Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 7/15 uku. 3
  • Vijana Katika Ulimwengu wa Kisasa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vijana Katika Ulimwengu wa Kisasa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UBORA WA MASADIKISHO IMARA
  • ‘WAKAZWA KUTENDA MABAYA’
  • Marafiki Wazuri na Wabaya
    Amkeni!—2004
  • Umuhimu wa Kuwa na Maadili
    Amkeni!—2019
  • Kubalehe—Kujitayarisha Kuwa Mtu Mzima
    Amkeni!—2011
  • 7 Kanuni za Maisha
    Amkeni!—2018
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 7/15 uku. 3

Vijana Katika Ulimwengu wa Kisasa

Muda wa Kubalehe Mpaka Kupevuka Mwili Ndio Hatari Zaidi!

Muda wa kubalehe kwa kijana mpaka kupevuka kwake akomae mwilini umeelezwa kuwa “ndio ukuzi hatari kuliko ukuzi mwingine wote unaompata mwanadamu” leo. Mtu aliyeyasema maneno hayo alieleza hivi: “Kijana ambaye ameanza kubalehe anakuwa hatarini kwa sababu sasa uhusiano wake na watu wakubwa unavunjika. Kwa mara ya kwanza anabaki akiwa peke yake kabisa bila kulindwa na wakubwa wake wa umri. Anapatwa na mikazo mingi kwa kushangazwa na desturi zinazofuatwa na watu wazima, kushangazwa sana na wakati ujao na kujisikia ameachiliwa kabisa bila ya wengine kumjali.”​—Maneno ya Ruth Aikins, katika kitabu Quality of Life​—The Early Years, kilichodhaminiwa na Shirika la Kitiba la Amerika.

Amebadilika upesi-upesi sana! Ameacha kuona ubora wa kufuata tabia njema. Amezidi kutia mashaka.

Vijana wenye kuhitaji uongozi hawaoni kielelezo cha wakubwa wao wa umri kikistahili kuigwa nao, hawawaoni wakifuata mambo bila ugeu-geu wala kufuata kanuni za adili kwa imara. Vijana wengi wanawaza kwamba wazazi wao wana tabia za kuchukiza sana. Lakini inawapasa vijana wakumbuke kwamba ingawa huenda vizazi vya hapo kwanza vikawa vilipuza kanuni zinazofaa, kanuni hizo zimekuwamo muda wote katika Biblia. Biblia inaonyesha mambo ambayo watu wangalipaswa kuyafanya, na mambo ambayo karibuni Mungu atayafanya atatue matatizo ya dunia.

UBORA WA MASADIKISHO IMARA

Je! watoto wako wanakuona wewe ukiwasaidia sana​—ukiwa mwenye kuwawekea kielelezo cha kufuata?

Joseph na Lois Bird waliandika hivi katika kitabu Power to the Parents!: “Mtoto huzaliwa ndani ya ulimwengu asioweza kuufahamu ulivyo, ulimwengu asimoweza kuendelea kuwa hai pasipo kusaidiwa sana na kulindwa sana. . . .Yeye anahitaji kujua kwamba watu wazima walio wa maana zaidi maishani mwake wamekwisha kupata utatuzi wa matatizo yao wenyewe maishani, kwamba wanaweza kuona kusudi katika ulimwengu wao.”

“Watoto wetu wanahitaji kutuona sisi tukiwa na masadikisho imara, tukiwa na kanuni za mwenendo zisizobadilika-badilika maishani mwetu. Wakituona tukisita-sita kufanya mambo, tukikubaliana na mambo yasiyofaa kwa sababu ya woga, na kuwa na matendo ya unafiki, watatatizika kuendeleza masadikisho yao wenyewe wanapoendelea kukomaa mwilini.”

Watoto wako ni wenye baraka sana ikiwa jamaa yako ina masadikisho hayo yenye kutegemea kweli ya Neno la Mungu! Neno hilo linaweza kuipa jamaa yako kanuni za maisha zisizobadilika, miradi imara ya kiroho, imani thabiti katika Mungu, na kichocheo kikubwa kitakachowapa watoto wako wapendwa imani hiyo iliyo nzuri sana.

‘WAKAZWA KUTENDA MABAYA’

Mkazo wa kuiga rafiki zetu ni nguvu kubwa. Msichana wa miaka 16 aliandika hivi: “Nilipokuwa mdogo zaidi, nilikuwa nikikazwa nyakati zote nitende mabaya, kama kuvuta sigara, kuiba na kufanya mambo mengine kama hayo. . . . Kusema kweli mimi sikutaka kuvuta sigara, lakini sikutaka niwe nikiambiwa na wengine, ‘Ah, wewe ni kaoga, wewe mjinga.’ . . . Sasa nimetambua kwamba urafiki unaotegemea kukubaliana na watu juu ya mambo yasiyofaa ni urafiki unaokwisha upesi.” Kijana mwenye umri wa miaka 12 alisema hivi: “Wakati unapokazwa na mtu fulani, jambo bora zaidi ni kumpuza au kujitenga naye, au kubaki ukiwa pamoja na rafiki unaowapenda.” (Kitabu Listen to Us, kurasa 110, 111) Hekima nzuri namna gani kutoka kwa vijana wawili​—ni afadhali kubadili rafiki zako badala ya kushawishwa uyachafue mambo unayojua ni ya haki!

Zamani za kale Yehova aliwaonya Israeli juu ya tatizo hilo. Alisema kwamba kushirikiana na watu wasioamini kungefanya ‘wakuite,’ nawe ungekula nyingine za dhabihu zao. Halafu mabinti wao wangeolewa na wana wako, na kuwaongoza wanao waabudu miungu ya uongo. (Kutoka 34:12-16) Kijana mwanamke Dina alijifunza hatari ya kushirikiana na watu wasiomcha Mungu baada ya kuingia katika mashaka yenye kumhuzunisha. Wakati yeye alipotembelea wasichana Wakanaani bila kutumia hekima, kijana mwanamume, “mwenye heshima kuliko wote nyumbani mwa babaye,” alimchafua, kisha damu nyingi sana ikamwagika kwa sababu ya tukio hilo. (Mwanzo 34:​1-31) Basi lina ukweli mwingi kama nini onyo hili la Kibiblia: “Urafiki mbaya huharibu tabia njema”! (1 Wakorintho 15:33, Habari Njema kwa Watu Wote) Au, ni kama vile The Jerusalem Bible inavyoeleza: “Rafiki wabaya huharibu watu wa cheo bora zaidi.”

Kurasa zinazofuata zinatoa maelezo mengi zaidi yenye kutegemea Neno la Mungu, kuonyesha namna jamaa zinavyoweza kuungana zishinde utatizi mbalimbali unaoletwa na ulimwengu huu wa kisasa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki