Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 1/15 uku. 30
  • Shika Imani na Dhamiri Njema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Shika Imani na Dhamiri Njema
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mawaidha ya Kushika Imani
  • Shauri Juu ya Ibada
  • Ujitoaji Kimungu Pamoja na Kutosheka
  • Kitabu cha Biblia Namba 54—1 Timotheo
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Timotheo Anapata Mashauri kwa Mwanamume Mzee
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Timotheo—“Mtoto Halisi Katika Imani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 1/15 uku. 30

Shika Imani na Dhamiri Njema

Mambo Makuu Kutokana na Timotheo wa Kwanza

KARIBU mwaka 56 W.K., mtume Paulo alionya wazee wa kundi la Efeso kwamba “mbwa-mwitu wakali” wangeinuka kati yao na ‘kusema mapotovu wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao.’ (Matendo 20:29, 30) Katika muda wa miaka michache, fundisho la uasi-imani likawa zito sana hivi kwamba Paulo akahimiza Timotheo afanye vita ya kiroho ndani ya kundi ili kuhifadhi utakato walo na kusaidia waamini wenzi kubaki katika imani. Hiyo ilikuwa sababu kubwa kwa nini Paulo alimwandikia Timotheo barua yake ya kwanza akiwa Makedonia karibu 61-64 W.K.

Timotheo aliagizwa juu ya wajibu mbalimbali wa mzee, mahali pa wanawake walipogawiwa na Mungu, sifa za wazee na watumishi wa huduma, na mambo mengine. Maagizo hayo ni yenye manufaa leo pia.

Mawaidha ya Kushika Imani

Paulo alifungua kwa shauri la kushika imani na dhamiri njema. (1:1-20) Alimtia Timotheo abaki katika Efeso na ‘kuwakataza wengine wasifundishe elimu nyingine.’ Paulo alikuwa mwenye shukrani kwa hudumu aliyogawiwa, akikiri kwamba alikuwa ametenda kwa kukosa maarifa na ukosefu wa imani aliponyanyasa wafuasi wa Yesu. Mtume alimwagiza Timotheo aendelee kupiga vita vya kiroho, akiwa ‘mwenye imani na dhamiri njema’ na kutokuwa kama wale ambao ‘waliangamia kwa habari ya Imani.’

Shauri Juu ya Ibada

Halafu, Paulo alitoa shauri akiwa “mwalimu wa Mataifa katika imani na kweli.” (2:1-15) Sala zilipasa kutolewa kuhusu wale walio katika cheo cha juu ili Wakristo waweze kuishi kiamani. Ni mapenzi ya Mungu kwamba namna zote za wanadamu waokolewe, na fundisho moja muhimu ni kwamba Kristo “alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi [unaolingana, NW] kwa ajili ya wote.” Paulo alionyesha kwamba mwanamke apaswa kujipamba kwa kiasi na ni lazima asijizoeze mamlaka juu ya mwanamume.

Ni lazima kundi lipangwe vizuri kitengenezo. (3:1-16) Paulo alipangilia sifa za waangalizi na watumishi wa huduma. Kutokana na mambo ambayo mtume aliandika, Timotheo angejua jinsi ya kujiendesha mwenyewe katika kundi, “nguzo na msingi wa kweli.”

Paulo alimpa Timotheo shauri la kibinafsi ili kumsaidia alinde dhidi ya fundisho bandia. (4:1-16) Katika nyakati za baadaye watu fulani wangeanguka mbali kutoka kwenye imani. Lakini kwa kutoa uangalifu wa daima kwake mwenyewe na kwa fundisho lake, Timotheo ‘angejiokoa nafsi yake na wale wamsikiao pia.’

Pia Timotheo alipokea shauri juu ya kushughulika na watu mmoja mmoja, vijana na wazee. (5:1-25) Kwa kielelezo, maandalizi yafaayo yalipasa kufanywa kwa ajili ya wajane wenye umri mkubwa wenye sifa nzuri ya Kikristo. Badala ya kupiga porojo, wajane wachanga wapaswa kuolewa na kuzaa watoto. Wanaume wazee wenye kusimamia kwa njia nzuri walipasa kuhesabiwa kustahili heshima maradufu.

Ujitoaji Kimungu Pamoja na Kutosheka

Shauri juu ya ujitoaji kimungu lilimalizia barua ya Paulo. (6:1-21) “Utauwa [ujitoaji kimungu, NW] pamoja na kuridhika” ni njia ya kuwa na pato kubwa, lakini kuazimia kuwa tajiri huongoza kwenye uharibifu na uangamivu. Paulo alimhimiza Timotheo apige lile pigano zuri la imani na ‘kupata [kushika imara, NW] uzima ulio kweli kweli.’ Ili kuushika uzima halisi huo, matajiri walipaswa ‘wasiutumainie utajiri, bali wamtumaini Mungu atupaye vitu vyote.’

[Picha katika ukurasa wa 30]

Kaokolewa Kupitia Kuzaa Watoto: Paulo hakuwa akizungumza wokovu wa kupata uzima wa milele bali sehemu ifaayo ya mwanamke mhofu Mungu alipoandika hivi: “Ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu katika imani na upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi.” (1 Timotheo 2:11-15) Kupitia kuzaa watoto, kutunza watoto wake, na kusimamia nyumba, mwanamke ‘angeokolewa’ kutokuwa mpiga porojo asiye na shughuli na mwingiliaji mambo ya watu wengine. (1 Timotheo 5:11-15) Utendaji wake wa kinyumbani ungekamilisha utumishi wake kwa Yehova. Bila shaka, Wakristo wote wapaswa kulinda mwenendo wao na kutumia wakati wao kwa hekima.—Waefeso 5:15, 16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki