Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 4/15 uku. 21
  • Kujua Yaliyo Katika Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujua Yaliyo Katika Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Matunda ya Dini
  • Kutibu Dalili za Magonjwa, Si Ugonjwa Wenyewe
  • Uhai Kabla ya Kuzaliwa
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutoa Mimba?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Uhai Huanza Wakati Gani?
    Amkeni!—1991
  • Kuiheshimu Zawadi ya Uhai
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 4/15 uku. 21

Kujua Yaliyo Katika Habari

Matunda ya Dini

Kuifanya dini iwe biashara kumetokeza “ufisadi, ukosefu wa adili na namna nyingine za kukosa nidhamu katika makanisa yetu,” akatangaza askofu wa Kanisa la Kimethodisti katika Nigeria. Kulingana na gazeti Daily Times la Nigeria, yeye alikiri kwamba kanisa lilishiriki kulileta wimbi la uhalifu katika jamii ya watu ya Nigeria kwa “kuchangisha pesa na kupokea zawadi kutoka kwa wahalifu na maafisa wa mitaa walio wafisadi.”Alisema pia kwamba kujiendesha vibaya kwa viongozi wa kidini na washiriki kumegeuza kanisa likawa “mahali pa wafanya fujo, wapunjaji, na vitendo vya ukosefu wa adili.”

Femi Abbas, mwelezaji juu ya mambo ya Kiislamu, alilishirikisha pia ongezeko la uhalifu na mmiminiko wa watu kuingia katika vikundi vya kidini vyenye ubiashara mwingi. Akiandika katika gazeti National Concord la Nigeria, alisema kwamba viongozi wa vikundi hivyo walipata wafuasi kwa kutumia “maneno matamu, ujanja na uwezo wa kuwashinda wengine kwa akili,” naye akaeleza kwamba wao “wanasingizia wasivyo kwa kujifanya wana imani.”

Matunda mabaya hayo yanapasa kutazamiwa kuwapo wakati dini inapokaza fikira juu ya vitu vya kimwili. Wao wanauthibitisha usahihi wa unabii wa Biblia kwamba katika “siku za mwisho” watu wangekuwa “wenye kupenda fedha, . . . wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake.” “Hawatakubali fundisho linalofaa, bali, kwa kulingana na tamaa zao wenyewe, watajikusanyia kwa wingi walimu kwa ajili yao ili watekenywe masikio.” Kwa upande mwingine, dini ya kweli inaweza kutazamiwa ikazie mambo ya kiroho wala si vitu vya kimwili. Hivyo ingewachochea watu ambao maisha zao zenye kuheshimika zinawafanya wawe raia bora na pia watumishi waaminifu wa Mungu.—2 Timotheo 3:1-5, UV; 2Ti 4:3, NW; Mathayo 6:19-21,33; 7:16-21.

Kutibu Dalili za Magonjwa, Si Ugonjwa Wenyewe

“Wasichana Waingereza Wanaweza Kupata Kibonge cha Kuzuia Uzazi Bila Ruhusa,” kikasema kichwa cha makala moja ya gazeti The New York Times. Makala hiyo ilifunua kwamba: “Kupitia kura ya 3 kwa 2, waheshimiwa wa kisheria wa sehemu ya bunge inayoitwa Ukumbi wa Waheshimiwa walisema kwamba wazazi hawana mamlaka kamili juu ya watoto wao na kwamba ni lazima sheria iendelee kurekebika kulingana na mielekeo ya kijamii inayobadilika.” Sasa madaktari Waingereza wamepewa na sheria uwezo wa kuandikia wasichana wa miaka inayopungua 16 dawa za kuzuia uzazi bila kuomba wazazi wao ruhusa. Sheria hiyo iliyopitishwa na ukumbi wa waheshimiwa ilisifiwa na Chama cha Wafanya Kazi, Shirika la Tiba Uingereza, na mashirika mbalimbali ya kupanga uzazi.

Kusudi la sheria hiyo linasemwa kuwa ni ‘kuzuia uchukuaji na utoaji wa mimba zisizotakwa za vijana-matineja.’ Lakini je, njia hiyo ya kushughulika na tatizo gumu linaloongezeka haitibu “dalili” zenyewe tu? Wakati watunga sheria, kwa kuungwa mkono na madaktari na matengenezo ya kijamii katika nchi yenye kuona fahari juu ya mapokeo yayo ya Kikristo, wanapopitisha sheria inayoendeleza kwa njia isiyo ya moja kwa moja ule “ugonjwa” wa uasherati wa vijana-matineja, je, hiyo haionyeshi jinsi nyakati zetu zilivyo?

Hakika njia iliyo bora zaidi ya kulinda wasichana-matineja wasidhihirishe “dalili” za uchukuaji na utoaji wa mimba zisizotakwa ni kuwafundisha maadili yanayowalinda na mwenendo mbaya wa ngono. Ghala lililothibitishwa kuwa lenye maadili hayo ni Biblia, ambayo pia inaonyesha mahali ambapo matibabu ya “ugonjwa” huo yanapatikana—kwa wazazi wanaopewa daraka la kutoa jibu juu ya mwenendo wa watoto wao.—Waefeso 5:5; 6:1-4.

Uhai Kabla ya Kuzaliwa

“Hisia za watoto wasiozaliwa zinaanza kujionyesha mapema kuliko tulivyokuwa tumedhania; na sehemu ndogo sana zilizo za maana na uwezo mbalimbali katika ubongo unaanza kukua mapema kuliko ilivyodhaniwa hivi majuzi.” Hivyo ndivyo wanavyoandika watungaji wa kijitabu Life Before Birth, kilichochapishwa mwaka 1984 katika Jamhuri ya Muungano wa Ujeremani na Waziri wa Serikali wa Ujana, Jamaa na Afya. Wanataja juu ya uhai usiozaliwa kuwa ni uhai ulio katika “namna yake ya udhaifu kabisa,” wakionyesha kwamba “uhusiano wa kwanza-kwanza wa mtoto na wazazi wake unafanyika tayari katika mimba.” Wanasema kwamba ingawa wanasayansi wengi hapo kwanza waliamini kwamba uhai usiozaliwa unapitia hatua-hatua za mageuzi, ukikua kutokana na chembe moja na kuwa samaki kisha kuwa mnyama wa maji na nchi kavu kabla ya kuwa mwanadamu, sasa nadharia hiyo imekataliwa kwa sababu “sayansi imefanya maendeleo.” Wanakiri kwamba ‘siku hizi hakuna mtu anayeng’ang’ania kwamba uhai usiozaliwa unakuwa haujawa mwanadamu mwenye uhai. Mwanadamu hawi mwanadamu mara ya kwanza anapozaliwa.’

Mambo hayo yaliyogunduliwa yanapatana na jinsi Muumba wa uhai anavyomwona mtoto asiyezaliwa—kuwa kipumuaji chenye uhai. Akimwambia Muumba wake, Daudi mtumishi wa Mungu aliandika hivi: “Uliniunga tumboni mwa mama yangu. Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa kwa jinsi ya ajabu ya kutisha . . . Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; chuoni mwako ziliandikwa zote pia.”—Zaburi 139:13, 14, 16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki