Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 8/1 uku. 9
  • Alifanya “Mizigo Mizito” Ikawa Myepesi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Alifanya “Mizigo Mizito” Ikawa Myepesi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Habari Zinazolingana
  • Mathayo 11:28-30—“Njoni Kwangu, . . . Nami Nitawapumzisha”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • “Nira Yangu ni ya Fadhili na Mzigo Wangu ni Mwepesi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • ‘Kupata Burudisho la Nafsi Zenu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • “Njooni Kwangu, . . . Nami Nitawaburudisha”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 8/1 uku. 9

Alifanya “Mizigo Mizito” Ikawa Myepesi

YESU alisema hivi kuhusu waandishi na Mafarisayo: “Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao.” (Mathayo 23:4) Ukiwa ni ushuhuda wa jinsi hayo yalivyokuwa kweli, twasoma katika kitabu A Dictionary of the Bible, kilichohaririwa (kilichoandikwa) na James Hastings:

“Waandishi hawakuwa wanafalsafa; walikuwa wafasiri wa Sheria takatifu. . . . Kila sehemu ya maisha iliongozwa nayo. . . . Kila amri ya Biblia ilizungukwa na maagizo mengi madogo-madogo. Hakuna rekebisho lililoruhusiwa hata hali zikibadilika; utii kamili wa Sheria katika sehemu zayo zote ulitakiwa kabisa kwa kila Myahudi. Kwenye maagizo ya Sheria Iliyoandikwa kuliongezwa ‘Halakha’ au Sheria ya Kupokezwa, ambayo ilipokezanwa kama amana tukufu kutoka kizazi mpaka kizazi, na hatimaye ikaunganishwa katika Talmudi. . . . Kwa njia hiyo jaribio likafanywa kuingiza kila kisa kinachowazika ndani ya Sheria, na kuongoza mwenendo wote wa kibinadamu kwa kila jambo dogo kwa mawazo yasiyo na rehema. Mambo ya undani ya kisheria yalizidishwa mpaka dini ikawa biashara, na maisha yakawa mzigo usiovumilika. Watu wakawa wanatenda tu bila kufikiria. Sauti ya dhamiri ilinyamazishwa; uwezo wenye kutendesha wa neno la Kimungu ukazuiwa na ukafunikwa na amri nyingi zisizo na mwisho. Kwa sababu hiyo Bwana yetu aliwashtaki Mafarisayo, kwamba kwa mapokeo yao waliitangua Sheria.”

Lazima iwe kwamba watu wanyenyekevu na wanyofu walitiwa moyo kujua kwamba Mwana wa Mungu hakuiona ibada kwa njia hiyo! Lazima wawe walipendezwa na maneno yake: “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”!​—Mathayo 11:28-30.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki