Makumbusha na Maagizo ya Mungu wa Mfumo Mpya
“Nimetunza Maagizo yako na makumbusha yako, kwa maana njia zangu zote ziko mbele yako.”—ZABURI 119:168, New World Translation.
1. Makumbusha yanatumika katika njia zipi kufurahisha watu wa Yehova?
MFUMO mpya wa Mungu wenye uadilifu umekaribia! Mashahidi wa Yehova, wanaopenda sheria yake ya uadilifu, wanahitaji kupewa makumbusha katika Neno lake na kupitia tengenezo lake katika nyakati za maana sana. Kwa sababu wanashika makumbusha hayo ya kimungu, wao ni wenye furaha. Makumbusha hayo yanawachochea wamtafute, na matokeo yanakuwa ni furaha. Tafsiri ya Kiswahili ya neno la Kiebrania ‘edoth’ kuwa “makumbusha” badala ya “shuhuda” (martyri’a, kulingana na Septuagint Version; ona pia Zaire Swahili Bible) ni yenye nguvu zaidi na yenye maana zaidi. Inaonyesha kwamba Yehova, ikitegemea pindi inavyotaka, anatukumbusha ni nini sheria zake, maagizo yake, kawaida zake na amri zake. Kwa hiyo yeye haachi tusahau hayo kabisa. Tusipoudhika kwa sababu ya makumbusha hayo, tunakuwa wenye furaha kwa sababu ya kuyashika.
2. Mwandikaji wa Zaburi 119 alikuwa na msingi gani wa kukazia makumbusha mengi hivyo?
2 Ikiwa alikuwa akiandika si baada ya karne ya tano kabla ya Wakati wa Kawaida wetu, mtunga-zaburi angeweza kutumia Maandiko ya Kiebrania yote tangu Mwanzo mpaka Malaki. Kitabu cha tano kinaitwa Kumbukumbu la Torati (Septuagint Version ya Kigiriki, kama ilivyotangulia kuonyeshwa), jina ambalo maana yake ni “Sheria ya Pili.” Kwa wazi mambo yaliyomo katika kitabu hicho kwa sehemu kubwa yalionwa kuwa ni maelezo ya Torati (agano) ambayo Yehova alifanya na Israeli kupitia upatanishi wa nabii Musa. Kwa hiyo kitabu cha Kumbukumbu la Torati chapasa kuwa chenye makumbusha, lakini pia vitabu vingine vyote vya Biblia vina makumbusha ya Mungu kwetu.
3. (a) Mitajo ya Maandiko ya Kiebrania inatukumbusha nini? (b) Furaha yetu inawezaje kuwa kubwa hata zaidi ya ile ya mtunga-zaburi?
3 Mamia ya mitajo kutoka Maandiko ya Kiebrania katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yanatumika kuwa makumbusha si ya mambo tu ambayo Yehova alifundisha watu wake chini ya Torati bali pia ya makusudi yake mazuri sana kuhusu kundi la Kikristo na jamii ya kibinadamu iliyokombolewa. Leo wanafunzi wa Yesu Kristo, aliye Musa Mkuu Zaidi, wana makumbusha zaidi kutoka kwa Yehova Mungu. Makumbusha hayo ni mengi zaidi ya aliyokuwa nayo mtunga-zaburi, na wakiyashika kwa uaminifu wanapaswa kuwa na furaha kubwa zaidi ya mtunga-zaburi. Kwa kutafuta makumbusha Yake kwa funzo la Biblia, kwa kweli wanamtafuta Yehova kwa moyo wao wote.
4. Badala ya kuudhika na makumbusha ya Mungu, ni nia gani inayofaa katika kumwiga mtunga-zaburi?
4 Jambo ambalo linatupa shauri jema na kutuepusha tusishiriki yatakayowapata waovu ni jambo la kuthaminiwa. Hivyo ndivyo mtunga-zaburi alivyoona juu ya makumbusha ya Mungu. (Zaburi 119:24, 119, 167) Mashahidi wa Yehova wa leo pia hawaudhiki kwa sababu Mungu anaona ni vema kuwakumbusha juu ya mambo yanayohusiana na sheria yake ama kupitia funzo la Biblia lao au kupitia tengenezo lake. Kwa ushikamanifu wanachagua kukamata makumbusha yake. “Nimekamatana na makumbusha yako. O Yehova, usiniaibishe.”—Zaburi 119:31, NW.
5. (a) Makumbusha ya Neno la Mungu na tengenezo lake yanatumikia kusudi gani? (b) Sisi binafsi tunawezaje kuonyesha heshima kubwa kwa makumbusha ya Yehova kama mtunga-zaburi?
5 Mungu hatoi makumbusha yake ili aaibishe Mashahidi wake, bali kupitia kwayo anawalinda wasiingie kwenye mwendo wa aibu. Wanataka kikalio cha shauku chao kiegemee mambo ambayo ni yenye faida kweli kweli daima; kwa hiyo wanajiunga na mtunga-zaburi kusali hivi: “Elekeza moyo wangu kwenye makumbusha yako, wala si kwenye mapato.” (Zaburi 119:36, NW) Kupenda Mungu wao kwa nafsi zao zote kunawasukuma wachukue mwendo huo. Hata ingawa huenda ikamaanisha wasahihishwe vikali, Mashahidi wa Yehova wanafurahi kwamba Yehova anawaongoza kwa njia ya makumbusha yake, ili kuwazuia wasipotee njia na kupotea milele: “Katika njia ya makumbusha yako nimeshangilia, kama vile katika mambo ya thamani mengine yote.”—Zaburi 119:14, NW.
6. Mashahidi wa Yehova wamejaribuje sana kujiendesha kwa unyofu mbele za Mungu?
6 Ingawa wamelaumiwa vikali na hata kukanushwa na wengi kwa ajili ya kufanya makosa, Mashahidi wa Yehova wamejiendesha kwa unyofu mbele za Mungu wao. Wanataka kwenda katika njia ambayo kitabu chake cha makumbusha kinawaonyesha. Historia yao ya kisasa inaonyesha kwamba wametenda kama vile mtunga-zaburi wa kale alivyofanya: “Nimefikiria njia zangu, ili nigeuze hatua zangu kwenye makumbusha yako.” (Zaburi 119:59, NW) Ni kwa kufanya hivyo tu wangeweza kumwomba Mungu awatunze wakiwa hai ili waendelee kufanya kazi aliyoiweka rasmi wajapokuwa maadui wao wenye kiu ya damu. (Zaburi 119:88) Wakiwa wanakubali wazi kwamba wao ni watumwa wa Mungu kwa sababu ya wakfu wao kwake kupitia Kristo na kwamba wanahitaji kuelewa kikweli mambo ambayo ameandika katika Neno lake, wanasema hivi: “Mimi ni mtumwa wako. Nieleweshe, nipate kujua makumbusha yako.”—Zaburi 119:125, NW.
7. Sababu zao za kuwa wenye shukrani ni gani, na wameomba nini katika sala?
7 Mambo ambayo Mungu amefunua katika Neno lake tangu mwisho wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza mwaka wa 1918 ni mazuri ajabu kwao, hata kwamba wanataka kufanya mambo wanayoonyeshwa na mafunuo hayo. (Zaburi 119:129) Yehova amekuwa na haki kabisa kutujulisha makumbusha yake na kutuwekea yawe amri. Tunafurahi kukubali hilo waziwazi kwa njia ya sala kwa maneno ya mtunga-zaburi: “Umeamrisha makumbusha yako katika uadilifu na katika uaminifu wenye kupita.” (Zaburi 119:138, NW) Asante kwa Mungu huyo Mshikamanifu!
8. Ni kwa njia gani uzima wa milele unategemea ufahamu na kutunza makumbusha ya Mungu?
8 Leo Mashahidi wa Yehova wanaelewa sana kwamba kupata kwao uzima wa milele katika mfumo mpya wa mambo wa Mungu wenye uadilifu kunategemea kuelewa kwao mambo anayowajulisha kisha wayatii kwa kuchagua kufanya hivyo. (Zaburi 119:144) Katika ulimwengu wenye uadui wamelazimika kumwomba Msikiaji wa sala wa kimungu awaokoe katika hali zenye kutisha sana, sana sana katika hizi siku ambazo mataifa yote yanakusanywa pamoja kwa ajili ya “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” katika Har–Magedoni. (Ufunuo 16:13-16) Yenye kufaa sana ni sala hii: “Nimekuita wewe. O niokoe mimi! Nami nitatunza makumbusha yako.”—Zaburi 119:146, NW.
9. Tuna uhakikisho gani kwamba tutaendelea kuwa na makumbusha ya kimungu?
9 Ingawa makumbusha yote yaliyoandikwa ya Yehova Mungu yalianzishwa miaka 1,900 iliyopita wakati wa kukamilishwa kwa Biblia ya vitabu 66, yanapatikana leo na yataendelea kupatikana kwetu mpaka wakati ujao usiojulikana. Zaburi 119:152, NW, kama ilivyoelekezwa kwa Mungu, imetimia: “Zamani za kale nimejua mengine ya makumbusha yako, kwa maana kwa wakati usiojulikana umeyaanzisha.” Kwa sababu ya maarifa ya kujua mengine ya makumbusha ya Yehova, gazeti Zion’s Watch Tower and Herald of Christ’s Presence lilianza kuchapishwa Julai wa 1879. Leo, baada ya miaka 105 ya kuchapishwa, gazeti hilo linaendelea kuenezwa. Na linaenezwa ulimwenguni pote katika lugha 102. Hata ikiwa huenda maadui wa Mashahidi wakaruhusiwa kukomesha gazeti hilo, hawataweza kamwe kukomesha Biblia Takatifu yenye makumbusha ya Yehova ambayo yanategemea msingi wa milele, au wenye kudumu mpaka wakati usiojulikana.
Kutekeleza Maagizo ya Mkubwa Wetu
10. Zaburi 119 inayapa “maagizo” ya Mungu umaana gani?
10 Baada ya mtunga-zaburi kushangilia katika mistari yake miwili ya kwanza furaha ya wale wanaotembea katika sheria ya Yehova na kushika makumbusha yake, anaendelea kusema: “Hakika hawakuzoea ukosefu wa adili wo wote. Katika njia zake wametembea. Wewe mwenyewe umetoa maagizo yako kwa kuamrisha ili yatunzwe kwa uangalifu.” (Zaburi 119:3, 4, NW) Katika zaburi hiyo mtungaji anatumia neno “maagizo” mara 21, akiyakumbuka kwa njia hiyo.
11. (a) Kwa sababu gani mtunga-zaburi alikuwa mwangalifu juu ya mwenendo wake kama inavyoonyeshwa katika Zaburi 119:168? (b) Ni nini maana ya neno “maagizo”?
11 Mtunga-zaburi anatuambia jinsi alivyoona na alivyofanya kuhusu “maagizo” hayo ya kimungu. Kwa njia hiyo alitumika kuwa mfano wenye kutegemeka kwetu leo. Yeye alithamini kwamba mwendo huo wa maisha ulikuwa ukiangaliwa na Mungu na kwamba alipaswa kuwa mwangalifu jinsi alivyojiendesha mwenyewe katika agano la Torati la Yehova. Alisema hivi kwa sababu nzuri: “Nimetunza maagizo yako na makumbusha yako, kwa maana njia zangu zote ziko mbele yako.” (Zaburi 119:168, NW) Makumbusha yanachochea akili, lakini maagizo ni maelekezo yanayotolewa na mkubwa kwa mdogo wake. Yanaeleza ni mambo gani ya kufanywa na yanavyopaswa kufanywa na mtumwa, mtumishi, mfanyi kazi au askari kwa njia ya kikazi. Tafsiri ya neno la Kiebrania maagizo, yaani, piqudim’, inamaanisha “miadi; maagizo.” Je! maagizo hayo ya kimungu yalionekana kuwa mzigo au yasiyopendeka kwa mtunga-zaburi, sana sana ikiwa kuyatunza kulifanya mtu ashtakiwe kwa uongo au kusingiziwa? Ebu tumsikilize: “O ona nimependa maagizo yako mwenyewe. O Yehova, kulingana na fadhili zako za upendo unihifadhi hai.”—Zaburi 119:159, 169, NW.
12, 13. (a) Kiwango kilichowekwa na mtunga-zaburi kiliwezeshaje watumishi wa Mungu wavumilie majaribu wakati na baada ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza? (b) Ingawa ‘walipakwa uongo,’ mabaki walitii maagizo ya nani?
12 Mtunga-zaburi aliweka kiwango kizuri kwa ajili ya Wakristo wa kweli wanaoshirikiana na tengenezo linaloonekana la Yehova katikati ya ulimwengu huu wenye kuvunja sheria, usio na upendo! Kuishi kupatana na kiwango hicho kumethawabisha. Katika mazingira yao yenye kujaa maadui wa Mungu wao, wanahisi sawa na mtunga-zaburi, kama “mgeni.” (Zaburi 119:19, 54) Hata hivyo wana maoni kwamba hakuna cho chote kinacholinganika na matakwa ya Mungu ya maisha yanayofaa. Walinusurika wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ya 1914-18. Wakati wa miaka hiyo ya wazimu wa vita maadui walishambulia juu mpaka kwa jamii ya wasimamizi wa tengenezo linaloonekana la Yehova ili waharakishe kuharibu watu wake, hata wakafikia hatua ya kufunga gerezani isivyo haki msimamizi na wanaume wengine wenye madaraka makubwa wa makao makuu ya Watch Tower Bible and Tract Society. Jambo hilo lilikuwa kama Zaburi 119:69 (NW) inavyoeleza: “Wenye kujitanguliza wamenipaka uongo. Kwa habari yangu, kwa moyo wangu wote nitashika maagizo yako.” Mungu Aliye Juu Zaidi, Mkubwa wao, lazima atiiwe kuliko kutii wanadamu walioko hapa chini kwenye kikanyagio cha Mungu.
13 Ndiyo, kwenye upeo wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, ikiwa inaonekana ki-nje-nje wameshinda wenye kutunza maagizo ya Mungu, maadui walihisi kwamba walikuwa wanakaribia kumaliza kabisa watu wa Mungu wenye kutii na waliojiweka wakfu. Kwa hiyo wangeweza kusema: “Walikuwa karibu na kunikomesha katika nchi; lakini sikuyaacha [maagizo] yako.” (Zaburi 119:87) Aliye Mkuu Zaidi wa ulimwengu wote alishinda hila ya maadui hao wenye kujitanguliza walio waoga wenye kuonea.
14. Ni katika maana gani mabaki wangeweza kusema maneno ya Zaburi 119:45?
14 Baada ya kukombolewa vita ikiisha kumalizika, walihisi uhitaji wa kutafuta maagizo ya Mungu kwa njia kubwa kupita wakati uliotangulia wo wote ili wajifunze aliyokusudia wafanye katika kipindi hicho cha amani kisichotazamiwa. Wangeweza kusema maneno ya Zaburi 119:45: “Nami nitakwenda panapo nafasi, kwa kuwa nimejifunza [maagizo] yako.”
Sasa na Mpaka Wakati Ujao
15. (a) Ni maoni gani yanayosemwa katika Zaburi 119 ambayo watu wa Mungu wameyafanya yakawa yao? (b) Wamekaza fikira kufanya nini tangu mwaka 1919?
15 Maadui wao wameongezeka kwa kadiri ambavyo kazi yao ya Ufalme imeenea mpaka sehemu za mwisho za dunia. Lakini hilo haliwaogopeshi hata wazime mafundisho ya Mungu katika akili zao. Kwa kuazimia wanaendelea. (Zaburi 119:93, 94) Kwa sababu ya kutokuwa wasikiaji wa Neno la Mungu wenye kusahau, kutia ndani makumbusha yake yenye kufaa, bali wakiwa wamekwisha kuwa watendaji wa kazi yake, sasa wanaweza kusema nini bila kujivuna, wakimpa Yehova sifa? Wakisema hivi: “Naenenda kwa ufahamu zaidi kupita wanaume wazee, kwa sababu nimeshika maagizo yako mwenyewe.” (Zaburi 119:100, 104, NW) Kwa hiyo tangu mwaka uliofuata vita wa 1919 kuendelea, hawajajishughulisha na mipango ya mataifa. Bila kuondoshwa kando wametangaza Ufalme wa Mungu kupitia Kristo kuwa tumaini moja la pekee kwa wanadamu, badala ya Ushirika wa Mataifa na mrithi wa sasa wa huo, Umoja wa Mataifa. Lo! huo ni “ufahamu”!
16. Ingawa tunakazwa tufanye yaliyo mabaya, sisi tuna uhakika juu ya jambo gani?
16 Wakati Neno la Mungu linapotuambia sisi tunaoishi katika kipindi hiki cha Umoja wa Mataifa tusiupende ulimwengu huu na vitu vyake, linatuambia maagizo ya kimungu tuliyokusudiwa. Ni lazima tuyaone kuwa ya haki! Nasi tunayaona ni ya haki! Nayo ni ya haki! Tunachukua msimamo wetu pamoja na Zaburi 119:128 (NW): “Hiyo ndiyo sababu nimefikiria maagizo yote kuhusu mambo yote kuwa ni ya haki; kila kijia cha uongo nimechukia.” Kwa ajili ya msimamo wetu usiogeuka-geuka huenda tukadharauliwa na walimwengu, lakini jambo la maana ni jinsi Mungu anavyotuhesabu, na kwa hiyo hatutaki maelekezo yake yaponyoke akili zetu.—Zaburi 119:141.
17. Ni mataraja gani yaliyo mbele, na ulinzi wa kimungu utapatikanaje wakati wapinzani watakapokaribia washambulie watu wa Yehova?
17 Kujapokuwa kuzidishwa kwa kuhubiri Ufalme wa Mungu kupitia Kristo kuwa tumaini pekee la ulimwengu wa wanadamu sasa kwa miaka zaidi ya 60, wakusudiaji na wapangaji wa mambo ya ulimwengu hawasikilizi. Sasa jamaa yote ya kibinadamu iko katika hatari ya kufagiliwa mbali na silaha za nyukilia. Si hilo tu, bali pia chuki ya kupinga dini inatia uchungu mioyo ya kibinadamu zaidi na zaidi. Namna zote za dini ya uongo zikiisha kuharibiwa, maadui wa Mungu watalazimika kushughulika na Mashahidi wa Yehova. Wapinzani wasiofuata dini wa Ufalme wa Mungu watakapokaribia mashahidi wa Yehova waliobaki, wao watahitaji nguvu zinazopita za kibinadamu kupita wakati mwingine uliotangulia. Itakuwa lazima wafunikwe kwa uvuli wenye kulinda wa mkono wenye uwezo wote, mkono wa Mungu. Watakuwa na msingi wa kulilia mkono huo wa kimungu uje kuwasaidia, kama vile tu inavyosemwa katika Zaburi 119:173 (NW): “Mkono wako utumike kunisaidia, kwa sababu nimechagua maagizo yako.” Katika hali hizo zenye kutatiza, mkono wa Yehova hautakuwa mfupi sana usiweze kukilia, hata ushindwe kuokoa washikaji-maagizo yake wenye kumwogopa Mungu.—Isaya 50:2.
18. (a) Kwa sababu gani kushirikiana na wanaofaa kutaamua kama mtu ataokoka au hataokoka mwisho wa mfumo huu wa mambo? (b) Tukiwa tunajua matokeo kwa wale wanaomwogopa Yehova, daima tutajishughulisha na jambo gani?
18 Tunapokaribia mwisho wenye msiba wa huu mfumo wa mambo wenye kuvunja sheria, usio na upendo na mwisho wa kubagua watu wa mataifa, sawa na wakati mchungaji anapobagua kondoo zake na mbuzi, sisi tunataka tukutwe tukiwa tunashirikiana na nani? Tukishirikiana na wenye mfano wa mbuzi watakaoharibiwa kwa umilele wasiwepo tena au tukishirikiana na wanaompenda Yehova ambao ni wenye mfano wa kondoo? (Mathayo 25:31-46) Sasa si mapema mno kuchagua wenzi wanaofaa. Sasa ndio wakati wa kufanya uchaguzi wa mtunga-zaburi, aliyesema hivi juu ya Aliye Mkuu Zaidi: “Mimi ni mshirika wa wale wote wanaokuogopa wewe, na wa wale wanaotunza maagizo yako.” (Zaburi 119:63, NW) Tunajua ni nini itakuwa sehemu ya wale wanaomwogopa Yehova Mungu, nasi tunataka kushiriki pamoja nao katika sehemu hiyo yenye kuridhisha nafsi, iwe kwa furaha ya Yehova mwenyewe. Kwa sababu tunampenda, daima tunashughulikia sana kumpendeza kwa kufanya anayotaka tufanye. Mtunga-zaburi anaeleza vizuri azimio letu, akisema: “Nitajishughulisha na maagizo yako, na mimi nitaangalia vijia vyako.”—Zaburi 119:15, NW.
19. Ni kazi gani nzuri ajabu inayoendeshwa sasa?
19 Tangu kumalizika kwa vita ya ulimwengu, iliyokuwa ya kwanza kwa namna yake, mwaka wa 1918, Mungu Aliye Juu Zaidi ameendesha kazi nzuri sana katikati ya ulimwengu wenye kupinga. Ni kazi ya kuwaagiza Mashahidi wake wahubiri “habari njema hizi za ufalme . . . katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote,” “mwisho” wa huu mfumo wa mambo ambao umekuwako kwa maelfu ya miaka ukiwa unakaribia. (Mathayo 24:14, NW) Tunataka kushiriki pamoja naye katika kazi zake. Tunataka kufanya mapenzi yake, na kwa hiyo tunamuuliza atufanyishe mapenzi yake. Sala yetu ya moyoni ingali ile ya Zaburi 119:27 (NW): “Nieleweshe njia ya maagizo yako mwenyewe, ili nijishughulishe na kazi zako za ajabu.”
20. Ni kazi gani ya Mungu ya ajabu ambayo ingali itafanywa, na wale watakaohifadhiwa hai watasema nini juu ya maagizo ya Mungu?
20 Mojawapo kazi za Mungu ya ajabu zaidi, ambayo ingali itafanywa, itakuwa ile ya kuhifadhi mashahidi wake waaminifu na washikamanifu wapite mwisho unaokuja wa huu mfumo wa mambo na kuingia katika Utaratibu Mpya. (2 Petro 3:13) Utakuwa uadilifu upande wake kuwalinda waokoke kifo cha huu mfumo wa mambo wenye ugonjwa wa kuua. Yeye atajibu sala hii iliyoongozwa kwa roho yake ambayo wao wanatoa: “Tazama! nimetamani maagizo yako. Katika uadilifu wako unihifadhi hai.” (Zaburi 119:40, NW) Hiyo na iwe sala yako. Kisha, baada ya dhiki kubwa zaidi ya historia yote ya ulimwengu na ukiwa salama kwenye mlango wa mfumo wa mambo ulio mpya na wenye uadilifu, utachochewa useme hivi kwa moyo mweupe: “Mpaka wakati usiojulikana sitasahau maagizo yako, kwa sababu kupitia hayo umenihifadhi hai.”—Zaburi 119:93, NW.—Kutoka w6/15/84.
Kikumbusho
◻ Ni “makumbusha” gani kutoka kwa Mungu yenye kupatikana kwako?
◻ Unaweza kufaidikaje na makumbusha ya Mungu?
◻ “Maagizo” ya Yehova ni nini?
◻ Kwa sababu gani utake kuyatekeleza?
[Picha katika ukurasa wa 20]
Watumishi wa Mungu leo wana “makumbusha” zaidi ya kujifaidi nayo
[Picha katika ukurasa wa 22]
Je! wewe umekwisha kuchagua kuwa ‘mshirika wa “kondoo” wanaotunza maagizo ya Mungu’?