Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 8/15 uku. 23
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Kielezi cha Talanta
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Kufanya Hesabu Juu ya Matumizi ya Hazina za Kristo
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Matokeo Mazito ya Kuwaza Kubaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Jifunze Kutokana na Mfano wa Talanta
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 8/15 uku. 23

Maswali kutoka kwa Wasomaji

● Katika ule mfano wa “talanta,” ni nani wanaofananishwa na wale watumwa watatu?​—Mathayo 25:14-30.

Kwa kuwa watumwa wote watatu wamo kati ya watu wa nyumba ya ‘bwana wao,’ wanasimamia wote wanaotazamiwa kuwa warithi wa ufalme kimbingu, wakiwa na uwezo wenye kutofautiana wa kufanya mambo na nafasi mbalimbali za kuongeza faida za Ufalme. Tangu Pentekoste 33 W.K. na kuendelea mpaka siku hizi, watumwa fulani waliotiwa mafuta wangekuwa na uwezo mkubwa zaidi, nguvu na nafasi nyingi zaidi za kuongeza “mali” za bwana wao alizowakabidhi wamtunzie. Mitume na wengine wenye mapendeleo makubwa zaidi ndio wangekuwa katika kila kikundi cha “talanta” tano. Kwa kuwalinganisha na hao, wengine wangeweza kufanya machache zaidi kwa sababu ya hali zao. Hata hivyo, wote walitakwa wawe wakijitoa na kufanya kazi kwa nafsi yote, na wote wangepokea thawabu ile ile moja.

Hata yule mtumwa aliyepewa “talanta” moja hakutangulia kuandikiwa kwamba angeshindwa kufaulu hata akijaribu namna gani, hapana. Kama yeye angaliongeza “talanta” ile moja ziwe mbili, inaelekea kwamba angalipokea thawabu ile ile ya ‘kuingia katika furaha ya bwana wake.’ Kwa sababu alikuwa ‘mlegevu’ na “mbaya,” anafananisha wale wenye kutazamiwa kuwa warithi wa Ufalme wanaogeuka na kuwa wasio waaminifu. Hao wanapoteza thawabu yo yote, zaidi ya kupoteza mapendeleo yao.

Washiriki wa Jumuiya ya Wakristo wanajisema kuwa ndio watumwa wa kweli wa Bwana, Yesu Kristo, lakini maneno na matendo yao yanawaonyesha kuwa hawastahili kuwa kati ya watu wa nyumba ya Bwana, hata kama wanadai sana kwamba wanastahili. Basi wao hawafai kuwa wanaotazamiwa kuwa warithi wa ufalme wa kimbingu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki