Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 2/1 uku. 19
  • Je! Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Unakumbuka?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Je, Unakumbuka?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 2/1 uku. 19

Je! Wakumbuka?

Umesoma matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi kwa uangalifu? Ikiwa ndivyo, bila shaka utayakumbuka mambo haya:

● Yehova Mungu anawavutaje watu mmoja mmoja waje kwake?

Anafanya hili kwa kuwawezesha kusikia juu ya mpango wake wa wokovu kupitia kwa Yesu Kristo. Kisha Aliye Juu Zaidi anawawezesha watu hao mmoja mmoja wasitawishe kuthamini faida kuu zinazotokana na kuwa na umoja na Mwanawe.​—10/15 uku. 14.

● Ni mambo gani yanayoamua kama mtu aweza kumkaribia Mungu kwa sala na kukubaliwa naye?

Lazima mtu amkaribie kwa unyofu wa moyo, kupatana na mapenzi ya kimungu na kupitia kwa Yesu Kristo, aliyewekwa na Mungu kuwa kuhani mkuu.​—11/15 kur. 9, 10.

● Ni jambo gani linalohakikisha kwamba watoto wachanga watafufuliwa?

Kulingana na Mathayo 2:17, 18 unabii juu ya Raheli akililia watoto wake ulitimizwa wakati Herode alipoagiza watoto wenye umri wa miaka miwili kurudi chini wauawe huko Bethlehemu na kandokando yake. (Yer. 31:15) Unabii huo unaendelea kusema hivi: “Zuia sauti yako, usilie, na macho yako yasitoke machozi; maana kazi yako itapata thawabu, nao watakuja tena toka nchi ya adui; ndivyo asemavyo [Yehova].” (Yer. 31:16) Kwa njia ya ufufuo peke yake ndipo watoto hao wachanga wangeweza kurudi kutoka sheol (kaburi) kwa faraja ya akina mama waliowapoteza katika mauti.​—1/1/80 uku. 6.

● Ni jambo gani linalowatambulisha Wakristo wa kweli leo?

Ni upendo wao kuelekea mmoja na mwenzake, mwenendo wao wa unyofu, na kwa kuwa watu kwa ajili ya jina la Mungu, kwa kuutangaza ufalme wa Mungu na kwa kutokuwamo katika mambo ya kisiasa na vita vya ulimwengu huu.​—7/1 kur. 15, 16.

● Twajuaje kwamba Zaburi 45 ni ya unabii?

Katika Waebrania 1:8, 9, mistari 6 na 7 ya Zaburi 45 imetumiwa na maneno yake yakatumiwa kuhusu Yesu Kristo. Katika mistari hiyo imeonyeshwa kwamba Yehova Mungu anatumika kama ‘kiti cha enzi’ kwa Mwanawe kuonyesha kwamba Aliye Juu Zaidi ndiye Chanzo cha ufalme wa Mwanawe na ndiye Anayetegemeza ufalme wake.​—7/15 uku. 13.

● Tuyaeleweje maneno ya Musa kwa Waisraeli juu ya wao kuwa na ‘amri za Mungu mioyoni mwao’?

Amri hizo za kimungu hazikupaswa kuwa jambo la akilini tu au la kukumbukwa bali zilipaswa zithaminiwe moyoni. Kwa kufanya hivyo ndipo tu Waisraeli hao wangeweza kumpenda Muumba kweli kweli na kuwa katika hali nzuri ya kukazia upendo kama huo kwa watoto wao.​—10/1 uku. 4.

● Sababu gani ‘ujana na utu mzima ni ubatili’?

Siku za nguvu za ujana hupita upesi, kwa kuwa mtu haendelei kuwa kijana milele. Hata vijana ambao ni watu wazima wenye nguvu za ujana waweza kupatwa na magonjwa na kufa. Mtu anayedharau uhakika huu kuhusu ujana huenda akashindwa kutumia nguvu za mwili wake na uwezo wake kwa hekima, akizitumia ovyo na kufanya maisha yake ya baadaye anapokuwa mtu mzima kuwa magumu.​—10/1 uku. 10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki