Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 2/1 kur. 20-23
  • Ushuhuda Watolewa Kuumba Kote Ya 70 W.K.

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ushuhuda Watolewa Kuumba Kote Ya 70 W.K.
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • (Funzo la Kitabu)
  • ROHO YAWASHUHUDIA KUWA NI WANA
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 2/1 kur. 20-23

Ushuhuda Watolewa Kuumba Kote Ya 70 W.K.

(Funzo la Kitabu)

WAKRISTO wengi walimwiga mtume Paulo na mitume wengine katika kuhubiri habari njema za ufalme wa Kimasihi. Kundi lililozaliwa kwa roho likiwa “kiumbe kipya” lilikuwa limetiwa mafuta lifanye kazi hiyo ya kuhubiri. (Isa. 61:1-3; 2 Kor. 1:21, 22.) Walikuwa na juhudi nyingi nao waliendelea kusonga mbele katika kuhubiri habari zilizo njema zaidi duniani kwa wengine wengi kama vile ambavyo ingewezekana. Basi, si jambo la kushangaza kwamba, karibu na miaka 60-61 W.K., au miaka kadha kabla Yerusalemu na hekalu lake zuri sana havijariharibiwa na Warumi katika mwaka 70 W.K., mtume Paulo aliweza kuwaandikia Wakristo katika Kolosai, Asia Ndogo, akiwa kizuizini katika nyumba yake, akasema hivi, hata katika wakati huo: “Habari njema zile . . . zilizohubiriwa katika kuumba kote kuliko chini ya mbingu. Mimi Paulo nikawa mhudumu wa habari njema hizi.”​—Kol. 1:23, NW.

2. Yaliyotimizwa na kundi hilo la karne ya kwanza ni mfano kwa nani leo, na kwa sababu ya wajibu gani walio nao leo?

2 Kutangazwa huko kwa ufalme wa Kimasihi katika kuumba kote na kundi la karne ya kwanza la wanafunzi wa Kristo waliotiwa mafuta ni mfano mzuri kwa kundi lililotiwa mafuta la karne yetu ya 20. Kundi hili lililotiwa mafuta, likiwa “kiumbe kipya” cha Mungu, lahitaji kumaliza kutoa ushuhuda wa ulimwenguni pote juu ya ufalme wa Mungu uliosimamishwa kabla ya “dhiki kubwa” kuja juu ya ulimwengu wote, na kabla Jumuiya ya Wakristo yenye unafiki haijabatizwa kwa moto katika uharibifu wake pamoja na sehemu nyingine yote ya taratibu hii mbovu ya mambo.​—Mt. 24:14-22; Marko 13:10.

ROHO YAWASHUHUDIA KUWA NI WANA

3. Paulo aliliandikia nini kundi katika Rumi juu ya ushuhuda wa roho, nalo ni ulizo gani linalotokea sasa kuhusu wale wanaotarajia kwenda mbinguni leo?

3 Huko nyuma katika karne ya kwanza W.K., waandikaji wa Biblia Wakristo pamoja na wanafunzi wenzao hawakuwa na shaka lo lote juu ya uhusiano wao na Mungu pamoja na daraka lao Kwake. Walikuwa na hakika kabisa kwamba wao walikuwa wana wa kiroho wa Mungu, na kwamba walitazamia urithi wa kimbinguni. Kwa hiyo, hata kabla mtume Paulo hajafika Rumi, angeweza kuliandikia kundi lililokuwa huko, maneno haya ya hakika, pasipo kuwa na shaka Io lote “Mlipokea roho ya kukubaliwa kuwa wana, kwa hiyo twalia: ‘Aba, Baba!’ Roho yenyewe hushuhudia pamoja na roho yetu kwamba sisi tu watoto wa Mungu. Basi, ikiwa sisi tu watoto, sisi tu warithi pia: warithi washirika pamoja na Kristo, tukiteswa pamoja ili tupate kutukuzwa pamoja pia.” (Rum. 8:15-17, NW) Leo, ni nani anayesema kwamba anatazamia kwenda mbinguni, aliye na ushuhuda kama huo wa roho ya Mungu pamoja na roho yake mwenyewe?

4. Roho ya Mungu ilishirikiana na roho ya Wakristo katika kundi la karne ya kwanza katika tendo gani?

4 Bila shaka roho ya Mungu haingetoa ushuhuda kama huo kwa anayedai kuwa Mkristo ambaye kwa kweli yeye si mrithi wa Mungu na mrithi pamoja na Yesu Kristo. Kila tendo linatokeza tendo. Kila tendo linalotokezwa laweza kuwa la kuitikia au la kutoitikia, la kuchukizwa. Katika Warumi 8:15-17, mtume Paulo anazungumza juu ya tendo la kuitikia. Anaeleza utendaji wenye ushirikiano kati ya roho ya Mungu na roho ya yeye aliye kweli kweli mtoto wa kiroho wa Mungu. Sasa, basi, roho ya Mungu ilitoaje ushuhuda pamoja na roho ya washiriki wa kundi la Kikristo la karne ya kwanza, hicho “kiumbe kipya”?

5. (a) Je! kundi la karne ya kwanza lilipinga ushuhuda wa roho ya Mungu kwao kupitia kwa watumishi wake walioongozwa kwa roho ya Mungu? (b) Hivyo, kundi katika Thesalonike liliuonaje ujumbe uliotolewa na Paulo?

5 Ikiwa roho ya Mungu hushuhudia juu ya sisi kuwa Wakristo na juu ya uhusiano wetu na Mungu pamoja na mipango ambayo amefanya kwa ajili yetu, basi, inatupasa kukubaliana na roho hiyo wala si kuipinga. Kwa hiyo, kundi ambalo Wakristo hao wa karne ya kwanza walikuwa washiriki wake waliobatizwa, waliposomewa barua kutoka kwa mtume au mwanafunzi wa Kristo aliyeongozwa na Mungu, walikubali yaliyosemwa kwao na juu yao na barua hiyo juu ya msimamo wao, wajibu wao, na matumaini yao ya wakati ujao katika mpango wa Mungu. Walikubali kwamba roho ya Mungu ilikuwa ikitenda kazi juu ya mitume na wanafunzi hao wenye mamlaka na kwamba ilikuwa ikitenda na kuandika kupitia kwa vyombo hivi vya kibinadamu. Barua ya mtume Paulo kwa kundi la Kikristo la karne ya kwanza huko Thesalonike, Makedonia, inaonyesha uhakika huo. Walijua ukweli wake wakati Paulo alipoandika hivi: “Mlipopata lile neno la ujumbe la Mungu mlilolisikia kwetu, mlilipokea si kama neno la wanadamu, bali kama neno la Mungu; na ndivyo lilivyo kweli kweli; litendalo kazi pia ndani yenu ninyi mnaoamini.”​—1 The. 2:13.

6. Kwa kupatana, Wakristo hao wa Thesalonike wangelipokeaje neno la Paulo lililoandikwa, na walikuwa wameteuliwa na Mungu kwa sababu gani, kulingana na alivyosema Paulo?

6 Hivyo, lingekuwa jambo linalopatana kabisa kwamba waamini hawa wakubali pia neno la Paulo lililoandikwa kuwa vilevile “neno la Mungu.” Katika barua hii Paulo aliandika juu ya ‘kuteuliwa’ kwao na Mungu. Sababu gani ‘wakateuliwa’? “Kwa maana, . . . injili yetu haikuwafikia katika maneno tu, bali na katika nguvu, na katika [roho takatifu] na uthibitifu mwingi; kama vile mnavyojua jinsi zilivyokuwa tabia zetu kwenu kwa ajili yenu. Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, mkiisha kulipokea neno katika dhiki nyingi, pamoja na furaha ya [roho takatifu].”​—1 The. 1:4-6.

7. Wale waliopokea karama za roho kupitia kwa mitume wangeonyeshwa kuwa na uhusiano gani na Mungu?

7 Walijua kwamba, kupitia kwa roho takatifu, Mungu alikuwa amesema na watu wake wateule wa nyakati zilizotangulia Ukristo. Vivyo hivyo, katika wakati wao wenyewe wa karne ya kwanza W.K. Mungu angeweza kusema kwa njia ya nguvu iyo hiyo ya utendaji kupitia kwa mitume wa Yesu Kristo. Zaidi ya hayo Mungu alikuwa akitumia mitume ao hao kupitisha kwa waamini waliobatizwa karama mbalimbali za roho takatifu. Bili shaka wale waliozipokea karama hizo wangeweza kuona kwamba kwa kuzipokea hivyo walikuwa wamefanywa kuwa watoto wa kiroho wa Mungu,—Matendo 8:15-18; 19:2-6.

8. Kupitia kwa barua za waandikaji Wakristo wa Biblia, roho ya Mungu ilikuwa inalishuhudiaje kundi hilo la karne ya kwanza kwamba uhusiano wao na Mungu ulikuwa wa namna ya pekee?

8 Je! mitume hao pamoja na waandikaji Wakristo wengine wa Biblia walikuwa wakiweka mbele ya waamini hao waliobatiwa tumaini la kidunia, tumaini la kuwa watoto wa Baba wa Milele, Yesu Kristo na kuishi katika dunia ya paradiso milele? Hapana! Walikuwa wakiweka mbele ya wale waliohubiri na kuandikia tumaini lililokuwa likipewa wakati huo wale waliokuwa wakizaliwa kama watoto wa Mungu, wana wa Yehova. (Isa. 9:6, 7) Wanafunzi wa siku hizo walikuwa wamehakikishiwa katika maandishi ya Kikristo yaliyokuwa yameongozwa na Mungu kwamba walikuwa wameitwa kwenye ufalme uliokuwa wa kimbinguni na kwamba tumaini lao lilikuwa lile la kuwa warithi washirika pamoja na Yesu Kristo mbinguni. (Kol. 1:13; 1 Kor. 1:26-31; 2 Pet. 1:10, 11) Jambo moja peke yake ndilo lililowekwa mbele yao; hawakuachwa wakiwa na shaka lo lote. Katika njia hiyo roho takatifu ilikuwa ikiwashuhudia wanafunzi hao wa karne ya kwanza kwamba walikuwa watoto wa Mungu, warithi wa Mungu. Hiyo ilimaanisha kwamba, wakati ule ule, walikuwa warithi washirika pamoja na Yesu Kristo aliyetukuzwa.

9. Roho ya Wakristo hao wa karne ya kwanza iliitikiaje ushuhuda uliotolewa na roho ya Mungu, kukawa na matokeo gani juu yao?

9 Msukumo wao wenyewe wa kutoka ndani yao, roho yao wenyewe, iliitikia kwa kushirikiana na roho hiyo ya Mungu yenye kutoa ushuhuda. Roho ya Baba wa mbinguni ilikuwa ikiwatia moyo na kuwatia nguvu wakiwa watoto wake wa kiroho na warithi. Alikuwa ameweka ndani yao hali ya kuwa wana kwa Baba yao wa kimbinguni, wala si hali ya kuwa wana kwa baba yao wa kidunia. Walikuwa na hali ya kuwa wana wa kiroho.

10. (a) Wayahudi waliogeuzwa kuwa Wakristo hawakujisikia tena kuwa chini ya agano gani, na katika hali gani? (b) Kwa kuitikia roho ya Mungu, roho ya Wakristo hao iliwasukumaje waonyeshe kwamba walikuwa wana wa Mungu wa kiroho?

10 Wayahudi au Waisraeli waliofanywa kuwa Wakristo hawakuendelea kujiona kuwa watumwa chini ya agano la kale la Torati ya Musa huku bado wakimngojea Masihi aje. Walijiona walijua kwamba wao walikuwa wana wa kiroho wa Mungu waliyemwabudu kulingana na agano jipya. Roho yao wenyewe, nguvu yenye kuwasukuma iliyotoka mioyoni mwao, iliwaongoza waitikie utendaji wa roho ya Mungu kutoka kwa mioyo yao na kumwita, “Aba, Baba!” Amri za Baba yao kwa wana wake wa kiroho walizitumia juu yao wenyewe. Kazi iliyogawiwa wana wake waliichukua kwa upendo. Ahadi zake za kimbinguni alizowawekea wana wake wa kiroho walizikubali na kujitahidi kujihakikisha kwamba wanastahili kutimiziwa ahadi hizo. Tumaini la kimbinguni aliloweka mbele ya wana wake wa kiroho walilitumaini, nao walijitahidi kuishi kulingana na tumaini hilo. Walikuwa na nia ya kuvumilia kutendwa vibaya na ulimwengu huu.

11. Wao walikuwa na nia ya kuteseka pamoja na Kristo na kufa kifo kama chake kwa sababu ya tumaini gani?

11 Walijua kwamba wangekuwa wana wa Mungu waliotukuzwa pamoja na Yesu Kristo, “tukiteswa pamoja.” (Rum. 8:17) Kwa hiyo walikuwa na nia ya kuteseka kwa sababu ya kuishi kulingana na tumaini lao la kimbinguni. Waliukubali uhakika wa kwamba lazima wafe kifo kama kile cha Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, ili waweze kushiriki ufufuo kama ule wake.​—Rum. 6:5-8.

12. (a) Roho yao iliungana na roho ya Mungu kutoa ushuhuda wa pamoja juu ya uhakika gani? (b) Sala zao na maisha zao zilipatana na tumaini gani, hata kutokee nini?

12 Katika njia hiyo roho ya wana hao wa kiroho wa Mungu wa karne ya kwanza ilijiunga na roho ya Mungu katika kutoa ushuhuda wa pamoja kwamba walikuwa watoto wa Mungu, kwa kuzaliwa mara ya pili wakiwa na urithi waliowekewa mbinguni. Kwa hiyo roho yao wenyewe ilitenda kazi kama nguvu yenye kuwasukuma maishani mwao ili sala zao walizomtolea Baba yao wa mbinguni zipatane kabisa na ushuhuda waliotolewa na roho Yake wala si kuwa kinyume chake. Katika sala zao walizomtolea Mungu, walitumia Maandiko yaliyohusu urithi wao wa kimbinguni. Sala za namna hiyo ziliangaza tumaini lao la kuingia kwenye urithi wa kimbinguni. Kwa hiyo waliishi, wakafikiri, wakasema na kutenda kulingana na sala na tumaini lao. Sala zao ziliwasaidia kuvumilia majaribu na mateso ili wapate msimamo unaokubaliwa na Mungu; nao walijua kwamba msimamo huo wenye kukubaliwa Naye unajenga tumaini ambalo halitakatiza tamaa hata kidogo. Walijua kwamba, ili wapate kutimiziwa tumaini lao la kimbinguni iliwalazimu kuwa ‘waaminifu hata kufa.’​—Rum. 5:3-5; Ufu. 2:10.

13. Sababu gani hayo yaliyotangulia yapaswa yawe uongozi kwa Mkristo aliye wakf na kubatizwa katika kuamua juu ya uhusiano wake na Mungu, sana sana tangu masika ya mwaka 1935 W.K.?

13 Hayo yote yaliyo hapo juu yapaswa kuwa uongozi leo kwa Wakristo walio wakf na kubatizwa wajichunguze na kuona kama roho ya Mungu inatoa ushuhuda pamoja na roho yao wenyewe kwamba wao ni wana Wake wa kiroho na warithi wake, pamoja na kuwa warithi washirika pamoja na Yesu Kristo katika ufalme wake wa kimbinguni. Ndivyo ilivyo, sana sana tangu masika ya mwaka 1935 W.K. Sababu gani tangu wakati huo? Kwa sababu wakati huo “mkutano mkubwa” unaotajwa katika Ufunuo 7:9-17 ulielezwa kuwa jamii ya kidunia ambayo ‘haizaliwi mara ya pili.’ Mahali pake, wanawekewa mbele yao taraja la kuiokoka ‘dhiki kuu’ ya ulimwengu inayokaribia na kutoka ndani yake na kuingia katika taratibu mpya ya Mungu yenye haki, wajifurahishe humo paradiso ya kidunia chini ya ufalme wa kimbinguni wa Yesu Kristo pamoja na warithi wake washirika 144,000. (Luka 23:43, ZSB) Kwa kuutii Ufalme na kujitoa kabisa kwa enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova Mungu katika jaribu la mwisho, hawatakuwa kamwe na lazima ya kufa katika mwili na kuondolewa usoni pa dunia. Wao ni sehemu ya wale “kondoo wengine” waliotajwa na Yesu Kristo, yule Mchungaji Mwema katika Yohana 10:16.

—Kutoka Holy Spirit—the Force Behind the Coming New Order Sura ya 7.

1. Kwa kuwa walitenda kulingana na utiwaji wao wa mafuta, Paulo aliweza kuwaandikiaje Wakristo katika Kolosai, hata karibu na miaka 60-61 W.K.?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki