Kufahamu Yaliyo Katika Habari
Ni Nani Walio Wazushi?
“Katika Biblia tunasoma kwamba Mungu ni Utatu,“ akaandika Profesa Johan Heynes, kiongozi wa kiroho wa Kanisa la Afrika Kusini linaloitwa Dutch Reformed Church, katika chapa ya gazeti Ia Afrika Kusini NaweekVolksblad ya Novemba 15, 1986. Kwa habari ya wale wanaotoa sababu kwamba Mungu hawezi kuwa watatu na bado mmoja, anaendelea kusema profesa huyo, “Kanisa la Kikristo lilisema kwamba watu hawa walikuwa wakihubiri fundisho Ia kidini Ia uwongo, na kwa hiyo pia kanisa Iinawalaani kuwa wazushi.“
Lakini ni wapi neno “Utatu“ linapopatikana katika Biblia? Profesa Heynes hakusema. Hili si jambo la kushangaza kwa sababu, kama The New Encyclopaedia Britannica inavyoeleza, “wala neno Utatu wala fundisho is kidini Iililo wazi halipatikani katika Agano Jipya, wala Yesu na wafuasi wake hawakukusudia kupinganisha Shema [ungamo la Kiyahudi la imani] katika Agano la Kale: ‵Sikiliza, Ee Israeli: Bwana, Mungu wetu, ndiye mmojaʼ (Kumbukumbu 6:4).“ lkiwa halikufundishwa na Yesu na mitume wake wala halisemwi waziwazi katika Biblia, fundisho la kidini la Utatu lilipataje kukubaliwa na watu walio wengi? Ingawa kichapo Britannica kinadai kwamba asili ya fundisho hilo Ia kidini imo katika “Agano Jipya,“ kinakubali kwamba “fundisho hilo la kidini lilisitawi polepole kwa muda wa karne kadha na kupitia mabishano mengi“ na kwamba kufikia mwisho wa karne ya nne “fundisho Ia Utatu Iikachukua kwa uhakika ile namna ambayo limedumisha tangu hapo.“
Ikiwa wale wanaokataa kuamini kwamba Mungu ni watatu katika mmoja ni wazushi, basi namna gani juu ya Yesu Kristo mwenyewe? Yeye alirudia maneno yaliyo juu ya Kumbukumbu 6:4: “Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja.“ (Marko 12: 29, Union Version) Yesu alisema pia: “Baba ni mkuu kuliko mimi.“ (Yohana 14:28) Kwa hiyo ni nani walio wazushi? Wale wanaoshikamana na yale aliyofundisha Yesu, au wale wanaoshikilia fundisho Ia kidini lililositawishwa karne nyingi baada ya kifo chake?—Linganisha 1 Wakorintho 4:6 na 2 Yohana 9.
Mji Ulio “Ngome“
“Sydney leo ni mji ulio chini ya mazingiwa,“ ikaanza makala ya mhariri katika The SunHerald, gazeti la Sydney, Australia. “Viunga vyao ambako watu wanaishi vimekuwa ngome iliyotiwa makomeo, vikazingiwa maradufu, na kulindwa kwa vifaa vya elektroni. Magarimoshi yao ya kusafiri usiku yameharibiwa, yakatiwa makovu kwa maneno machafu-machafu na ni matupu vya kuogopesha. Barabara zao baada ya giza kuingia zinazidi kukosa usalama.“
Ingawa yaliyo juu yangeweza kuwa mfano wenye kutaabisha wa miji mingi mikubwa kuzunguka uiimwengu, yanatoa maonyo yenye kuhangaisha sana kwa Waaustralia. Hata hivyo, wanafunzi wa Biblia hawashangai kuona ukosefu wa kutokutii sheria ukienea. Kwa sababu gani? Kwa sababu wanakumbuka maneno ya kiunabil ya Yesu juu ya hall za siku zetu. Yesu alisema kwamba “kwa sababu ya kuongezeka kwa kutokutii sheria upendo wa wengi zaidi utapoa.“ (Mathayo 24:12, NW) Na ijapokuwa makala ya mhariri katika The SunHerald inaombolezea mweneo wa woga unaoathiri ule ambao umepata kuitwa mji wenye bahati zaidi wa Nchi Yenye Bahati, “bahati“ haitakomesha uovu. Yehova peke yake, kupitia serikali yake ya kimbingu, ndiye atafanya hivyo. Zaburi 5:4 inatuhakikishia kwamba Yehova si “Mungu apendezwaye na ubaye; mtu mwovu hatakaa kwako.“
Matokeo Yasiyotazamiwa Yaliyo Kinyume Yenye Kuleta Kifo
Biblia inawaamuru Wakristo ʼwajiepushe na damu.ʼ (Matendo 15:29) Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba amri hii ya Kimaandiko inahusu kula damu na kutiwa damu mishipani vilevile. UKIMWI, ugonjwa wenye kuua unaoshambulia mfumo wa mwili wa kujikinga na magonjwa, unaweza kupitishwa kwa kutiwa damu mishipani. Katika kisa chenye kuhuzunisha ambacho ni kinyume cha matokeo yaliyotazamiwa, kitoto kilichozaliwa kikiwa na ugonjwa unaotokea mara chache sana wenye kuua unaoshambulia mfumo wa mwili wa kujikinga na magonjwa unaoitwa reticular dysgenesis kilipewa mwatiko wa mafuta ya mfupani kikiwa na umri wa miezi sita. Njia iliyotumiwa ilihusu kutiwa damu mishipani. Mwatiko huo ulionekana kuwa unafaulu mpaka wakati madaktari walipogundua kwamba damu iliyotumiwa kutiwa mishipani ilikipa kitoto hicho ugonjwa mwingine wenye kuleta kifo. “Akiwa na [umri wa miaka] 2 1/2 mgonjwa huyo anafanya vizuri isipokuwa jambo moja,“ laripoti jarida Physicianʼs Weekly. “Mtoto huyo alipewa visahani [vya damu] baada ya kutiwa damu mishipani kabla ya kuchunguza [damu] kwa ajili ya (virasi ya UKIMWI) kufanywa kuwa jambo la lazima na sasa kivulana huyo ana UKIMWI.“