“Ni Mnyofu na Dini Yake”
Ingawa idara za serikali zimesaidia sana shughuli za ujenzi wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi katika Naijeria, magazeti fulani na viongozi wa kidini wamejaribu kutokezea Mashahidi wa Yehova matata juu ya suala la kutokuwamo. Ijapokuwa hivyo, waandishi wa habari wengine katika magazeti wametoa sifa. Mwandikaji mmoja, ambaye ni mwanasheria, aliuliza kama Mashahidi wa Yehova “wanajionyesha kuwa wenye kupinga uzalendo.” Akitoa jibu lake mwenyewe alisema: “Mashahidi ni raia wanaolipa kodi na kutii sheria. Ye yote . . . aliye Shahidi anayeweza kuwa mnyofu na dini yake kwa kadiri ya kuitii ajapokabiliwa na hatari ya kupoteza mapendeleo fulani atakuwa mnyofu ivyo hivyo katika mambo mengine yaliyo mengi . . . Sababu inayomfanya yeye akatae kuiba pesa za serikali huku wafanya kazi wenzake... wakiimba wimbo wa taifa na bado wakiiba-iba pesa ni kwa sababu Biblia yake inayomwagiza asiimbe wimbo wa taifa ilisema pia haimpasi aibe.”