Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 9/1 uku. 3
  • Je! Wewe Unatembea Katika Hatua za Mwokozi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unatembea Katika Hatua za Mwokozi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Yesu Alikuwa Mtu Mzuri Tu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Endelea Kutembea Kama Vile Yesu Kristo Alivyotembea
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • ‘Fuateni Hatua Zake kwa Ukaribu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 9/1 uku. 3

Je! Wewe Unatembea Katika Hatua za Mwokozi?

MOJA ya njia bora zaidi unayoweza kulipa mtu ni kumwiga. Mara nyingi watoto wanaiga wazazi wao. Huenda vijana-matineja wakajifuatisha kwa kielelezo cha watumbuizaji wanaopendwa na watu wengi, nao watu wazima wajifuatishe kwa kielelezo cha viongozi mashuhuri katika mambo ya kikazi na ya kisiasa. Lakini ni wangapi wanaojaribu kuiga yule kiongozi aliyekuwa mkuu zaidi katika historia ya kibinadamu​—Yesu Kristo?

Uchunguzi wa maoni ya watu wengi uliofanywa juzijuzi na tengenezo lilanalohusika na kuchunguza maoni ulifunua hivi: “Wanane kati ya Waamerika 10 walisema wanafanya angalau jitihada fulani ili kufuata mfano wa Yesu.” “Asilimia 12 [tu ndio] walisema wanafanya jitihada iliyo kubwa zaidi. “

Ingawa hivyo, ni jambo gani linalofanya Yesu astahili kufuatwa kuliko watu wengine mashuhuri? Kwanza, kama kilivyosema kichapo The World Book Encylopedia, Yesu Kristo “labda ndiye amekuwa na nguvu za kuvuta wanadamu zaidi ya mtu mwingineye yote aliyepata kuishi.” Lakini tofauti na watu wengine mashuhuri, Kristo hakuongoza majeshi yakatumie nguvu ili “kuongoa watu.” Yeye hakutegemea propaganda zenye gharama kubwa kama wanavyofanya waeneza-evanjeli wanaojulikana sana leo. Wala hakuunga mkono chama cho chote cha kisiasa. Nguvu zake za kuvuta watu zilitokana tu na uthabiti wa ujumbe wake na njia yake ya kuusema.​—Mathayo 7:28, 29; Yohana 7:46.

Yesu alivuta mioyo ya watu ili wafanye mabadiliko ya kutazamisha katika maisha zao, kiroho na kiadili. Ni mtu gani mwingine mashuhuri ambaye amegeuza watu wengi hivyo kwa kuwafaidi? Pia, ni kiongozi gani mwingine wa kibinadamu angeweza kuelezwa kuwa ni “mshikamanifu, asiye na hila, asiyetiwa unajisi, aliyetenganishwa na watenda dhambi”? (Waebrania 7:26, NW) Basi mfano wa Yesu ni mkamilifu​—tofauti na ule wa mwanadamu mwingineye yote ambaye amepata kutembea duniani!

‘Ingawa hivyo, ni kwa njia gani mwanadamu dhaifu asiye mkamilifu anavyoweza kufuata mfano kama huo?’ wengine wanawaza. Mwanahistoria H. G. Wells katika kitabu chake The Outline of History kinasema kwamba tangu mwanzo wanadamu walisita-sita kumfuata Kristo. “Kwa maana kumchukua [Kristo] kwa uzito,” anasema Wells, “kulikuwa ni kuingia katika maisha mageni na yenye kugutusha, kuacha tabia-tabia, kuzuilia maelekeo ya silika na misisimuko ya moyo, kujaribu kuwa na furaha isiowezekana.”. . . Wells anamalizia hivi: “Je! ni ajabu kwamba mpaka leo hii Mgalilaya huyu [Kristo] anatulemea na mambo mengi mno yasiyoweza kufuatwa na mioyo yetu midogo.”

Lakini je! kwa kweli hivyo ndivyo ilivyo? Ni wazi kwamba kufuata Kristo kwa ukamilifu kungekuwa ni jambo lisilowezekana. Hata hivyo mtume Petro alisema kwamba Kristo ‘alituachia mfano ili tufuate sana hatua zake.’ (1 Petro 2:21, NW) Angalia kwamba, alisema kuzifuata “sana” si ‘kwa ukamilifu.’ Basi je! ni mfano gani aliotuachia Yesu? Sisi tunaweza kuuigaje?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki