Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 3/1 kur. 20-21
  • Je! Wewe Unaitafuta Kabisa Kabisa Imani ya Kweli?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unaitafuta Kabisa Kabisa Imani ya Kweli?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • “Imani Iliyotenganishwa na Matendo Imekufa Kama Mzoga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Onyesha Imani Yako Katika Ahadi za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • “Nisaidie Mahali Ambapo Nahitaji Imani!”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Zoea Imani Yenye Msingi Wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 3/1 kur. 20-21

Je! Wewe Unaitafuta Kabisa Kabisa Imani ya Kweli?

JE! WEWE unautafuta kabisa kabisa ukweli? Labda ungejibu: “Bila shaka ninautafuta!”

Lakini watu wengi hawautafuti ukweli kabisa kabisa. Kwa kweli, huenda hata wasitake kuamini. Kwa nini mtu asitake kuamini kwamba Mungu yuko na kwamba Biblia, pamoja na ahadi zayo za wakati ujao zenye kutokeza, ni Neno lake zuri ajabu?

Kwa wengine, ili wakubali mambo hayo ya hakika huenda ikahitaji mabadiliko katika namna yao ya maisha. Kwa sababu hawataki kupatanisha maisha zao na njia za Mungu, inakuwa lazima wabuni mashaka na vipingamizi, na kujisadikisha kwamba Biblia si ya kweli.

Hata watu fulani mmoja mmoja kundini wanaweza kuwa hivyo. Ukweli ni mzuri kwao, lakini huenda wakawa wangali wanashikilia zoea fulani la siri ambalo wanajua Neno la Mungu linakataza. Kwa hiyo hawachukui hatua za kusonga mbele au wanaambaa-ambaa polepole. Biblia inasema: “Ilikuwa kwa kupuuza dhamiri kwamba watu fulani wakavunja imani yao.”​—1 Timotheo 1:19, The New English Bible.

Yesu Kristo alipokuwa duniani, ukweli uliwaudhi watu wengi. Kwa sababu ya kutaka kufanya mambo katika njia yao wenyewe, walikataa kukubali ushuhuda uliokuwa thabiti. Akitaja maneno ya kiunabii ya mapema zaidi, Yesu alisema kwamba moyo wao ulikuwa usioitikia. Walikuwa wamefunga macho na masikio yao “wasije wakaona kwa macho yao, wakasikia kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao” ili waponeshwe kiroho.​—Mathayo 13:14, 15.

Watu wa namna hiyo huenda wakasema tu kwamba mambo hayajafanywa yakawa wazi. Wengine waliompinga Yesu walimuuliza hivi: “Hata lini utatuhangaisha nafsi zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi.” Lakini kushindwa kwao kufahamu hakukuwa kosa la Yesu; lilikuwa kosa lao wenyewe. Yesu alijibu: “Naliwaambia, lakini ninyi hamsadiki. Kazi hizi ninazozifanya kwa jina la Baba yangu ndizo zinazonishuhudia. Lakini ninyi hamsadiki, kwa sababu hammo miongoni mwa kondoo wangu.”​—Yohana 10:24-26.

Mtu ye yote asipotaka kusikia na kuelewa ukweli na kugeuka aponeshwe, Shetani Ibilisi atatumia jambo hilo kwa faida yake. Shetani anapofusha “akili za wasioamini, ili mwangaza wa habari njema zenye utukufu juu ya Kristo, ambaye ni mfano wa Mungu, usipate kung’aa kwa kupenya.”​—2 Wakorintho 4:4, NW; ona pia Mathayo 13:10-15.

Je! hiyo maana yake ni kwamba hakuna tumaini la kusikia na kuelewa habari njema? Bila shaka haimaanishi hivyo! Maana yake ni kwamba sehemu kubwa inakutegemea wewe, uliye msikiaji.

Mambo ambayo Biblia inasema yanasikika kuwa ya kweli ikiwa unaitafuta kabisa kabisa imani ya kweli. Viongozi wa kidini wenye kiburi na wenye kujikweza, ambao hawakutaka kusikiliza, walimpinga Yesu. Lakini namna gani umati wa watu? Lo! “walishangaa mno kwa mafundisho yake”! Hata maafisa waliotumwa wakamkamate walirudi wakiwa na ripoti hii: “Hajanena kamwe mtu ye yote kama huyu anavyonena.”​—Mathayo 7:28; Yohana 7:46.

Ikiwa unautafuta ukweli, unatafuta njia ya Mungu na una nia ya kufuata Neno lake maishani mwako, utaipata imani ya kweli. Yesu alisema: “Heri wenye njaa na kiu ya haki; maana hao watashibishwa.” “Walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi.” “Kondoo wangu waisikia sauti yangu; nami nawajua, nao wanifuata.” “Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu.”​—Mathayo 5:6; Yohana 10:14, 27; 18:37.

Imani ni tunda linalozaliwa na roho takatifu ya Mungu. (Wagalatia 5:22, 23) Ukiomba upate maarifa sahihi na imani, utie jitihada kabisa kabisa upate hivyo na kufuata hivyo maishani mwako, Mungu atakusaidia. Kama Yesu alivyosema: “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.”​—Mathayo 7:7.

Hata ikiwa una tatizo ambalo unahitaji kurekebisha, Mungu atakusaidia. Maandiko yanasema: “Mtumaini [Yehova] kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe. Katika njia zako zote mkiri yeye, naye atanyosha mapito yako.”​—Mithali 3:5, 6.

Mungu “huutazama moyo.” (1 Samweli 16:7) Yeye anajua kama unautafuta ukweli na uadilifu na kama una nia ya kufanya mambo katika njia yake inayofaa. Ukimkaribia Mungu, yeye atakukaribia wewe.​—Yakobo 4:8.

Je! wewe ni mtu wa namna hiyo? Je! wewe unaitafuta kabisa kabisa imani ya kweli? Je! wewe umekwisha kusikia mafundisho ya Baba na kufungua akili yako iyatwae? Je! wewe umejifunza hayo na kuyakubali? Na ili ujipatanishe na njia za Mungu za uadilifu, je, wewe umenyosha mambo ambayo labda yalikuwa matatizo maishani mwako mwenyewe?

Ikiwa ndivyo, unaweza kutiwa moyo na maneno ya Yesu: “Imeandikwa katika manabii, Na wote watakuwa wamefundishwa na [Yehova]. Basi kila aliyesikia na kujifunza kwa Baba huja kwangu.”​—Yohana 6:45.

Mafundisho ya Baba wa kimbingu yanapatikana katika kitabu cha pekee sana. Ebu sasa na tuchunguze thamani yacho na jinsi kinavyoweza kugeuza imani yako.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki