Muono-Ndani Juu ya Habari
Kuwa na Biblia Hakutoshi
Uchunguzi wa hivi majuzi ulipata kwamba kati ya watu ambao wana Biblia zao, nusu yao walisema hawakuzisoma kamwe. Hii ilikuwa ni kutia na wengi ambao hujitambulisha kuwa Wakristo waliozaliwa tena. Karibu asilimia 30 ya Wakristo hao wa kujidai walioombwa maoni yao hawakujua kwamba Yesu alizaliwa katika Bethlehemu. Kulingana na The Detroit News, “asilimia kumi na nane walijibu Yerusalemu, hali asilimia 8 walisema ni Nazareti.” George Barna, mkuu wa kikundi hicho cha uchunguzi, alisema hivi: “Ikiwa wao hawana habari kuhusu mambo ya msingi kama haya, waweza kutarajiwa wazungumze yaliyomo katika Maandiko pamoja na mtu asiye mwamini au waishi kwa njia yenye kupatana na kanuni za kibiblia?”
Mtume Paulo aliona hali kama hiyo miongoni mwa watu fulani waliokuwa na “bidii ya kumtafuta Mungu; lakini bidii hiyo haikujengwa juu ya ujuzi wa kweli [maarifa sahihi, NW].” Pia alirejezea watu fulani waliokuwa na “namna ya ibada ya kujitakia wenyewe, unyenyekevu wa uwongo” na akatabiri kwamba “siku za mwisho” zingetiwa alama na kuwapo kwa wale “wenye namna ya ujitoaji kimungu lakini wakithibitika kuwa bandia kwa nguvu zao.” (Warumi 10:2; Wakolosai 2:23, HNWW; 2 Timotheo 3:1-5) Hata hivyo, Wakristo wa kweli hustahi sana Neno la Mungu. Wao hutambua kwamba kuwa na Biblia hakutoshi. Bali, wao hufuata kwa moyo wote shauri lalo la ‘kufanyiza nia ya kutamani sana maziwa yasiyochanganywa kitu ambayo ni ya lile neno.’—1 Petro 2:2, NW.
Wana Uzoelevu wa Kutotii Sheria
Moja la mambo yaliyoorodheshwa na Yesu Kristo kuwa sehemu ya “ile ishara” ya siku za mwisho za mfumo huu wa mambo ni “kuongezeka kwa kutokutii sheria.” (Mathayo 24:3, 12, NW) Utumizi wa dawa za kulevya umekuwa na uvutano wa kutazamisha kuhusu ongezeko kubwa la kutotii sheria leo. Kwa kielelezo, ile karatasi-habari ya Australia The Sydney Morning Herald yaripoti kwamba saba kati ya visa kumi vya uhalifu wenye kufanywa katika New South Wales huwa vyahusiana na dawa za kulevya, na karibu asilimia 85 ya visa vya unyang’anyi wa kutumia silaha katika mkoa huo hufanywa na watumizi wa dawa heroini. Na tatizo la utumizi mbaya wa dawa za kulevya linaongezeka.
U.S.News & World Report yasema kwamba “hakuna mahali popote katika Ulaya pasipopatwa na tauni hiyo.” Katika Urusi, hesabu ya wenye kutumia vibaya dawa za kulevya yakadiriwa kuwa mamilioni. Katika jaribio kali la kuzuia wimbi la utumizi mbaya wa dawa za kulevya, serikali ya Urusi imeanzisha katika nchi 25 mashauriano pamoja na mashirika yenye kutekeleza mambo ya dawa za kulevya. Hata hivyo, matumaini ya kwamba serikali zitafikia miradi hiyo yaonekana hayafai kwa kukabiliwa na ripoti za kwamba mapato yenye kutokana na dawa za kulevya yanatumiwa kuwatia ufisadi mapolisi, waongoza-mashtaka wa kiserikali, na hata mahakimu. Alisema hivi ofisa mmoja wa serikali aliyevurugika fikira: “Hakuna kikosi chochote cha polisi ulimwenguni ambacho zaidi ya kufanikiwa chembe ndogo tu kimeweza kukomesha ugavi [wa dawa za kulevyaj uliomo kwa wingi katika mabarabara.” Aliongezea hivi: “Hiyo inashusha moyo kwa sababu hakuna matatuzi yoyote kamwe yanayotokezwa wazi.”
Maneno hayo yakumbusha juu ya unabii wa Yesu kuhusu siku za mwisho. Yeye alitabiri kwamba katika wakati huu ‘watu wangezirai kwa hofu, wasijue njia ya kutokea.’—Luka 21:25, 26, NW.
Yesu na Siasa
Kichwa kikuu cha habari katika The Star ya Johannesburg, karatasi-habari ya Afrika Kusini, kilisomwa hivi: “Kanisa Katoliki Lafunua Mpango wa Kufanya Uchungaji Afrika Kusini.” Mpango huo ni wa “kuleta ufalme wa Mungu” katika Afrika Kusini kupitia “jitihada ya kanisa kukomesha kabisa ubaguzi wa rangi.” Ili lifikie lengo hili, Jude Pieterse, mwandishi-mkuu wa Mkutano wa Maaskofu Wakatoliki wa Afrika Kusini, alisema kwamba kanisa linatafuta kuungwa mkono na makanisa mengine na pia “pande zote za jamii ya Afrika Kusini.” Hata hivyo, Wakatoliki fulani wahisi kwamba mpango huo ni “hila ya kugeuza Wakatoliki wawe wanaharakati wa kisiasa,” aeleza askofu wa Johannesburg, Reginald Orsmond. Ingawa Pieterse alikiri kwamba mpango huu una mimaanisho ya kisiasa, Orsmond alisema kwamba hilo si “jambo jipya” kamwe bali lilianza “tangu enzi zile za Yesu mwenyewe.”
Kwa kweli, Yesu Kristo asingaliwaelekeza kamwe wanafunzi wake wawe wanaharakati wa kisiasa. Alipoulizwa na Pontio Pilato, Yesu alijibu kwa imara hivi: “UfaIme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.” (Yohana 18:36, NW) Pia, Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni tatu wana shangwe ya upatano kati ya watu wa rangi mbalimbali miongoni mwao kwa sababu wao huishi kulingana na amri mpya ya Yesu, kwamba wapendane; sawa na vile Yesu alivyowapenda’—si katika Afrika Kusini tu, bali ulimwenguni pote! —Yohana 13:34.