Kuyafuata Kwa Uangalifu Maagizo ya Mfalme
“Nijishughulisha na maagizo yako, na mimi nitaangalia vijia vyako. Kwa sheria zako mimi nitaonyesha kutamani sana. Mimi sitasahau neno lako.”—ZABURI 119:15, 16,NW.
1. Kwa sababu gani kila mtu na kila kitu kiko chini ya maagizo ya Yehova?
KILA mtu na kila kitu kiko chini ya maagizo ya Mungu Mwenye Nguvu Zote Yehova, yule Mfalme wa umilele. Yeye ndiye aliyeumba ulimwengu mzima. Yeye ndiye Chanzo cha uhai wote. Yeye ndiye aliyeifanyiza dunia na kuitayarisha ikaliwe. Yeye ni Mungu wa utaratibu, na kwa kufililiza sheria zake, utaratibu utadumishwa katika sehemu zote za uumbaji wake.—Zaburi 36:9: Isaya 45:18; Ufunuo 15:3.
2. Ni nani anayeziongoza mbingu zenye nyota, na jinsi gani?
2 Yehova Mungu ndiye aliyeziagiza mbingu zenye nyota zitandae kama hema juu ya dunia halafu akaalika watu wake akiwaambia: “Inueni macho yenu juu mkaone; ni nani aliyeziumba hizi; aletaye nje jeshi lao kwa hesabu; aziita zote kwa majina.” Yehova ndiye aliyemwuliza Ayubu hivi: “Je! unazijua amri zilizoamuriwa mbingu? Waweza kuyathibitisha mamlaka yake juu ya dunia? ” Sheria Zake za uvutano na mwendo ndizo zinazofunganisha pamoja yale mamilioni ya galaksi zenye mabilioni ya nyota na kuongoza usafiri ya dunia inapopita katika anga. Isaya 40:26; Ayubu 38:33.
3. Ni kwa maagizo ya nani wanyama wanaendelea kuwa hai, na ingetukia nini kama wao hawangetii?
3 Yeye ndiye anayetokeza mimea ya kijani inayokuwa zulia la kupamba dunia. Ni kwa maagizo yake kwamba mbegu zinachipuka na kukua na kuzaa tena. Katika dunia mna namna nyingi sana zisisohesabika za uhai wa wanyama—kuanzia zile ncha zayo za kaskazini na kusini mpaka kwenye misitu iliyo na majira ya tropiki, kuanzia juu kule angani mpaka ndani sana ya udongo, kuanzia kwenye uso wa bahari kuu mpaka ndani kabisa ya sehemu zayo zilizo na giza zaidi. Ili wanyama hao waishi, kila mmoja ya aina hizo zisizohesabika ni lazima aishi kama ilivyoagizwa na Yehova. Kupitia tabia ya silika, yeye anaingiza ndani yazo mipango ya kufuata ili ziendelee kuwapo. “Zina hekima ya silika.” (Mithali 30:24, NW ) Lakini namna gani kama yule ndege mdogo mtetemesha-sauti wa Alaska angejiambia hivi, ‘Mimi sitaruka maelfu ya maili kwenda Amerika Kusini. Mbona nifanye hivyo? ’ Mtetemesha-sauti huyo mdogo angekufa katika pepo zenye baridi nyingi za majira ya kipupwe. Lakini ndege huyo hatasema hivyo. Yeye amepangiwa ndani yake kuhama ili aendelee kuwa hai. Ndivyo ilivyo na wanyama wote. Wao wanafuata kwa tabia ya silika maagizo yalioingizwa ndani yao na Yehova Muumba wao. Hawana uchaguzi wao wenyewe katika jambo hilo.
4. Watu wana mambo gani ya kuchagua, na matokeo ni nini?
4 Lakini watu ni tofauti. Sisi tumeumbwa kwa sura ya Mungu, nasi tunaweza kujifanyia uchaguzi. Lakini, ingawa Yehova hakuingiza ndani yetu mipango ya kututendesha kwa hekima kwa kutegemea silika tu, wala yeye hakutuacha bila kujua la kufanya. Kupitia Neno lake Biblia, yeye anatupa sisi maagizo yake ya kupatia uzima. Tukiyafuata kwa uangalifu maagizo haya ya Mfalme, tutaishi. Tukitumia uhuru wetu kuyapuuza na kufuata barabara ya kujitegemea wenyewe, tutakufa. Ni lazima sisi tujipange wenyewe kwa njia itakayotuwezesha kuendeleza, uhai. Ni hivyo tu, hakuna zaidi. “Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu,” akasema mtunga zaburi. Kwa upande mwingine, “barabara [tofauti] huenda ikaonekana kama kwamba ni nyofu kwa mtu, hata hivyo huenda ikaja kuwa ndiyo njia ya kifo.” (Zaburi 119:105; Mithali 14:12, The New English Bible) Katika wakati huu wa mwisho, ni lazima tujihusishe wenyewe na maneno ya Zaburi 119:15, 16, ambayo Yehova anaambiwa: “Nitayatafakari mausia [maagizo, NW ] yako, nami nitaziangalia njia zako. Nitajifurahisha sana kwa amri zako, sitalisahau neno lako.”
Yehova Mtengenezaji wa Watu Wake
5. Ni kwa njia zipi Yehova alikuwa Mwaamuzi wa Israeli, Mpaji sheria, na Mfalme?
5 Yehova alinena na Musa juu ya Mlima Sinai, akampa maagizo ya kuongozea Israeli. Kati ya maagizo hayo, zenye kutokeza zaidi zilikuwa ni zile Amri Kumi, zilizoandikwa katika mbao za mawe kwa kidole cha Mungu. (Kutoka 20:1-17; 31:18) Zaidi ya kuwa Mpaji sheria wa Israeli, Yehova alikuwa ndiye Hakimu wao, akitenda kupitia Musa na wanaume wengine wazee. Musa aliwaonya kwa upole wanaume hao wazee wakumbuke hivi: “Msitazame nafsi za watu katika hukumu; mwasikize wadogo na wakubwa sawa sawa: msiche uso wa mtu awaye yote; kwa kuwa hukumu ni ya Mungu.” (Kumbukumbu 1:17) Yehova alikuwa ndiye Mfalme wao pia, mwenye kuyapanga kitengenezo mamilioni hayo ya watu ili waendeshe vizuri mambo yao. Kwa sababu hiyo, mmoja wa manabii wake angeweza kutangaza hivi baadaye: “[Yehova] ndiye mfanya sheria wetu; [Yehova] ndiye mfalme wetu.”—Isaya 33:22.
6. Yehova alithibitikaje kuwa Mtengenezaji na Mwongozi wa Israeli jangwani?
6 Taifa la Israeli lilipangwa kitengenezo katika makabila, jamaa, na nyumba za ukoo. Walipokuwa wakisafiri jangwani, Yehova aligawia kila kabila mahali palo katika mwendo huu wa kupiga miguu. Walipopiga kambi kuzunguka lile hema takatifu, kila kabila lilikuwa na mahali palo lilipogawiwa.’ (Hesabu 2:1-34; Yoshua7:14) Yehova alikuwa akiwaagiza wahame-hame kwa kutumia wingu: “Na kila lilipoinuliwa lile wingu juu ya ile Hema, ndipo wana wa Israeli waliposafiri: na mahali lilipokaa lile wingu, ndipo wana wa Israeli walipopiga kambi yao. Kwa amri [agizo, NW ] ya [Yehova] wana wa Israeli walisafiri, na kwa amri [agizo, NW ] ya [Yehova] walipiga kambi.”—Hesabu 9:17, 18.
7. Ni nani angeweza kufanya na kwa kweli akafanya mabadiliko katika tengenezo la Israeli?
7 Wakati badiliko la kitengenezo lilipohitajiwa, Yehova alilifanya. Musa alilalamika hivi: “Mimi siwezi kuwachukua watu hao wote peke yangu, kwa kuwa ni mzigo mzito sana wa kunishinda.” Yehova alijibu: “Nikusanyie watu sabini, miongoni mwa wazee Waisraeli, ambao wewe wawajua kuwa ndio wazee wa watu hao, na maakida juu yao, . . . nao watachukua mzigo wa watu hao pamoja nawe, ili usiuchukue wewe peke yako.” (Hesabu 11:14, 16, 17) Hata wakati watu badaaye walipodai wapewe mfalme wa kibinadamu, yule Mfalme mkuu wa umilele hakuwaachilia Israeli. Mfalme wa kibinadamu alikuwa na nakala ya sheria ya Yehova. Manabii walitangaza hukumu za Yehova. Wafalme waaminifu bado walitumikia wakiwa wasimamizi kwa ajili ya Mungu ‘walipoketi juu ya kiti cha enzi cha Yehova.”—Kumbukumbu 17:18; 2 Wafalme 17:13; Yeremia 7:25; 1 Mambo ya Nyakati 29:23, NW.
Yule Aliye Mfano Mkamilifu wa Kufuata Maagizo ya Mfalme
8. Ni jinsi gani, mahali gani, na kwa matokeo gani Yesu alitangaza Ufalme wa Yehova uliokuwa ukija?
8 Yesu alipofika akiwa ndiye Masihi aliyeahidiwa, yeye alifuata maagizo ya Baba yake ya kimbingu kwa bidii yenye kumula. Ilipoanza ile huduma kubwa ya Galilaya, yeye “alianza kuhubiri na kusema, “Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia. Naye alikuwa akizunguka katika Galilaya yote, akifundisha katika sinagogi yao, na kuihubiri Habari Njema ya ufalme na kuponya ugonjwa na udhaifu wa kila namna katika watu. Na makutano mengi wakamfuata, kutoka Galilaya na Dekapoli, na Yerusalemu, na Uyahudi, na ng’ambo ya Yordani.” (Mathayo 4:17, 23, 25; Yohana 2:17) Yeye hakuhubiri kwenye masinagogi tu. Alitangaza habari njema za Ufalme ko kote ambako watu walisikiliza: hekalu, pwani kando za milima, katika nyanda, miji na vijiji, na katika nyumba za watu. Makutano ya watu yalimmiminikia, “wakimsikiliza kwa furaha.” Wao “walikuwa wakiandamana naye, wakimsikiliza.”—Marko 12:37; Luka 19:48.
9. Yesu alifanya nini aipanue kazi ya kuhubiri, na alitoa maagizo gani?
9 Yeye aliwaambia mitume wake kwamba kulikuwa na uhitaji wa wafanyakazi zaidi, kwa hiyo “hao Thenashara Yesu aliwatuma, akiwaagiza, akisema: “Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie. Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia. Na mji wo wote au kijiji cho chote mtakachoingia, tafuteni ni nani humo aliye mtu mwaminifu; mkae kwake hata mtakapotoka. Nanyi mkiingia katika nyumba isalimuni. Na nyumba ile ikistahili, amani yenu na iifikilie; la, kwamba haistahili, amani yenu na iwarudie ninyi.” (Mathayo 10:5-7, 11-13).Baadaye alituma wengine 70 wakiwa na maagizo kama ayo hayo, na kwa kuyafuata kwa uangalifu maagizo hayo walipata mafanikio na furaha kuu.—Luka 10:1, 17.
10. (a) Baada ya kufufuliwa, Yesu aliondoa kizuizi gani, na matokeo yalikuwa nini? (b) Kwa sababu gani kuwekwa rasmi kwa wanaume fulani kulihitajiwa, na ni matakwa gani yaliyopaswa kutimiza?
10 Baada ya kufa na kufufuliwa, Kristo Yesu alikiondoa kile kizuizi cha kuhubiri nyumba ya Israeli tu, akiwaambia wafuasi hivi: “Mimi nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kwa kuwabatiza katika jina la Baba na Mwana na roho takatifu, kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.” (Mathayo 28:18-20; NW ) Alipopaa mbinguni, alitoa agizo kama hilo: “Mtakuwa mashahidi wangu mimi katika Yerusalemu na katika Yudea yote na katika Samaria na kwenye sehemu za mbali zaidi sana za dunia.” (Matendo 1:8, NW ) Wafuasi wake walipokuwa wakiueneza ujumbe wa Ufalme, maelfu ya watu walijiunga nao (Matendo 2:41; 4:4; 5:14; 6:7) Makundi yalichipuka kila mahali. Waangalizi na Wasaidizi wa huduma waliotimiza sifa za Kimaandiko waliwekwa rasmi wayachunge makundi hayo ya wanaume na wanawake. Makundi yalisitawi sana na kuongezeka hesabu.—1 Timotheo 3:2-10, 12, 13; Tito 1:5-9.
11. Mashahidi wa Yehova wana tengenezo la aina gani leo, na kwa sababu gani tengenezo lenye kufanya kazi vizuri linahitajiwa sana sasa?
11 Leo ni jambo la maana sana makundi ya Mashahidi wa Yehova yafuate mfano wa Yesu katika kuhubiri. Ili yafanye hivyo kwa njia yenye matokeo mazuri, yanafuata muundo wa kitengenezo ulioanzishwa siku za mitume. Sisi tumo katika wakati wa mwisho, wakati ambao Yesu alitabiri kwamba kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote ingetukia: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote, inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14, NW ) Baada ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, maelfu wachache walianza kutangaza habari njema hizi za Ufalme; sasa hesabu zao zimeongezeka sana wakawa zaidi ya milioni tatu! Huu ni wakati wa haraka kufuata kwa uangalifu maagizo ya Yule mfalme mkuu wa umilele, Yehova Mungu na pia ya Mfalme wa wafalme Kristo Yesu.
Wazee Wanahitaji Kuheshimiwa na Kuungwa Mkono Nawe
12. Ni mambo gani yanayotakwa kwa wazee leo, na ni jinsi gani utumishi wao unavyoweza kufanywa ujawe na furaha?
12 Katika kufuata maagizo ya Mfalme, wazee wa kundi wana daraka kuu. Wao wanapaswa kuwa mifano myema: “Lichungeni kundi la Mungu lililo katika uangalizi wenu, si kwa kulazimishwa bali kwa moyo wa kupenda: wala si kwa kupenda pato la udangalifu, bali kwa bidii; bali si kwa kupiga ubwana juu ya wale ambao ni urithi wa Mungu, bali mwe mifano kwa kundi.” (1 Petro 5:1-3, NW ) Ni kundi la Mungu. Yeye anawapasisha wazee wajibu wa kumtolea hesabu, lakini kazi yao inaweza kujawa na furaha kila mtu akiwapa ushirikiano wa kutii: “Iweni wenye kutii wale wanaoongoza kati yenu na kuwa wenye kunyenyekea, maana wanaendelea kulinda nafsi zenu kama wale watakaotoa sababu; kwamba wapate kufanya hivyo kwa furaha si kwa kusikitika, maana hilo lingekuwa lenye kuleta hasara kwenu ninyi.”—Waebrania 13:17, NW.
13. Kwa sababu gani wazee wanapaswa kuonyeshwa heshima mara mbili?
13 Wote katika kundi wanapaswa kuonyeshwa heshima, lakina sana-sana wazee wanaofanya kazi kwa bidii: “Acheni wanaume wazee wanaosimamia kwa njia nzuri wahesabiwe kustahili heshima mara mbili, hasa wale wanofanya kazi ngumu katika kusema na kufundisha.” (1 Timotheo 5:17, NW; Warumi 12:10, UV ) Kwa sababu gani wazee wapewe “heshima mara mbili”? Kwa sababu ya kazi yao nzuri. Imeandikwa hivi juu yao: “Roho takatifu imeweka ninyi kuwa waangalizi, kuchunga kundi la Mungu.” (Matendo 20:28, NW ) Wao wanatia bidii kukutumikia wewe na wengine. Huenda ikawa lazima wawape nidhamu watu fulani fulani wakati maagizo ya Mfalme yanapopuuzwa au yanapovunjwa—kazi isiyopendeza ambayo huenda ikaudhi wengine. Huenda ikawa lazima mashauri juu ya mavazi au mwenendo yatolewe na huenda watu wakachukizwa nayo. Hata hivyo mambo yote hayo yanafanywa kwa ajili ya masilahi ya kiroho ya kundi. Wazee wanapaswa kuheshimiwa na kustahiwa.
14. (a) Kulingana na Yakobo 4:12, ni kwa njia gani tu maamuzi yanayofanywa na wazee yanaweza kufaa? (b) Ni wakati gani hukumu inapoweza kupunguzwa, na ni wakati gani rehema iwe kuu kuliko hukumu?
14 Nyakati nyingine inakuwa lazima wazee watumikie katika halmashauri za hukumu na kufanya maamuzi—nyakati nyingine yasiyopendwa na wengi. Kuhukumu huko kunalinganaje na Yakobo 4:12? Hapo panasema: “Mtoa sheria na mwenye kuhukumu ni mmoja tu, ndiye awezaye kuokoa na kuangamiza. U nani wewe umhukumuye mtu mwingine? ” Ndiyo, watu mmoja mmoja hawapaswi kuhukumiana. Zaidi ya hilo, maamuzi yanayofanywa na wazee hayapasi kuwa kulingana na maoni yao wenyewe bali kulingana na neno la Yehova. Angalia jinsi Mfalme Yehoshafati alivyowatahadharisha mahakimu aliyowaweka rasmi: “Hammfanyii mwanadamu hukumu, ila [Yehova]; . . . hofu ya [Yehova] na iwe juu yenu; angalieni mkaifanye; kwa maana [Yehova], Mungu wetu, hapana uovu, wala kujali nafsi za watu, wala kupokea zawadi [hongo, NW ] .” (2 Mambo ya Nyakati 19:6, 7) Ni lazima tengenezo liwekwe katika hali ya usafi. Hata hivyo haiwapasi wazee kuwa wakali-wakali. ‘wapiga watu.’ Rehema na msamaha zinaweza kuonyeshwa wakati majonzi yanapokuwa ya kina kirefu na toba inapokuwa ya kweli. ‘Rehema itashangilia kwa ushindi juu ya hukumu, ikiwa ni kuu kuliko hukumu.’—1 Timotheo 3:3; Yakobo 2:13, NW; ona maaelezo ya chini katika NW Reference Bible.
15. Ni utumishi gani mbalimbali unaotolewa na wazee unaofanya wastahili heshima na staha?
15 Kwa hiyo mara nyingi kazi za wazee ni ngumu na zenye kuwadai mengi, lakini wazee wanaotunza kwa uaminifu na upendo madaraka hayo wanaweza kuwa chanzo cha burudisho na ulinzi wa kiroho. “Ni lazima kila mmoja awe kama mahali pa kujificha na upepo na mahali pa ficho kutokana na tufani ya mvua, kama vijito vya maji katika nchi isiyo na maji, kama kivuli cha mwamba mzito katika nchi isiyo na kitu.” (Isaya 32:2, NW ) Mlinzi mwenye fadhili na upendo—si mshitaki mwenye haraka haraka wala mtia-nidhamu mkali-mkali—ndiye anayewaletea wote furaha, anayejipatia heshima na staha, na kupata kibali ya Yehova.
Onyeshaneni Subira
16. (a) Watu fulani wanatendaje kwa sababu ya makosa ya wengine, na ni jambo gani linaloweza kuwafanya wapunguze hali yao ya kulaumu na kuwa wenye ufahamu zaidi? (b) Yehova anawaonaje watumishi waaminifu wanaofanya makosa?
16 Wakati wo wote watu wanapofanya kazi pamoja wakiwa karibu karibu, matatizo yataelekea kutokea. Makosa yanafanywa. Wakati hilo linapotokea, wengine wanasumbuka sana mawazo. Watu fulani hata wanatumia makosa ya wengine kuwa udhuru wa kufanya kosa lililo kubwa zaidi ya yote—kuacha kumtumikia Yehova! Lakini, wakiyachunguza kwa uangalifu mwingi makosa yao wenyewe kama vile wanavyofanya ya wengine, inaelekea kuwa watapunguza hali yao ya kulaumu na kuwa wenye ufahamu zaidi. Musa alifanya makosa. Ndivyo na Daudi. Ndivyo na Petro, Ndivyo sisi sote tunavyoyafanya. Lakini Yehova aliendelea kuwatumia watu hao waaminifu wa kale, naye anaendelea kututumia sisi. Kwa hiyo je, “wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Na, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha.”—Warumi 14:4.
17. Kuhusu shauri hili la kufanya makosa na kuhukumu wengine, ni mambo gani zaidi tunayopaswa kukumbuka?
17 Na tukumbuke pia: Hapa duniani, Yehova anatumia watu wasiokamilika—hao tu ndio aliyo nao kwa sasa. Kwa kweli, jambo hilo linaonyesha Yehova anastahili sifa. Yeye anatimiza mengi sana kwa kutumia vitu haba sana! Udhaifu wetu unatukuza uwezo wake: “Neema yangu yakutosha maana uwezo wangu hutimilika katika udhaifu.” (2 Wakorintho 12:9) Kazi ya kutoa ushuhuda ulimwenguni pote inapata ufanisi kwa sababu ile inayotolewa na Yehova mwenyewe: “Si kwa jeshi, wala kwa uwezo, bali kwa roho yangu.” (Zekaria 4:6, NW ) Kwa hiyo na tuwe wenye kusamehe makosa na hali za kutokukamilika za wengine ili zetu wenyewe ziweze kusamehewa. Kumbuka: “Mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.”—Mathayo 6:14, 15.
Wapangwa Kitengenezo Wafuate Agizo la Mfalme Kuhubiri
18. Ili kutoa mwelekezo wenye umoja kwa kazi ya kuhubiri ya makundi, ni mpango gani uliokuwapo siku za mitume na uliopo sasa siku zetu?
18 Mitume na wanaume wazee waliokuwa Yerusalemu walijumlika kuwa baraza lenye kuongoza lililofanya maamuzi kuyapa mwelekezo wa umoja makundi ya Kikristo ya kwanza. (Matendo 15:1-31; 16:1-5) Leo mashahidi wapakwa mafuta wa Yehova, yule “mtumwa mwaminifu mwenye akili.” wana Baraza Linaloongoza kwenye makao makuu yao katika Brooklyn, New York, (Mathayo 24:45-47) Baraza hilo linaelekeza kazi kubwa sana ya kutoa ushuhuda ulimwenguni pote juu ya Ufalme ambao sasa inafanywa katika sehemu zote za dunia kwa utimizo wa agizo a kutangaza Ufalme wa Yehova. (Mathayo 24:14) Kazi hiyo haingeweza kamwe kufanywa bila tengenezo fulani. Mtu mmoja akiwa peke yake hangeweza kamwe kuifanya.
19. Ni kazi gani ambayo watu mmoja mmoja wakiwa peke yao hawangeweza kamwe kuifanya ambayo Mashahidi wa Yehova wanafanikiwa kuifanya kwa kufuata uangalifu maagizo ya Mfalme?
19 Hakuna mtu mmoja wala vikundi vya watu vyenye kutapakaa bila kupangwa kitengenezo vingeweza kuhubiri katika lugha zaidi ya 190 na katika nchi 205, viongoze kwa ukawaida mafunzo ya nyumbani ya Biblia zaidi ya milioni mbili na robo, na vibatize kila mwaka wahudumu wapya karibu 190,000 wa habari njema za Ufalme. Hapana, iliwachukua Mashahidi zaidi ya milioni tatu karibu saa za kuhubiri milioni mia sita kufanya kiasi hicho cha kazi katika ule mwaka mmoja wa 1985. Wao waliweza kuifanya kwa sababu tu walikuwa wamepangwa kitengenezo vya kutosha katika makundi 50,000, yote yakiwa chini ya mwelekezo unaoonekana wa Baraza Linaloongoza moja lao. Hata ikiwa hivyo, bado kazi hiyo iliweza kufanywa kwa sababu Baraza Linaloongoza, yale matawi 94, yale makundi 50,000, na wale Mashahidi mmoja mmoja 3,000,000 wote walikuwa wameungana katika kufuata kwa uangalifu maagizo ya Mfalme.
Je! Wewe Unakumbuka?
◻ Yehova alilipangaje kitengenezo taifa la Israeli?
◻ Ni mfano gani mkamilifu ambao Yesu aliacha wa kutimizia kazi ya kutangaza Ufalme wa Yehova?
◻ Ni utumishi gani mwingi unaofanywa na wazee ambao unastahili tuonyeshe staha?
◻ Ni kwa sababu gani vikundi au watu mmoja mmoja wenye kujitegemea hawangeweza kuifanya kazi ya ushuhuda?
[Picha katika ukurasa wa 23]
Ni lazima watu wajipange wenyewe kwa njia itakayoendeleza uhai wao kwa kujifunza maagizo ya Yehova
Muumba anaingiza ndani ya wanyama wote mipango ya kufuatwa ili waendelee kuwa hai