Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 12/15 uku. 30
  • Je! Wewe Unakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Simama Imara Dhidi ya Hila za Shetani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Kuiponyosha Codex Sinaiticus
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Kusaidia Wengine Waabudu Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 12/15 uku. 30

Je! Wewe Unakumbuka?

Je! wewe umefikiria kwa uangalifu matoleo ya hivi majuzi ya Mnara wa Mlinzi? Ikiwa ndivyo, labda utaweza kukumbuka mambo yanayofuata:

◻ Ni nini chanzo cha furaha ya kweli?

Yesu alisema: “Wenye furaha ni wale wanaosikia neno la Mungu na kulishika!” (Luka 11:28, NW) Hivyo Yesu alionyesha kwamba furaha ya kweli inapatikana katika kuwa mtumishi mwaminifu wa Mungu na kufanya mapenzi yake.​—8/15, ukurasa 8.

◻ Ni nini njia moja ambayo katika hiyo sisi tunaweza kukinza vitendo vya Shetani vya werevu na vya kiufundi?

Ili kukinza Shetani, ni lazima tujichunguze wenyewe. Je! sisi tuna udhaifu fulani ambao Shetani angeweza kutumia au anatumia kwa faida yake sasa hivi? Mathalani: Je! sisi tuna tatizo la kujiona kuwa watu wa maana sana? Je! ni lazima sikuzote sisi tuwe ndio namba moja? Ikiwa tunajijua wenyewe, basi tunaweza kurekebisha matatizo hayo, mradi sisi ni wanyenyekevu. Kwa njia hiyo, hatutajiacha wenyewe tukiwa wazi kuingiliwa na Shetani,—9/1, kurasa 15, 16.

◻ Ni nini alama ya ufananishi ambayo yule mtu ‘aliyevaa bafta’ anaitia juu ya wale wanaokuwa “kondoo wengine” za Kristo? (Ezekieli 9:2-4; Yohana 10:16)

“Alama” hiyo ni ithibati ya kwamba hao walio mfano wa kondoo ni watu mmoja mmoja waliojiweka wakfu na kubatizwa, walio na utu kama wa Kristo.​—9/15, ukurasa 4.

◻ Mtume Petro alimaanisha nini aliposema kwamba inatupasa sisi ‘tupendane kwa juhudi nyingi sana’? (1 Petro 1:22, NW)

“Kwa juhudi nyingi sana” humaanisha ‘kwa kunyooka kirefurefu.’ Ili upendo wa jinsi hiyo uonyeshwe miongoni mwa Wakristo, kunatakiwa kujitahidi na kupanuka kwa mioyo yetu ili ihusishe ndani watu ambao kwa kawaida hatungevutiwa nao.​—10/1, ukurasa 12.

◻ Ni nini hekalu linalorejezewa kwenye Ufunuo 11:1, na lilitokea wakati gani?

◻ Ni hekalu kuu la kiroho​—patakatifu pa patakatifu ambapo ni kao la Yehova mbinguni. Lilitokea katika 29 W.K. wakati Yesu alipopakwa mafuta na kuanza kutumikia akiwa kuhani mkuu. (Waebrania 3:1; 10:5)—10/15, ukurasa 12.

◻ Codex Sinaiticus ni nini, nayo ni ya maana kadiri gani?

Codex Sinaiticus ina Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yote na Maandiko ya Kiebrania. Ina umri wa angalau miaka 1,600, na ni kiunzi muhimu katika orodha yetu ya hati za Biblia.​—10/15, kurasa 30, 31.

◻ Ni nini huleta furaha kubwa zaidi katika ndoa?

Ni lazima kila mwenzi ahakikishe kwamba Mungu yumo katika ndoa yao. Kwa njia hiyo, mahitaji ya kiroho yatatoshelezwa, na kifungo cha ndoa kitaimarishwa. (Mhubiri 4:12; Mathayo 5:3)—11/1, ukurasa 16.

◻ Ni nini “amani ya Mungu” ambayo mtume Paulo anainena kwenye Wafilipi 4:7?

Amani hiyo ni utulivu mwingi na ushwari unaotolewa na Mungu, hata katikati ya mastakimu zenye kujaribu sana. Inaletwa na uhusiano wa karibu pamoja na Yehova na usadiki wa mtu kwamba anafanya yaliyo ya kufurahisha machoni pake.​—11/1, ukurasa 30.

◻ Ni kuanzia hatua gani ya wakati ambapo mmoja anakuwa mwenye kukubaliwa na Yehova?

Kuanzia mtu anapojiweka wakfu na kubatizwa na kuendelea tangu hapo, inawezekana mwanadamu asiyekamilika kuwa ‘mtu wa nia njema,’ au mtu anayekubaliwa na Mungu. (Luka 2:14)—11/15, ukurasa 11.

◻ Wazazi wanaweza kufanya nini wasaidie mtoto wao mwenye kukosa hata ikiwa ameondolewa ustahili wa kuwa mhubiri asiyebatizwa au ametengwa na ushirika?

Sawa na vile ambavyo wazazi wataendelea kuandaa chakula, nguo, na makao, ndivyo wanavyohitajiwa kumwagiza na kumtia nidhamu kupatana na Neno la Mungu. Wao wanaweza kujifunza wakiwa pamoja na yeye peke yake au kumwacha ashiriki katika mpango wa funzo la jamaa.​—11/15, ukurasa 20.

Ni jinsi gani pokeo la Kiyahudi lilivyotangua amri ya Mungu kwenye Kutoka 20:12 kwamba watoto wanapaswa kuheshimu wazazi wao?

Mtu angeweza kufanya ahadi rasmi kwamba mali yake ichangiwe hekalu baadaye kwa kuitangaza kuwa “korbani,” ambayo ilimaanisha, “zawadi iliyowekwa wakfu kwa Mungu.” (Marko 7:11, NW) Korbani hiyo ingeweza bado kutumiwa na mtu huyo kwa faida yake mwenyewe, lakini yeye angeweza kuwanyima wazazi wake wasiitumie.​—12/1, kurasa 4, 5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki