Mzee-Mzee Mwenye Uthamini
Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 79 wa kutoka Japani alisukumwa na moyo kuandika barua inayofuata baada ya kusoma lile toleo la Juni 1, 1987 la Mnara wa Mlinzi juu ya kile kichwa “Nani Atawatunza Watu Wazee-Wazee?”
“Kwa Akina Ndugu Ambao Mimi Ninaheshimu Sana,
Ninapojifunza lile toleo la Juni 1, 1987, kuhusu watu wazee-wazee, mimi ninapata habari zile kuwa za kuielewa sana hali na za fadhili. Wakati mimi nilipofika fungu 11, nililazimika kuchukua kitambaa-mkononi changu kwa sababu nilizidi tu kulia na kulia na singeweza kuacha. Hayo yalikuwa machozi ya shukrani zenye kina kirefu. Lo, ni upendo na fadhili gani! Mimi ningeweza tu kufanya lile ambalo Zaburi 150 inasema—kusifu Yah!
Mimi natoa kwa unyenyekevu shukrani zangu za kina kilicho kirefu zaidi kwenu ninyi akina ndugu kwa kuchapisha makala hizo zilizofanywa kwa fikira nyingi juu ya kuonyesha fadhili kwa watu wazee-wazee, hata kwenye yale mambo madogo-madogo sana. Bila shaka, mimi ni mwenye kujawa na shukrani kwa zile makala nzuri ambazo ninyi mnachapisha kila mwezi, na hakuna maneno ya kueleza uthamini wangu vya kutosha. Kwa mara nyingine tena, mimi nawapigia ninyi asante.
Jambo la kufurahisha ni kwamba, kila mmoja katika kundi letu ni mwenye kupenda na kufadhili sana. Wao wananipeleka mimi kwenye eneo la kuhubiri na kunirudisha nikiwa katika magari yao, na kwa sababu ya utumishi wao wa fadhili, mimi ni painia-msaidizi.
Mimi nimejawa na shukrani kwa kina kirefu kwa ajili ya ki-i-la siku ambayo mimi naweza kuishi katika tengenezo zuri ajabu lenye himaya namna hii.
Katika ulimwengu leo, ambamo watu wazee wanazidi kuwa wengi sana lakini wasiokaribishwa sana, hakuna jambo lenye thamani zaidi ya zile baraka ambazo sisi tunapokea kutoka kwa Mungu mwenye kupenda jinsi hiyo. Ni sala yangu kwamba mimi niweze kusaidia watu wengi iwezekanavyo kujifunza ukweli ili wao waweze kushangilia pamoja na sisi.
Sifa iende kwa Yehova na asante iende kwenu ninyi, ndugu zangu wapendwa. Tafadhali mniwie radhi kwa mwandiko wangu mbaya sana, ambao mimi naonea aibu. Yehova na awabariki ninyi, na kuwapa ninyi afya njema.
Mwanamke mzee asiye na ubingwa wa jambo lo lote,
[imetiwa sahihi] Nogami
Maneno na misisimuko ya moyoni kama hiyo inathibitisha ule uhakika wa kwamba upendo wa kweli wa Kikristo haujui mpaka au hadi ya umri. Mashahidi wa Yehova, vijana na wazee, wanaonyesha uanafunzi wao kwa kuishi kulingana na taarifa ya Yesu: “Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.”—Yohana 13:35.