Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 2/1 kur. 23-24
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Heshimu “Kile Ambacho Mungu Ameunganisha”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Je, Mashahidi wa Yehova Wana Sheria Kuhusu Urafiki wa Kimapenzi?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 2/1 kur. 23-24

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Wakati rafiki yangu alipopata kuwa Mkristo, mke wake alimtaliki naye hukataa hata kumwona. Ingawa huyo rafiki yangu wa kiume anajua kutokana na Biblia kwamba hana uhuru wa kuoa tena, amekuwa akifanya matembezi na mwanamke fulani. Biblia inaonyesha nini juu ya matembezi hayo, nami naweza kumsaidiaje kwa njia iliyo bora zaidi?

Ni jambo la kusikitisha kwamba mke wake ametumia talaka isiyo haki akamwachia hali ya upweke na ya kuweza kupata vishawishi (majaribu). Hata hivyo, maadamu mume huyo hana uhuru wa Maandiko wa kuoa tena, matembezi yake na mwanamke huyo mwingine ni makosa na ni hatari. Yeye anahitaji msaada wenye fadhili lakini wenye imara pia, nawe unaweza kumpa kiasi fulani cha msaada huo.

Siku hizi talaka za kisheria zinaruhusiwa kwa sababu nyingi. Katika macho ya serikali, talaka ya namna hiyo inapokwisha kuamuliwa kabisa watu wale wawili wanakuwa tena “waseja” (wasiooa au wasioolewa). Lakini Neno la Mungu linatoa maoni yaliyo tofauti. Yesu alisema: “Kila mtu atakayemwacha [atakayemtaliki, NW] mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati [porneia, uchafu mbaya sana wa kutumia viungo vya uzazi], akaoa mwingine, azini.” (Mt. 19:9) Kwa hiyo serikali ikitoa ruhusa ya talaka ya kisheria wakati ambao hakuna msingi wa Maandiko wa kutoa talaka hiyo, wala hakuna uasherati uliofanywa, bado Mungu anawaona watu hao wawili kuwa mume na mke.

Kujua hivyo kunasaidia Wakristo wathamini jinsi mtu asiye na uhuru wa Maandiko wa kuoa au kuolewa tena anavyopaswa kujiendesha mwenyewe. Atajiendesha sawasawa na vile angejiendesha kama angalikuwa bado ameoa au ameolewa kisheria na vile angalijiendesha kama angalikuwa akiishi na mwenzi wa ndoa. Ingawa Mithali 5:15-21 inamaanisha ngono hasa, inaonyesha wazi kwamba mwanamume aliyeoa hapaswi kutaka mahaba katika wanawake wengine: ‘Uwe mwaminifu kwa mke wako mwenyewe na umpe yeye peke yake upendo wako. Uwe mwenye furaha pamoja na mke wako na upate furaha yako pamoja na yule msichana uliyemwoa, Acha madaha yake yaendelee kukufanya uwe mwenye furaha; mwache akuzunguke wewe na upendo wake. Kwa nini umpe mwingine upendo wako? Bwana aona kila jambo utendalo.’ (Biblia ya Habari Njema kwa Kiingereza) Naam, mtu ambaye katika macho ya Mungu ameoa au ameolewa anapaswa aepuke kuhusika katika mahaba na mtu mwingine. Yusufu mwaminifu alikataa kufanya uasherati na mwanamke aliyeolewa.​—Mwa. 39 :10-12.

Kufanya tofauti na hivyo kungeonyesha dharau kwa mpango wa ndoa na kwa Mwanzilishi wa mpango huo, Yehova, tena kungewekea wengine mfano mbaya juu ya mwenendo wa Kikristo. Kuongezea hilo, watu hao wawili wakiendelea kushirikiana kwa kuoneana mahaba, wangepatwa na mkazo wenye nguvu wafanye matendo ya ngono yanayofaa katika ndoa tu. Tunasoma hivi: “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.”​—Ebr. 13:4.

Watu wenye kustahili kiroho wanapaswa wamtolee mashauri yenye kutegemea Biblia mtu anayefanya matembezi na mwanamke au mwanamume mwingine ijapokuwa hayuko huru kuoa au kuolewa tena kulingana na Maandiko, wakijaribu “kumrekebisha.” (Gal. 6:1, NW) Ikiwa yeye hasikii, wanapaswa wazidi kutia jitihada za kumsaidia, wamwonye na kumkaripia, hata ‘kumkaripia kwa ukali.’​—Mit. 29:1; Tito 1:10, 13, NW.

Huenda wakaweza kuutia nguvu upendo alio nao kwa Mungu na kumtia nguvu afahamu kwamba anaweza kupata furaha nyingi na kuridhika sana kwa sababu ya kupendwa na kubarikiwa na Mungu. (Rum. 8:35-39; 2 Kor. 4:16-18) Wao, na wengine kundini, huenda wakaweza kumsaidia ashinde upweke wake kwa kuwa na ushirika ufaao, wenye kujenga, na kuendelea kujishughulisha katika kazi njema. (Tito 2:14) Hivyo huenda wakaweza kumgeuza aache mwendo unaoweza kumfanya aivunje sheria ya Mungu inayokataza uzinzi, kwa maana akiivunja huenda akalazimika kutengwa na ushirika wa kundi.​—1 Kor. 5:9-11.

Mtu fulani akiendelea kujikaza afanye matembezi na mwanamke au mwanamume bila ya kuwa huru kuoa au kuolewa kulingana na Maandiko, inaelekea kwamba wengi kundini watajisikia wakiwa na wajibu wa kulitumia shauri la Biblia lililotolewa juu ya mtu aliyekataa kufanya kazi: “Ikiwa mtu ye yote hatii neno letu kupitia barua hii, mwekeni huyu katika hali ya kutiwa alama [jihadharini na mtu huyo, UV], acheni kushirikiana na yeye ili apate kuaibishwa. Hata hivyo msiwe mkimwona yeye kama adui, bali endeleeni kumwonya kwa upole kama ndugu.” (2 The. 3:14, 15, NW) Wakristo wengi wanaouheshimu sana mpango wa Mungu wa ndoa hawatataka kushirikiana kwa urafiki na mtu anayeudharau mpango huo kwa makusudi. Wakikataa kushirikiana naye kwa njia hiyo, na kwa maneno wanayosema kundini juu ya kuyakubali mashauri ya Mungu yenye hekima, huenda wakaweza kumvuta moyo auache mwendo wake wenye makosa.​—Yuda 23a.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki