Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 4/1 uku. 3
  • Mungu Je! Yeye Ni Mtu Halisi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Je! Yeye Ni Mtu Halisi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Mungu Ni Mtu Halisi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Je, Mungu Yuko Kila Mahali?
    Amkeni!—2005
  • Jinsi Tunavyoweza Kupata Kumjua Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Je! Wewe Waweza Kuwa na Uhusiano wa Karibu Sana na Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 4/1 uku. 3

Mungu Je! Yeye Ni Mtu Halisi?

“NI LAZIMA kuwe na Mungu” likatangaza toleo la Agosti 14, 1981, la gazeti Daily Express. Gazeti hilo lilikuwa likiripoti juu ya kilichoonekana kuwa kuongolewa kwa wanasayansi wawili mashuhuri kwenye kuwa na imani katika Mungu. Usadikio wao mpya waliopata ulitokea baada ya wao kugundua tofauti kubwa mno ya hisabati inayopinga wazo la uhai kujitokeza wenyewe. Hata hivyo, waamini hao wapya wawili walimaanisha nini waliposema : “Mungu.” Linaripoti hivi gazeti Daily Express: “Mungu wao wanadokeza NI ulimwengu wote mzima.”

Ikiwa wewe unaamini Mungu, wazo lako juu yake ni nini? Je! pia wewe vilevile unamwona kuwa akili isiyoelezeka, kani ya kuwaziwa tu iliyopo pote, “Kitu fulani” kikubwa? Au wewe unamwona kuwa Mtu mwenye akili, anayeelezeka?

Wengine wanaona ugumu wa kumfikiria Mungu kuwa Mtu. Huenda wakahisi kwamba kufanya hivyo kunamshusha na kumfanya kuwa binadamu tu ​—kama vile katika akili ya kitoto ya mzee mwenye kuvalia vazi refu linalofunika kichwa na mwenye ndevu ndefu nyeupe, anayeketi winguni. Au kama vile Michelangelo alisanii sura ya Mungu kuwa katika mchoro wake unaojulikana sana kwenye dari ya kanisa dogo lililoitwa Sistine​—mwanamume mzee hodari, mwenye nguvu nyingi aeleaye hewani.

Kweli, tunaposikia neno “mtu,” huenda kwa kawaida tunamfikiria mwanadamu. Kwa mfano, kamusi Webster’s Third New International Dictionary, hufafanua “mtu” kuwa “binadamu mmoja mmoja.” Lakini pia inafafanua “mtu” kuwa “mtu mwenyes ifa za utambuzi wenye ufahamu, akili, na ufahamu wa adili.” Kwa hiyo, mtu anaweza kumfikiria kwa usahihi Mungu kuwa Mtu bila ya kumwazia yeye kuwa binadamu.

Lakini huenda wengine wakapinga hivi: ‘Inafanyiza tofauti gani ukimwona Mungu kuwa kani inayowaziwa tu au kuwa Mtu?’ Basi, ikiwa Mungu ni kani tu, “Kitu fulani,” tu je! hilo halimaanishi kwamba vivyo hivyo uhai wa kibinadamu unaendelea tu bila kusudi lo lote? Hivyo binadamu angeshushwa kuwa “kitu” tu, kidude kisicho cha maana sana katika mashine kubwa. Lakini ikiwa Mungu ni Mtu mwenye akili, je! jambo hilo halingeyapa maisha maana kubwa zaidi. Kweli kweli, lingefungua uwezekano wa kuwa na uhusiano pamoja na Mungu​—uhusiano si baina ya “vitu” viwili bali baina ya watu wawili.

Kwa wazi, uhusiano wa mtu kwa mtu pamoja na Mungu ungetamanika sana. Lakini kwanza, sisi tunajuaje kama Mungu ni Mtu au sivyo? Na, ikiwa yeye ni Mtu, sisi tunawezaje kuwa na uhusiano huo? Acheni tuangalie yale yanayosemwa na Biblia juu ya jambo hili.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki