Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 4/1 kur. 4-7
  • Jinsi Tunavyoweza Kupata Kumjua Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Tunavyoweza Kupata Kumjua Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia​—Kitabu cha Mungu
  • Kumjua Mungu kwa Undani
  • Kusoma Biblia Kunatuleta Sisi Karibu na Mungu
  • Manufaa Makubwa Kutokana na Kumjua Mungu
  • Unaweza Kufanya Nini Ili Umjue Mungu Kibinafsi?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Mungu Ni Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Je, Kweli Unaweza ‘Kumkaribia Mungu’?
    Mkaribie Yehova
  • Kuthamini Sifa za Mungu Zisizo na Kifani
    Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 4/1 kur. 4-7

Jinsi Tunavyoweza Kupata Kumjua Mungu

WATU fulani wanaamini kwamba Mungu yuko kila mahali, akiwapo katika nyota na sayari, katika upinde wa mvua, katika bawa la ndege, katika jani la unyasi. Hata hivyo, Biblia inafundisha kwamba Mungu, akiwa Mtu, ana kao halisi. Mfalme Sulemani mwenye hekima alisema katika sala kwa Mungu hivi: “Basi, uyasikie maombi yao na dua yao, huko mbinguni, makao yako.” Na katika kitabu cha Biblia cha Isaya, Mungu mwenyewe ananakiliwa akisema hivi: “Mbingu ni kiti changu cha enzi.”​—1 Wafalme 8:49; Isaya 66:1.

Ingawa Mungu mwenyewe hayuko katika uumbaji wake, sifa za utu wake zinaonyeshwa humo. Akasema mtume Paulo kwenye Warumi 1:20, NW: “Sifa zake zisizoonekana zinaonekana wazi tangu kuumbwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinafahamika kwa vitu vile vilivyofanywa, hata uweza wake wa milele na Uungu.” Kwa jinsi iyo hiyo mtunga zaburi Daudi aliandika hivi: “Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, na anga laitangaza kazi ya mikono yake. Mchana husemezana na mchana, usiku hutolea usiku maarifa.”​—Zaburi 19:1,  2.

Ndiyo, tazama nje katika usiku wenye nyota na kutafakari kwa kitambo hekima na uweza mkubwa uliohitajiwa kuumba na kuendeleza ulimwengu wote mzima wetu! (Linganisha Isaya 40:26.) Kweli kweli, uumbaji ni chanzo kisichokwisha cha habari juu ya utu wa Mungu. Naye mwanadamu hawezi kamwe kufahamu kabisa ushuhuda mkubwa unaotolewa kuhusu sifa na tabia za Mungu. Kitabu cha Ayubu kinatukumbusha sisi hivi: “Tazama, hivi ni viunga tu vya njia zake; na jinsi yalivyo madogo manong’ono tusikiayo katika habari zake!” (Ayubu 26:14) Kuna mithali ya kale ya Kiswedi isemayo: ‘Bwanamkubwa ni mkuu kuliko kazi zake.’ Kwa kulingana, ikiwa uumbaji ni mkubwa, lazima Mungu awe mkubwa zaidi; ikiwa uumbaji unaonyesha hekima, lazima Mungu awe mwenye hekima zaidi; ikiwa uumbaji unaonyesha uweza, lazima Mungu awe mwenye uweza zaidi!

Biblia​—Kitabu cha Mungu

Hivyo uumbaji unatoa habari nyingi juu ya Mungu. Hata hivyo, je! funzo juu ya uumbaji linaweza kukuambia jina la Mungu? Je! litafichua ni nini kusudi la uumbaji au ni kwa sababu gani yeye anaruhusu uovu? Majibu ya maswali hayo yanataka zaidi ya funzo juu ya kazi za kimwili za Mungu. Uzuri ni kwamba, Mungu amehakikisha kwamba habari kama hiyo juu yake imeandikwa katika Biblia.

Humo Mungu haonyeshwi kamwe kuwa akili ya kuwaziwa tu isiyoelezeka au uweza ulio popote. Kwenye Matendo 3:19, NW tunasoma juu ya ‘utu wa Yehova.’ Wakati Mwanaye, Yesu Kristo, alipoinuliwa kutoka kwa wafu, Biblia inasema kwamba yeye aliingia katika mbingu yenyewe aonekane mbele ya ‘utu [kwa halisi, “uso”] wa Mungu.’ (Waebrania 9:24, Kingdom Interlinear) Hakika, Yesu hakumwita Mungu kamwe Kani Kubwa, Akili Isiyo na Mipaka, au jina jinginelo lote lisiloelezeka alipoongea juu yake au aliposali kwake. Tofauti na hilo, mara nyingi yeye alimwita Baba wa kimbingu, jina linalofichua ukaribu wa kadiri sana pamoja na Mungu.​—Mathayo 5:48; 6:14, 26, 32.

Kwa hiyo Mungu si “Kitu Fulani” kisicho na jina bali badala yake yeye ni Mtu aliye na jina. Yasema Zaburi 83:18: “Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, Ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.” Kweli, Biblia pia hutumia majina ya cheo au semi zenye kumweleza Mungu: “Mungu Mwenye Nguvu Zote,” “Mfalme wa umilele,” “mwokozi,” “Mchungaji,” “Mzee wa Siku,” “mwangalizi,” “Mwalimu Mkuu,” “Mfanyi Mkuu,” “Mwamba.” (Ruthu 1:20, NW; 1 Timotheo 1: 17, NW; Isaya 43:11; Zaburi 23:1; Danieli 7: 9, 13, 22, NW; 1 Petro 2:25; Isaya 30:20, NW; 54:5, NW; Kumbukumbu 32:4) Hata hivyo, semi hizo, hufichua nyuso zaidi za utu wa Mungu, kama vile nguvu zake zote, upendo wake wenye kuhangaikia kwa ajili ya watu wake, na hekima yake isiyo na mwisho.

Kwa sababu Mungu ni Mtu, pia yeye ana mambo anayopenda na mambo asiyopenda​—hata hisia. Biblia hutuambia kwamba yeye anapenda watu wake (1 Wafalme 10:9), anafurahia kazi zake (Zaburi 104:31), anachukia ibada ya sanamu (Kumbukumbu 16:22), na anahuzunishwa na uovu. (Mwanzo 6:6) Kwenye 1 Timotheo 1:11, NW yeye hata anaitwa “Mungu mwenye furaha.”

Kumjua Mungu kwa Undani

Kweli, hakuna akili ya kibinadamu iliyo na nafasi ya kutosha kutia ndani ufunuo wote wa utu wa Mungu. “Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani! Maana ni nani aliyeijua nia ya [Yehova]? Au ni nani aliyekuwa mshauri wake?” (Warumi 11:33, 34) Ingawa hivyo, kwa mtu mwenye imani, Mungu anaweza kuwa halisi kama vile mtu mwingineye yote. Biblia hutuambia kwamba “Noa alitembea pamoja na Mungu wa kweli,” kana kwamba Yehova alikuwa kando yake yenyewe. (Mwanzo 6:9, NW) Mungu pia alikuwa halisi sana kwa Musa hivi kwamba ilikuwa kana kwamba yeye alikuwa ‘akimwona yeye asiyeonekana.’ (Waebrania 11:27) Na kwa habari ya Abrahamu ilisemwa kwamba yeye alikuwa “rafiki wa Mungu.”​—Yakobo 2:23.

Bila shaka, Mungu mwenyewe binafsi alijifunua kwa Noa, Abrahamu, na Musa. ‘Basi, ikiwa Mungu angejifunua mwenyewe kwangu katika njia hiyo ya kibinafsi,’ huenda wengine wakasema, ‘yeye angekuwa halisi kwangu pia.’ Ingawa hivyo, kumbuka, Noa, Abrahamu na Musa hawakuwa na Biblia. Wao hawakujua juu ya Yesu Kristo wala juu ya ule unabii wote mwingi aliotimiza. Kama matokeo, mambo yote ambayo Yesu Kristo alifichua juu ya Mungu hayakujulikana kwao. Chini ya hali kama hizo, ilikuwa lazima na ilifaa kwa Mungu kufanya mafunuo yake mwenyewe kama hayo ya moja kwa moja.

Hata hivyo, leo, sisi tuna Biblia na pia utimizo ulio wazi wa karne nyingi wa unabii mbalimbali wa Biblia. Sisi tuna maandishi ya gospeli ya maisha, kazi, na maneno ya Yesu Kristo. Na asema Paulo: “Ni katika yeye [Kristo] kwamba utimilifu wote wa sifa za kimungu hukaa kwa mwili.” (Wakolosai 2: 9, NW) Ndiyo, sisi tu katika hali ya kuweza kumjua Mungu kwa undani ambao haukuwezekana katika siku za wazee wa ukoo. Je! hilo halitoshi sana kulipia uhakika wa kwamba yeye hakujifunua moja kwa moja kwetu sisi?

Kusoma Biblia Kunatuleta Sisi Karibu na Mungu

Tunasoma hivi kwenye Yakobo 4:8: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.” Kwa kusoma Biblia, sisi tunaweza kumkaribia Mungu. Lakini jinsi gani? Jambo moja ni kwamba, kwa kusoma kisehemu cha Biblia kila siku, unajifunza sifa na tabia mpya za utu wake. Usomapo, tua mara kwa mara na kujiuliza: ‘Nimejifunza nini juu ya Mungu katika mstari huo au kisehemu hiki?’ Kwa kuongezea, unaweza kuomba roho ya Mungu itende kama “msaidizi” katika ufahamu wako na katika kumkaribia kwako Mungu.​—Yohana 14:26.

“Mimi nimethamini kupata ufahamu mzuri zaidi juu ya Yehova akiwa mtu,” akaeleza mwanamke mmoja Mkristo aliyesoma Biblia kutoka jalada mpaka jalada. Yeye alikuwa mwanafunzi kwenye Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi, inayowazoeza wamisionari wanaotumwa ulimwenguni pote. Ni njia zipi za kujifunza Biblia zinazotumiwa katika shule hii? Anaeleza hivi mwalimu mmoja wa shule hiyo: “Tulianza mpango wa kujifunza Biblia nzima kama kikundi. Tulichukua kurasa 10 kufikia 15 kila siku, wanafunzi . . . wote wakifanya uchunguzi na kuchangia mazungumzo yetu. Tulipokutana na mstari mgumu, tulifikiria (1) vifungi vinavyouzunguka, (2) hali za wakati wa kuandika, na (3) maana ya maneno makuu katika andiko. Tuliendelea kujiuliza, “Jambo hili linatuambia nini juu ya Yehova na sifa zake?’ Sikuzote tuliona lilituambia jambo fulani juu yake.”

Ijapokuwa huenda wewe usiwe na pendeleo la kujifunza Biblia kwa kikawaida kwenye shule hii, baadhi ya njia hizi za kujifunza zinaweza kuwa na matokeo mazuri kwako na kwa jamaa yako. Kwa mfano, miongoni mwa Mashahidi wa Yehova ni desturi kujifunza sura chache za Biblia kila juma kuhusiana na mikutano yao ya kundi. Kwa sababu gani usiifuate ratiba hii ya kusoma Biblia mkiwa jamaa? Zaidi ya hilo, Sosaiti ya Mnara ya Mlinzi huchapisha misaada ya uchunguzi, kama vile Aid to Bible Understanding na Biblia ya New World Translation yenye marejezo inayoweza kukusaidia ufahamu vifungu vigumu vya Biblia.a Programu ya kawaida ya kusoma Biblia inaweza kukuongezea sana uthamini wako wa utu wa Yehova.

Unaweza pia kuchagua kisehemu cha Biblia ambacho hasa kinakuvutia wewe. Ikiwa, kwa mfano, unachagua kujifunza ile mistari 17 katika Zaburi 86, NW utapata angalau tabia mbalimbali 15 katika utu wa Mungu: Yeye ni mwema, tayari kusamehe, ana wingi wa fadhili za upendo, ana nia ya kujibu sala, hana kifani miongoni mwa miungu, halinganiki akiwa mfanyi kazi katika kuumba, ni mtawala mwenye enzi kuu, ni mfanya mkuu wa mambo yenye kustaajabisha, ni mkombozi kutoka kwa kifo, mwenye rehema, mwenye neema, si mwepesi wa hasira, mwingi katika ukweli, msaidizi, na mfariji. Ni mradi gani bora zaidi unaoweza kuwa nao kuliko kujaribu kujifunza juu ya Muumba wako?

Manufaa Makubwa Kutokana na Kumjua Mungu

Kufikia mradi wetu mkuu wa uzima wa milele ni manufaa moja tu kutokana na kumjua Mungu. (Yohana 17:3) Kuongezea, kuna ile manufaa ya kuwa na mwenzi wa kila siku anayekujali na aliye imara kama mwamba. (Zaburi 18:31) Wakati Mfalme Daudi alipohisi kuwa anazungukwa na adui na kulemewa na matatizo, yeye aligundua ya kwamba Mungu alikuwa ndiye msaidizi halisi wa pekee aliyepatikana. Kwa hiyo yeye alisema: “Umtwike [Yehovaj mzigo wako naye atakutegemeza, hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele.”​—Zaburi 55:22.

Wewe, pia, unaweza kufurahia uhusiano kama huo pamoja na Mungu, ikiwa tu utachukua wakati wa kuja kumjua. Si vigumu sana. Jitahidi kusoma Neno lake. Shirikiana na wale ambao maisha zao huonyesha kwamba wao wanamjua Mungu, watu kama wale waliokuletea jarida hili. Mwite Yehova katika sala. Kwa kuwa Mungu si kani fulani tu isiyo na utu ambayo haitasikia kilio chako. Yeye ni Mungu aliye hai “Msikiaji wa sala.” Na “ukimtafuta, ataonekane nawe.”​—Zaburi 65:2, NW; 1 Nyakati 28:9.

[Maelezo ya Chini]

a Fahirisi ya Watch Tower Publications Index 1930-1985 itakusaidia kupata maelezo na mazungumzo ya vifungu katika misaada hii ya uchunguzi.

[Picha katika ukurasa wa 5]

Mungu mwenyewe binafsi alijifunua kwa Noa, Abrahamu, na Musa

[Picha katika ukurasa wa 7]

Uumbaji ni chanzo kisichokwisha cha habari juu ya utu wa Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki