Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 3/15 kur. 22-24
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Huleta Wana Wengi Kwenye Utukufu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • “Mjawe na Furaha Milele”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Kujitahidi Kuufikia Ufalme
    “Ufalme Wako Uje”
  • Kitabu cha Biblia Namba 58—Waebrania
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 3/15 kur. 22-24

Maswali kutoka kwa Wasomaji

● Kulingana na Waebrania 12:22, 23 (Habari Njema kwa Watu Wote) mtume Paulo anasema juu ya “roho za watu waadilifu [wenye haki, UV] waliofanywa kuwa wakamilifu.” Je! “watu” hao wanaweza kuwa wale watu waaminifu ambao juu yao Paulo aliandika katika Waebrania sura ya 11.

Dokezo la kwamba maneno hayo yaweza kutumiwa juu ya watu wa imani na waaminifu wa nyakati zilizotangulia Ukristo kufikia Yohana Mbatizaji si dokezo jipya. Tayari toleo la Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) la Agosti 15, 1913, kurasa 248 na 249, lilidokeza hivyo kwa uangalifu, nayo maoni hayo yaliendelea kushikiliwa kwa miaka mingi. Katika mstari huu neno “watu” halipatikani katika maandishi ya awali ya Kigiriki. Ndiyo sababu tafsiri ya New World yasomwa, “na maisha za kiroho za wenye haki waliofanywa kuwa wakamilifu.”​—Angalia Jerusalem Bible, Emphatic Diaglott, Rotherham, Westminster Version, Kingdom Interlinear Translation.

Waebrania 11:8-10 huwataja Ibrahimu, Isaka na Yakobo na kuonyesha kwamba Ibrahimu aliondoka mji wa Uru wa Ukaldayo na ya kwamba yeye pamoja na Isaka na Yakobo waliishi maisha ya kuhama-hama mpaka Yakobo alipohamia nchi ya Misri katika siku za mwanawe Yusufu. Kwa hiyo katika kipindi hicho cha wakati, wao hawakuishi katika hali iliyotulia, iliyoimarika kama vile kuishi katika mji. Hakuna lo lote katika Maandiko ya Kiebrania linalosema kwamba Mungu aliahidi wanaume hao watatu “mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.” Hayo ni maelezo ya Paulo kuhusu jambo hilo. Bila shaka usemi huo unaitaja ile serikali ya Mungu iliyosimamishwa na ‘uzao wa Ibrahimu,’ serikali ambayo chini yake hao wazee watatu wa ukoo wataishi duniani na kupata ukamilifu wa kibinadamu kufikia mwisho wa ile miaka elfu.​—Gal. 3:16.

Wakati Mungu alipowatoa wazao wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo kutoka nchi ya Misri na kuwaingiza katika nchi aliyokuwa amemwahidi Ibrahimu, walikaa katika miji ya Wakanaani, peke yake ukiwa mji Yeriko uliharibiwa kwa uweza wa Mungu. Baada ya hayo manabii wote waaminifu pamoja na wanawake waaminifu walikuwa na makao ya daima katika miji. Kwa hiyo, haingeweza kusemwa juu yao kama vile ilivyosemwa kuhusu Ibrahimu, Isaka na Yakobo, kwamba walikuwa wakitafuta mji duniani katika wakati ujao. Yerusalemu uliharibiwa katika mwaka 70 W,K., miaka 39 baada ya Yohana Mbatizaji kukatwa kichwa. Kwa hiyo hata Wayahudi Wakristo waliishi katika mji huo uonekanao wa kidunia, mpaka Jemadari Galo akaondoka Yerusalemu wakati ambapo Wakristo walitii amri ya kiunabii ya Yesu watoke katika mji huo.​—Mt. 24:15-22.

Waebrania 13:12-14 hutaja juu ya Yesu akitundikwa mtini nje ya kuta za Yerusalemu wa kidunia, au “nje ya lango.” Kwa sababu ya hali hiyo, Paulo anaendelea kusema, “Basi tutoke tumwendee nje ya kambi [kama “yule mbuzi...kwa ajili ya Azazeli’ alipelekwa jangwani siku ya upatanisho (Law. 16:10)], tukichukua shutuma lake. Maana hapa hatuna mji udumuo, bali twautafuta ule ujao.” “Mji” huo unamaanisha ule ufalme wa kimbingu, ule Yerusalemu Mpya, anaotaja Paulo katika Waebrania 12:22.

Wale watu wa kale, sana sana kuanzia na Ibrahimu kufikia Yohana Mbatizaji, hawakuwa wakitafuta kwenda mbinguni na kuingia kwenye Yerusalemu huo wa kimbinguni. Wao hawakuwa na wazo lo lote kama hilo. (Mt. 11:11) Wao hawangeweza kuwa na tumaini la namna hiyo kwa kuwa hawakuwa wamezaliwa kwa roho takatifu ya Mungu. Yohana 7:39 huthibitisha hilo, likisema hivi: ‘Na neno hilo alilisema katika habari ya roho, ambayo wale wamwaminio wataipokea baadaye; kwa maana roho ilikuwa haijaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.’ Kuzaliwa kiroho kwa wanaume na wanawake Wakristo hakukuanza mpaka Pentekoste ya mwaka 33 W.K. Wale waliozaliwa kwa roho takatifu tangu wakati huo na kuendelea walitazamia mbele kwenye uzima katika ule mji wa kimbinguni uliofananishwa na Yerusalemu wa kidunia.

Hiyo ndiyo sababu Paulo katika kuwaandikia Wakristo Waebrania aliweza kusema kwa usahihi hivi katika Waebrania 12:22, “Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi.” Katika siku za Paulo, “[kundi] la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni” lilikuwa halijafikia umri wa miaka 30, kwa hiyo lilikuwa karibu na mwanzo wake, nalo lilikuwa na hesabu iliyokuwa chini sana kuliko 144,000. Kukamilishwa kwa hesabu 144,000 ya “wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni” kunafanyika kufikia mwisho wa inayoitwa Enzi ya Ukristo, inayomalizika wakati wa “dhiki kubwa” ya Ufunuo 7:14 na Mathayo 24:21, 22. Hivyo, Paulo pamoja na Wakristo Waebrania aliowaandikia walikuwa wakilifikilia ‘kundi’ hilo katika habari ya hesabu yake kamili ya 144,000.

Baada ya hapo, Waebrania 12:23, 24, NW husema, “na Mungu Hakimu wa wote, na maisha za kiroho [maelezo ya chini, roho] za wenye haki waliofanywa kuwa wakamilifu, Yesu mpatanishi wa agano jipya, na damu ya kunyunyizia ambayo, husema katika njia bora zaidi kuliko damu ya Habili.” Kwa hiyo Mungu ndiye hakimu wa wote, kutia na wale 144,000 waliofanywa washiriki. Kwa hiyo wale wanaotazamia kuwa washiriki wa “kundi” lililotukuzwa lazima wapitie kwenye kipindi cha kuhukumiwa kabla ya kukubaliwa na Yehova Hakimu Mkuu Zaidi. Hiyo ndiyo sababu, baada tu ya kumtaja, mstari huo unaendelea kusema, “na maisha za kiroho za wenye haki waliofanywa kuwa wakamilifu.” Washiriki wa ‘kundi’ la Kikristo waliozaliwa kwa roho ndio waliohesabiwa haki kwa imani. (Rum. 5:1; 8:1-4) Kwa sababu hiyo wanatajwa kuwa “wenye haki waliofanywa kuwa wakamilifu.”

Kwa hiyo wanasihiwa ‘waitoe miili yao kuwa dhabihu iliyo hai, takatifu, yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mtakatifu pamoja na nguvu yenu ya akili.’ (Rum. 12:1, NW) Hivyo ‘wanatoka na kumwendea nje ya kambi, wakichukua shutumu lake.’ (Ebr. 13:13) Kwa kweli, Wakristo hawa waliozaliwa kwa roho wana “maisha za kiroho” sasa wanapokuwa duniani nao wanasihiwa waenende kulingana na roho ambayo kwayo walizaliwa.

Mtume Paulo anataja hizo “maisha za kiroho” za Wakristo hao waliohesabiwa haki katika sura iyo hiyo ya Waebrania 12:9, NW: “Je! sisi hatutajitiisha zaidi kwa Baba ya maisha zetu za kiroho tuishi?” Kwa halisi, maandishi ya Kigiriki husomwa, “Baba ya roho.” Yeye ndiye baba ya kundi lililozaliwa kwa roho ambalo Paulo alikuwa akiandikia na kwa hiyo hapa tafsiri ya New World inafasiri usemi huo ikitumia neno la kibinafsi, na kusema, “Baba ya maisha zetu za kiroho.” Usemi huo unalitangulia andiko la Waebrania 12:23 kwa mistari 14 na kwa hiyo ni sehemu ya maneno yanayolizunguka.

Katika Waebrania 12:1 mtume Paulo anageuza fikira zake kutoka kwa mazungumzo juu ya wanaume na wanawake waaminifu wa nyakati zilizotangulia Ukristo na kuzielekeza kwenye kundi la Kikristo lililozaliwa kwa roho pamoja na mwendo wa kimungu wa utumishi uliokuwa mbele ya Wakristo hao waliozaliwa kwa roho. Kwa hiyo katika Waebrania 12:23, yeye hakuwa akirudia yale aliyokuwa akizungumza juu yake katika sura ya 11. Kulingana na mambo hayo ya hakika, usemi “maisha za kiroho za wenye haki waliofanywa kuwa wakamilifu” hulionyesha “[kundi] la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni” katika maoni yaliyo tofauti na kwa hiyo si kurudia tu kusiko na maana kwa yale yaliyokuwa yamesemwa katika mstari wa 22. Kwa hiyo hakuna sababu ya kujaribu kuutumia juu ya jamii nyingine ya watu wenye kumwogopa Mungu kama vile wanaume na wanawake waaminifu wa nyakati zilizotangulia kuanzia na Habili mpaka Yohana Mbatizaji.

Na kwa kuwekea mipaka zaidi andiko lote la Waebrania 12:22, 23 litumike juu ya kundi la Kikristo lililozaliwa kwa roho, Paulo anaendelea kusema, “na Yesu [mpatanishi] wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili.” (Ebr. 12:24) Kundi lililozaliwa kwa roho limo katika hilo agano jipya na kwa hiyo Yesu ni mpatanishi wao. Wao ndio ambao juu yao “damu” ya Yesu Kristo inanyunyizwa katika njia ya kiroho hivi kwamba inaleta matokeo bora zaidi kuliko vile damu ya Habili mfia-imani ingefanya. (Ebr. 11:4) Ndiyo kusema, wanahesabiwa haki kweli kweli au kutangazwa kuwa wenye haki sasa kwa kuiamini damu hiyo.​—Rum. 5:9.

Kupatana na hayo yote, Paulo anaendelea kuzungumza na kundi hilo lililozaliwa kwa roho katika Waebrania 12:25-28, akiwasihi wajihakikishe kwamba wanastahili kuuingia ufalme wa kimbinguni, ambao ndio “mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni,” ambao ndio walioukaribia. Mabaki ya kundi lililozaliwa kwa roho la washiriki 144,000 wanakaribia zaidi mambo yaliyoelezwa na Paulo katika mistari 22 na 23 kuliko vile walivyokuwa hao Wakristo Waebrania wa karne ya kwanza. Nalo kundi kubwa la “kondo wengine” wanafurahi pamoja nao kwamba ndivyo ilivyo. Kwa kweli leo “kundi kubwa” hilo hutembea kwa imani kama vile walivyofanya wanaume na wanawake waaminifu wa nyakati zilizotangulia Ukristo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki