Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 1/15 uku. 6
  • Mzee-Mzee Mwenye Uthamini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mzee-Mzee Mwenye Uthamini
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Familia ya Kikristo Huwasaidia Wazee-Wazee
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • “Toeni Shukrani Kuhusu Kila Jambo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Ni Daraka la Kikristo Kuwatunza Walio Wazee
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • ‘Kuendelea Kuangalia’ Masilahi za Watu Wazee-Wazee
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 1/15 uku. 6

Mzee-Mzee Mwenye Uthamini

Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 79 wa kutoka Japani alisukumwa na moyo kuandika barua inayofuata baada ya kusoma lile toleo la Juni 1, 1987 la Mnara wa Mlinzi juu ya kile kichwa “Nani Atawatunza Watu Wazee-Wazee?”

“Kwa Akina Ndugu Ambao Mimi Ninaheshimu Sana,

Ninapojifunza lile toleo la Juni 1, 1987, kuhusu watu wazee-wazee, mimi ninapata habari zile kuwa za kuielewa sana hali na za fadhili. Wakati mimi nilipofika fungu 11, nililazimika kuchukua kitambaa-mkononi changu kwa sababu nilizidi tu kulia na kulia na singeweza kuacha. Hayo yalikuwa machozi ya shukrani zenye kina kirefu. Lo, ni upendo na fadhili gani! Mimi ningeweza tu kufanya lile ambalo Zaburi 150 inasema—kusifu Yah!

Mimi natoa kwa unyenyekevu shukrani zangu za kina kilicho kirefu zaidi kwenu ninyi akina ndugu kwa kuchapisha makala hizo zilizofanywa kwa fikira nyingi juu ya kuonyesha fadhili kwa watu wazee-wazee, hata kwenye yale mambo madogo-madogo sana. Bila shaka, mimi ni mwenye kujawa na shukrani kwa zile makala nzuri ambazo ninyi mnachapisha kila mwezi, na hakuna maneno ya kueleza uthamini wangu vya kutosha. Kwa mara nyingine tena, mimi nawapigia ninyi asante.

Jambo la kufurahisha ni kwamba, kila mmoja katika kundi letu ni mwenye kupenda na kufadhili sana. Wao wananipeleka mimi kwenye eneo la kuhubiri na kunirudisha nikiwa katika magari yao, na kwa sababu ya utumishi wao wa fadhili, mimi ni painia-msaidizi.

Mimi nimejawa na shukrani kwa kina kirefu kwa ajili ya ki-i-la siku ambayo mimi naweza kuishi katika tengenezo zuri ajabu lenye himaya namna hii.

Katika ulimwengu leo, ambamo watu wazee wanazidi kuwa wengi sana lakini wasiokaribishwa sana, hakuna jambo lenye thamani zaidi ya zile baraka ambazo sisi tunapokea kutoka kwa Mungu mwenye kupenda jinsi hiyo. Ni sala yangu kwamba mimi niweze kusaidia watu wengi iwezekanavyo kujifunza ukweli ili wao waweze kushangilia pamoja na sisi.

Sifa iende kwa Yehova na asante iende kwenu ninyi, ndugu zangu wapendwa. Tafadhali mniwie radhi kwa mwandiko wangu mbaya sana, ambao mimi naonea aibu. Yehova na awabariki ninyi, na kuwapa ninyi afya njema.

Mwanamke mzee asiye na ubingwa wa jambo lo lote,

[imetiwa sahihi] Nogami

Maneno na misisimuko ya moyoni kama hiyo inathibitisha ule uhakika wa kwamba upendo wa kweli wa Kikristo haujui mpaka au hadi ya umri. Mashahidi wa Yehova, vijana na wazee, wanaonyesha uanafunzi wao kwa kuishi kulingana na taarifa ya Yesu: “Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.”—Yohana 13:35.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki