Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 3/1 kur. 18-22
  • Uzazi Miongoni mwa Watu wa Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uzazi Miongoni mwa Watu wa Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uzazi Katika Israeli
  • Nyakati Zenye Magumu kwa Watoto Katika Israeli
  • Uzazi Miongoni mwa Wakristo wa Mapema
  • ‘Dhiki Katika Mnofu’
  • “Wakati Unaobaki Umepunguzwa”
  • Uzazi Leo
  • Kielelezo cha Kale
  • “Nyakati za Hatari”
  • Uzazi Unaojali Madaraka ya Kuzaa Katika Huu Wakati wa Mwisho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Shika Imani na Dhamiri Njema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Huu Ndio Wakati Tunaopaswa Kuwa Wenye Kulinda Zaidi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 3/1 kur. 18-22

Uzazi Miongoni mwa Watu wa Mungu

“Yehova na . . . akuongeze wewe mara elfu.”—KUMBUKUMBU 1:11, NW.

1. Biblia inasema jinsi gani kuhusu uzazi?

“TAZAMA! Wana ni urithi kutoka kwa Yehova; tunda la tumbo ni thawabu. Kama mishale katika mkono wa mwanamume hodari, ndivyo walivyo wana wa ujana. Mwenye furaha ni mwanamume kakawana ambaye amejaza podo lake kwa hao.” Hivyo ndivyo tunavyosoma kwenye Zaburi 127:3-5, NW. Ndiyo, uzazi ni pendeleo zuri ajabu ambalo Muumba Yehova aliwapa wenzi wa kwanza waliooana wa kibinadamu na wazao wao.—Mwanzo 1:28.

Uzazi Katika Israeli

2. Kwa sababu gani jamaa kubwa zilitamanika miongoni mwa wazao wa Abrahamu, Isaka na Yakobo?

2 Jamaa kubwa zilifikiriwa kuwa zenye kutamanika sana miongoni mwa wazao wa Abrahamu kupitia Isaka na Yakobo. Hata watoto waliozaliwa na wake wa pili na masuria walifikiriwa kuwa halali. Ndivyo ilivyokuwa kwa habari ya wana fulani wa Yakobo, ambao walikuja kuwa mababa wa msingi wa yale makabila kumi na mawili ya Israeli. (Mwanzo 30:3-12; 49:16-21; linganisha 2 Nyakati 11:21.) Ingawa mpango wa kwanza wa Mungu kwa ndoa ulikuwa kuwa na mke mmoja, yeye alivumilia ndoa yenye wake wengi na masuria miongoni mwa wazao wa Abrahamu, na hiyo iliongeza idadi ya watu kwa haraka sana. Waisraeli walipaswa kuwa “jamii ya watu iliyo na hesabu kubwa sana kama chembe-chembe za mavumbi ya dunia.” (2 Nyakati 1:9; Mwanzo 13:14-16, NW) Ndani ya taifa hilo, ungekuja ule “uzao” ulioahidiwa ambao kupitia kwao “mataifa yote ya dunia” yangeweza kujibariki yenyewe.—Mwanzo 22:17, 18; 28:14; Kumbukumbu 1:10, 11.

3. Hali ilikuwa nini katika Israeli wakati wa utawala wa Sulemani?

3 Kwa uwazi, katika Israeli uzazi ulitazamwa kuwa ishara ya baraka ya Yehova. (Zaburi 128:3, 4) Hata hivyo, inapasa iangaliwe kwamba yale maneno ya kufungua makala hii, yaliyodondolewa kutoka Zaburi 127, yaliandikwa na Mfalme Sulemani, na sehemu kubwa ya utawala wa mfalme huyo ilikuwa wakati wenye upendeleo sana kwa Israeli. Biblia hutaarifu hivi juu ya kipindi hicho: “Yuda na Israeli walikuwa wengi kama mchanga wa pwani kwa wingi, wakila, na kunywa, na kufurahi. Yuda na Israeli wakakaa salama, kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, tokea Dani [katika kaskazini] mpaka Beer-sheba [katika kusini], siku zote za Sulemani.”—1 Wafalme 4:20, 25.

Nyakati Zenye Magumu kwa Watoto Katika Israeli

4, 5. (a) Kwa sababu gani si sikuzote uzazi ulikuwa kisababishi cha shangwe katika Israeli? (b) Ni tamasha gani za kuhuzunisha sana zilizotukia katika angalau pindi mbili katika Yerusalemu?

4 Lakini kulikuwako vipindi vingine katika historia ya Israeli wakati uzazi haukuleta shangwe hata kidogo. Wakati wa uharibifu wa kwanza wa Yerusalemu, nabii Yeremia aliandika hivi: “Macho yangu yamefikia mwisho kwa kutoa machozi matupu . . . kwa sababu ya kule kuzimia kwa mtoto na mnyonyaji katika njia kuu za mji. Je! wanawake wapaswe kula tunda lao wenyewe, watoto ambao walizaliwa wakiwa na umbo kamili? ” “Ile mikono yenyewe ya wanawake wenye huruma imechemsha watoto wao wenyewe.”—Maombolezo 2:11, 20; 4:10, NW.

5 Inaonekana kama tamasha zinazofanana na hizo za kuhuzunisha sana zilitokea karibu karne saba baadaye. Mwanahistoria Myahudi Yosefo hueleza kwamba wakati wa mazingiwa ya Yerusalemu katika 70 W.K., watoto walinyakua vyakula kutoka vinywani mwa baba zao, na akina mama walichukua vyakula kutoka vinywani mwa vitoto vyao vichanga. Yeye anasimulia jinsi mwanamke mmoja Myahudi alivyoua mtoto wake mwenye kunyonya, akauchoma mwili wake kwa moto, na kula sehemu fulani ya mwili huo. Kuzaa watoto katika ulimwengu wa Kiyahudi katika miaka iliyoongoza kwenye mfikilizo wa hukumu za Yehova dhidi ya Yerusalemu katika 607 K.W.K. na 70 W.K. hakungeweza kamwe kusemwa kuwa uzazi unaojali madaraka ya kuzaa.

Uzazi Miongoni mwa Wakristo wa Mapema

6, 7. (a) Ni mazoea gani ambayo Yesu aliondolea mbali kwa ajili ya Wakristo? (b) Ni kwa kutumia njia gani Israeli wa kiroho wanapaswa kukua, na ni nini linalothibitisha jambo hilo?

6 Uzazi ulionwa jinsi gani miongoni mwa Wakristo wa mapema? Kwanza, inapasa iangaliwe kwamba Yesu aliondolea mbali ndoa yenye wake wengi na masuria miongoni mwa wanafunzi wake. Yeye alirudia kusimamisha kwa uthabiti kiwango asilia cha Yehova, yaani ndoa ya mwanamume mmoja kwa mwanamke mmoja. (Mathayo 19:4-9) Ijapokuwa taifa la Israeli wa kimwili lilikuja kuwa na watu wengi sana kupitia uzazi, taifa la Israeli wa kiroho lingekua kupitia kazi ya kufanya wanafunzi.—Mathayo 28:19, 20; Matendo 1:8.

7 Kama mpanuko wa Ukristo ulipasa kutokea kupitia uzazi hasa, Yesu hangaliwatia moyo wanafunzi wake “kutafutia nafasi” useja “kwa ajili ya ufalme wa mbingu.” (Mathayo 19:10-12, NW) Mtume Paulo hangaliandika hivi: “Yeye pia anayeutoa ubikira wake kuutia katika ndoa afanya vema, lakini yeye asiyeutoa kuutia katika ndoa atafanya vizuri zaidi.”—1 Wakorintho 7:38, NW.

8. Ni nini linaloonyesha kwamba wengi wa Wakristo wa kwanza walikuwa wamefunga ndoa na walikuwa na watoto?

8 Hata hivyo, ingawa wao walitia moyo kuepuka ndoa ili kutegemeza masilahi za Ufalme, wala Yesu wala Paulo hakulazimisha jambo hilo. Wote wawili walitangulia kuona kwamba Wakristo fulani wangefunga ndoa. Kwa asili, watu fulani kati ya hao wangekuwa na watoto kama ilivyo kawaida. Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yana vifungu kadha ambavyo viliwapa Wakristo wa mapema mashauri ya moja kwa moja juu ya malezi ya watoto. (Waefeso 6:1-4; Wakolosai 3:20, 21) Ikiwa wazee au watumishi wa huduma walikuwa wameoa, wao wangekuwa wazazi wenye kielelezo chema.—1 Timotheo 3:4, 12.

9. Kulingana na mtume Paulo, ni jinsi gani wanawake fulani Wakristo wangepata himaya kwa kuzaa, lakini wao wangehitaji nini zaidi?

9 Mtume Paulo hata alitaarifu kwamba kuwa na watoto kungeweza kuwa himaya kwa wanawake fulani Wakristo. Kwa habari ya msaada kwa wajane wenye uhitaji, yeye aliandika hivi: “Wakatalie wajane wenye umri mdogo . . . Wao pia wanajifunza kuwa wenye kukaa bila kujishughulisha, wakitanga-tanga kuziendea nyumba; ndiyo, si wenye kukaa tu bila kujishughulisha, bali pia ni wenye kupiga porojo na wajidukizi katika mambo ya watu wengine, wakisema juu ya mambo wasiyopaswa. Basi mimi natamani kwamba wajane wenye umri mdogo waolewe, wazae watoto, wawe na usimamizi wa watu wa nyumbani, kutompa mpinzani kisababishi cha kutukana. Kwa kweli, tayari wengine wamegeuziwa kando ili kufuata Shetani.” Wanawake kama hao “wangeendelezwa kuwa salama kupitia uzazi, mradi wanaendelea katika imani na utakaso pamoja na utimamu wa akili.”—1 Timotheo 5: 11-15; 2:15, NW.

‘Dhiki Katika Mnofu’

10. Ni shauri gani tofauti kwa wajane-wake ambalo Paulo alitoa katika barua yake ya kwanza kwa Wakorintho?

10 Hata hivyo, inastahili kuangaliwa kwamba, katika barua yake ya kwanza kwa Wakorintho, mtume yule yule Paulo alidokeza utatuzi tofauti kwa wajane-wake. Yeye alieleza waziwazi sababu ya shauri lake juu ya kufunga ndoa, akitaarifu kwamba alilitoa “kwa njia ya hisani.” Yeye aliandika hivi: “Sasa mimi nasema kwa watu wasiofunga ndoa na wajane, ni vema kwao kwamba wabaki kama mimi nilivyo. Lakini ikiwa hawana kujiweza, acheni hao wafunge ndoa, kwa maana ni vizuri zaidi kufunga ndoa kuliko kuwa mwenye kuwaka harara. Lakini yeye [mjane-mke] ni mwenye furaha zaidi akibaki kama yeye alivyo, kulingana na maoni yangu. Mimi kwa uhakika nafikiri mimi pia nina roho ya Mungu.”—1 Wakorintho 7:6, 8, 9, 40, NW.

11. (a) Wale ambao wanafunga ndoa wangepatwa na nini, na ni jinsi gani rejezo la pambizoni juu ya 1 Wakorintho 7:28 linatoa nuru juu ya jambo hilo? (b) Paulo alimaanisha nini aliposema, “Mimi ninawaepusha na jambo hilo”?

11 Paulo alieleza hivi: “Ikiwa mtu bikira angefunga ndoa, mtu kama huyo hangetenda dhambi. Hata hivyo, wale wanaofanya hivyo watakuwa na dhiki katika mnofu wao. Lakini mimi ninawaepusha na jambo hilo.” (1 Wakorintho 7:28, NW) Kwa habari ya hiyo “dhiki katika mnofu,” rejezo la pambizoni la Biblia ya New World Translation linaturejeza kwenye Mwanzo 3:16, ambapo tunasoma hivi: “Kwa mwanamke yeye [Yehova] alisema: ‘Mimi nitaongeza sana lile umivu la mimba yako; kwa machungu ya uzazi wewe utatokeza watoto, na mtamanio wako wewe utakuwa kwa mume wako, na yeye atakutawala wewe.’ “Kuongezea magumu ya ndoa ambaye yangeweza kutokea, ile “dhiki katika mnofu ambayo ingewapata wale ambao wangefunga ndoa ingetia ndani bila shaka matatizo yanayohusiana na uzazi. Ingawa Paulo hakukataza wala ndoa wala uzazi, kwa uwazi yeye alihig akiwa amefungwa na wajibu wa kuonya Wa kristo wenzake kwamba mambo hayo yange weza kuleta matatizo na vikengeua-fikira ambavyo vingeweza kuwazuia katika utumi shi wao kwa Yehova.

“Wakati Unaobaki Umepunguzwa”

12. Ni shauri gani ambalo mtume Paulo aliwapa Wakristo waliofunga ndoa, na kwa sababu gani?

12 Katika karne ya kwanza W.K., Wakristo hawakuwa huru kuongoza maisha zao kama watu wa kilimwengu. Hali yao ingeathiri hata maisha yao ya ndoa. Paulo aliandika hivi “Zaidi ya hayo, mimi nasema hivi, akina ndu gu, wakati unaobaki umepunguzwa. Tango sasa na kuendelea acheni wale walio na wake wawe kama kwamba hawakuwa nao, . . . na wale wanaotumia ulimwengu kama wale wasioutumia kwa ukamili; kwa maana tamasha ya ulimwengu huu inabadilika. Kweli kweli, mimi nataka ninyi mwe huru na hangaiko. . . . Lakini mimi ninasema hilo kwa faida yenu ya kibinafsi, si ili kwamba nirushe kitanzi juu yenu, bali kuwahamisha mwende kwenye lile linalofaa na lile linalomaanisha kutumikia Bwana daima bila kikengeua-fikira.”—1 Wakorintho 7:29-35, NW.

13. Ni katika maana gani ‘wakati uliobaki ulipunguzwa’ kwa Wakristo wa karne ya kwanza?

13 Mwanachuo wa Biblia, Frederic Godet aliandika hivi: “Ijapokuwa wasioitikadi wanauchukua ulimwengu kuwa ni hakika kwamba utadumu kwa wakati usio dhahiri, sikuzote Mkristo anauweka mbele ya macho yake ule uhakika mkubwa unaotazamiwa, ile Parousia [Kuwapo].” Kristo alikuwa amewapa wanafunzi wake ishara ya “kuwapo” kwake, na alikuwa amewaonya hivi: “Kwa hiyo, endeleeni kuwa katika lindo kwa sababu ninyi hamjui ni katika siku gani Bwana wenu ninyi anakuja.” (Mathayo 24:3, 42, NW) Wakati uliobaki ulikuwa “umepunguzwa” katika maana ya kwamba Wakristo hao wa karne ya kwanza walilazimika kuishi daima wakitazamia kuja kwa Kristo. Tena, wao hawakujua ni kadiri gani ya wakati iliyowabakia wao mmoja mmoja kabla ya “wakati na tukio lisilotazamiwa” kukomesha uhai wao, kumaliza uwezekano wote wa ‘kufanya mwito wao uwe hakika.’—Mhubiri 9:11; 2 Petro 1:10, NW.

14. (a) Mathayo 24:19 inaeleweka jinsi gani? (b) Onyo la Yesu lilipataje uharaka zaidi wakati ule mwaka wa 66 W.K. ulipokaribia?

14 Kwa Wakristo katika Yudea na Yerusalemu, ule uhitaji wa ‘kuendelea kuwa katika lindo’ ulikuwa wa lazima hasa. Wakati Yesu alipotoa onyo la uharibifu wa pili wa Yerusalemu, yeye alitaarifu hivi: “Ole kwa wanawake wenye mimba na wale wanaonyonyesha kitoto katika siku hizo! ” (Mathayo 24:19, NW) Ni kweli kwamba, Yesu hakuambia Wakristo wa karne ya kwanza kwamba walipaswa kuepuka kuwa na watoto. Yeye alitaja tu kwa unabii jambo lililo uhakika wa maisha, akionyesha kwamba wakati kiashirio cha uharibifu wa Yerusalemu kingetokea, lingekuwa jambo gumu zaidi kwa wanawake wenye mimba au wale wenye watoto wadogo kukimbia kwa haraka. (Luka 19:41-44; 21:20-23) Hatahivyo, wasiwasi ulipoendelea kuongezeka miongoni Uzazi Leo

Uzazi Leo

15, 16. (a) Ni jinsi gani‘wakati unaobaki umepunguzwa’ kwa Wakristo wanaoishi leo? (b) Kwa hiyo ni maswali gani ambayo inawapasa Wakristo wajiulize wenyewe?

15 Inawapasa Wakristo waone ndoa na uzazi jinsi gani leo, katika huu “wakati wa mwisho”? (Danieli 12:4) Sasa ni kweli zaidi ya wakati mwingine wowote kwamba “tamasha ya ulimwengu huu inabadilika,” au, kama vile tafsiri nyingine inavyosema, “mpangilio wa kisasa wa mambo unapitilia mbali kwa haraka.”—1 Wakorintho 7:31, Phillips.

16 Sasa, kama isivyopata kamwe kuwa hapo mbele, “wakati unaobaki umepunguzwa.” Ndiyo, ni wakati mchache tu unaobaki kwa watu wa Yehova kuimaliza kazi ambayo yeye amewapa wafanye, yaani: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.” (Mathayo 24:14, NW) Lazima kazi hiyo itimizwe kabla ya mwisho kuja. Kwa hiyo, inafaa Wakristo wajiulize wenyewe ushiriki wao katika kazi hiyo muhimu utaathiriwa jinsi gani na kufunga ndoa au kuwa na watoto, ikiwa wamefunga ndoa.

Kielelezo cha Kale

17. (a) Ni kazi gani ambayo Noa na wana watatu wake walilazimika kutimiza kabla ya Gharika, na inaonekana ni kama ilichukua muda gani? (b) Inawezekana ni kwa sababu gani mbalimbali wana wa Noa na wake zao walijiepusha kuwa na watoto wakati wa kile kipindi kilichotangulia Gharika?

17 Yesu alifananisha wakati wa “kuwapo kwa Mwana wa binadamu” na “siku za Noa.” (Mathayo 24:37, NW) Noa na wana watatu wake walikuwa na kazi fulani ya wazi ya kutimiza kabla ya Gharika. Hiyo ilihusisha ndani kujenga safina kubwa sana na kuhubiri. (Mwanzo 6:13-16; 2 Petro 2:5) Wakati Yehova alipotoa maagizo juu ya ujenzi wa safina, inaonekana kwamba tayari wana wa Noa walikuwa wamefunga ndoa. (Mwanzo 6:18) Sisi hatujui vizuri kabisa ilichukua muda gani kujenga safina, lakini inaelekea kwamba ilichukua miongo kadha. Jambo la kupendeza ni kwamba, kipindi chote hicho kilichotangulia Gharika, wana wa Noa na wake zao hawakuwa na watoto. Mtume Petro anataarifu waziwazi kwamba ‘nafsi nane walichukuliwa salama kupita yale maji,’ yaani, wenzi wanne waliofunga ndoa, lakini bila ya watoto kuwako. (1 Petro 3:20, NW) Inawezekana kwamba wana hao walibaki bila watoto kwa sababu mbili. Kwanza, wao walikuwa na kazi waliyowekewa rasmi na Mungu ambayo ilitaka kuangaliwa kwa fikira zisizogawanywa, kwa sababu ya uharibifu uliokuwa unakaribia wa gharika ya maji mengi. Pili, bila shaka wao walihisi kutotaka kuzaa watoto katika ulimwengu ambamo “ubaya wa mwanadamu ulikuwa tepetepe katika dunia na kila mwinamio wa fikira za moyo wake ulikuwa mbaya tu wakati wote,” ulimwengu ‘wenye kujaa jeuri.’ —Mwanzo 6:5, 13, NW.

18. Ingawa hauweki kanuni ya kufuatwa, ni jinsi gani mwendo uliochukuliwa na wana wa Noa na wake zao huandaa jambo la kufikiria?

18 Hiyo si kusema kwamba mwendo wa kitendo uliochukuliwa na wana wa Noa na wake zao kabla ya ile Gharika ulimaanishwa uweke kanuni ya kuongoza wenzi waliofunga ndoa wanaoishi leo. Hata hivyo, kwa kuwa Yesu alilinganisha siku ya Noa na kipindi ambamo sisi tunaishi sasa, kielelezo chao kinaweza kuandaa jambo la kufikiria.

“Nyakati za Hatari”

19. (a) Ni jinsi gani nyakati zetu zinalingana na siku ya Noa? (b) Paulo alitabiri nini kwa “siku za mwisho,” na unabii wake unahusu uzazi jinsi gani?

19 Kama Noa na jamaa yake, sisi pia tunaishi katika “ulimwengu wa wasiomcha Mungu.” (2 Petro 2:5) Kama wao, sisi tumo katika “siku za mwisho” za mfumo mwovu wa mambo ambao uko karibu kuharibiwa. Mtume Paulo alitoa unabii kwamba “siku za mwisho” za mfumo wa Shetani zingeleta “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” Akionyesha kwamba kulea watoto kungekuwa moja la mambo yaliyo magumu kushughulikia, yeye aliongeza kwamba watoto wangekuwa “wasiotii wazazi.” Yeye alitaarifu kwamba watu kwa ujumla, kutia ndani watoto na vijana wenye kubalehe, wangekuwa “wasio na shukrani, wasio washikamanifu, wasio na shauku ya asili.” (2 Timotheo 3:1-3, NW) Ingawa hapa Paulo alikuwa akitoa unabii wa hali ambazo zingekuwa miongoni mwa watu wa kilimwengu, kwa uwazi mielekeo hiyo yenye kuenea pote ingefanya kulea watoto kuendelee kuwa jambo gumu zaidi kwa Wakristo, kama vile wengi wamejionea.

20. Ni mambo gani ambayo yatafikiriwa katika makala inayofuata?

20 Yote yaliyotangulia yanaonyesha kwamba inahitajiwa kabisa kuwa na maoni yaliyosawazika kuhusu uzazi. Ingawa huo unaweza kuleta shangwe za namna nyingi, unaweza pia kuleta maumivu mengi ya moyo. Huo una faida na hasara fulani-fulani. Baadhi yazo zitafikiriwa katika makala inayofuata.

Mambo ya Kupitia

◻ Kwa sababu gani jamaa kubwa zilikuwa za kutamanika katika Israeli?

◻ Ni jambo gani linaloonyesha kwamba kulikuwako nyakati ambapo uzazi ulileta maumivu ya moyoni kwa Wayahudi?

◻ Ni jinsi gani Israeli wa kiroho walipaswa kukua katika hesabu?

◻ Ni jinsi gani ‘wakati uliobaki ulipunguzwa’ kwa Wakristo wa mapema?

◻ Inawezekana kuna sababu gani zilizofanya wana wa Noa na wake zao wabaki bila watoto kabla ya Gharika, na namna gani juu ya hali hiyo leo?

[Picha katika ukurasa wa 21]

Kimbio la haraka kutoka Yerusalemu lingekuwa gumu zaidi kwa wale wenye watoto wachanga

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki