote katika Hitachi Manufacturing Company asingeweza kuwa “painia.” Kwa hiyo alifanya nini? Aendelea kusema:

“Nilijiuzulu katika shirika letu. Mke wangu nami tukawa waalimu wa kujiandika, tukawa tukifundisha watoto watano au sita wenye kuhudhuria madarasa ya chini ya masomo ya juu wakati wa jioni nyingi. Badala ya sisi kuwatembelea wazazi, wao ndio walioanza kututembelea, wakatuomba tufundishe watoto wao. Baada ya muda mfupi tukawa tukifundisha watoto zaidi ya 20. Julai 1972 nikawa painia wa kawaida naye mke wangu akanifuata Mei 1973. Ingawa ilitulazimu kuondoka katika nyumba tuliyokuwa tumepewa na Hitachi Company, tuliweza kupata nyumba nzuri sana katika Mji wa Hitachi, yenye vyumba viwili vya kulala na vifaa vingine vyote, kwa kiasi cha $11 (shilingi karibu 90) tu kwa mwezi. Kwa kula kiasi vyakula vyenye kulisha mwili, hatutatizwi kuendelea kumtumikia Yehova wakati wote.”

Kwa habari ya matokeo ya utendaji huo juu ya mwana wao, mume asema hivi: “Kivulana wetu wa miaka minne, Shinya (linalomaanisha, ‘Ni Kweli’), apenda utumishi kuliko mambo mengine yote. Hata nyakati za asubuhi mvua inapokunya sana, Shinya hupaza sauti akisema, ‘Ikitai! Ikitai’ (‘Nataka kwenda! Nataka kwenda!’) Kwa hiyo tunakwenda. Halafu kila alasiri tunaongoza mafunzo ya Biblia na kurudia watu wenye kupendezwa katika wilaya moja tu ili kuhifadhi mafuta ya gari, kisha tunakutana tena nyuma ya gari wakati ufikapo wa kwenda nyumbani. Kwa kawaida Shinya huenda nami, kwa hiyo inawezekana nitembelee wanawake ambao huenda wakaona haya nikienda peke yangu.”

Mtu huyo aliyekuwa fundi wa umeme anafurahia pamoja na mke wake mambo wanayofanya sasa. Asema: “Nimeona kwamba mojawapo mambo yanayonifurahisha zaidi ni kwamba sina wasiwasi wa kushirikiana mchana kutwa na watu wenye mawazo ya ulimwengu tu. Muda mwingi sasa tunashirikiana na Wakristo wenzetu wanaotaka sana kusaidia watu wengine wapate maarifa sahihi ya Biblia, na watu wanaopenda haki wanaojifunza nasi. ‘Kupainia’ kumeipa jamaa yetu furaha halisi!”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki