Je! Wakumbuka?
Je! wewe umepata matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi yakiwa yenye thamani inayoweza kutumika kwako? Basi kwa nini usitahini kumbukumbu lako kwa yafuatayo?
◻ Ni lazima tufanye nini ikiwa tutapata upatano na amani kwa watu wa jamii za rangi zote walioonwa katika njozi kwenye Isaya 2:4?
Kwanza, lazima tukiri kwamba Muumba wetu, Yehova, ana haki ya kutuagiza “njia zake.” Na pili, lazima tuwe na tamaa ya moyo ya kujipatanisha na sheria zake kwa kusema: “Tutakwenda katika mapito yake.” (Isaya 2:2, 3)—12/15, kurasa 5, 6.
◻ Kwa nini Mashahidi wa Yehova hawavunjwi moyo na kulegezwa moyo na chuki na upinzani wa ulimwenguni pote?
Yesu alitabiri kwamba upinzani na chuki hiyo ingekuwa alama ya kutambulisha waabudu wa kweli. (Yohana 15:20, 21; 2 Timotheo 3:12) Kwa hiyo wapiga mbiu ya habari njema wanahakikishiwa kwamba wana kibali cha kimungu. Kwa kuongezea, Mashahidi wa Yehova wanajua kwamba wanaungwa mkono na Yehova, Mungu Aliye Juu Zaidi.—1/1, ukurasa 12.
◻ Ni nini baadhi ya matakwa ya msingi ambayo lazima tutimize ikiwa sala zetu zitajibiwa?
Lazima tuamini kwa moyo mweupe kwamba Mungu yuko. Lazima tuwe ‘tukimtafuta kwa bidii,’ tukiwa na uhakika kwamba yeye atathawabisha wale wanaofanya hivyo. (Waebrania 11:6, NW) Pia, lazima tumkaribie Yehova kupitia Yesu Kristo na yeye pekee. (Yohana 14:6, 14)—1/15, kurasa 4, 6.
◻ “Ujitoaji kimungu” ni nini? (1 Timotheo 3:16, NW)
Ujitoaji kimungu ni staha yenye kicho, ibada, na utumishi kwa Mungu, pamoja na ushikamanifu kwa enzi yake kuu ya ulimwengu wote mzima.—1/15, ukurasa 11.
◻ “Mtu wa kuasi [sheria]” anayesemwa na mtume Paulo kwenye 2 Wathesalonike 2:3 ni nani?
Paulo hasemi juu ya mtu mmoja, kwa kuwa yeye anataarifu kwamba huyu “mtu” alikuwa wazi katika siku ya Paulo naye angeendelea kuwapo mpaka Yehova amharibu mwishoni mwa mfumo huu. Kwa sababu hiyo, “mtu wa kuasi [sheria]” ni usemi wa ufananisho. Uthibitisho huonyesha kwamba yeye ni baraza la makasisi wenye kiburi, wenye kutaka makuu wa Jumuiya ya Wakristo, ambao kwa muda wa karne nyingi wamejiweka kuwa sheria kwao wenyewe.—2/1, ukurasa 11.
◻ Pupa inaweza kumalizwaje?
Pupa miongoni mwa binadamu yaweza kumalizwa kupitia tu elimu inayofaa na mazoezi, pamoja na miongozo, au kanuni za mwenendo zenye kufuatiliwa sana. Elimu kama hiyo lazima itoke kwenye chanzo ambacho chenyewe hakina pupa. Mungu wa mbingu tu ndiye anaweza kutoa aina hii ya elimu, nayo inapatikana katika kitabu cha mafundisho chake kilichoandikwa, Biblia Takatifu.—2/15, ukurasa 5.
◻ Ikiwa funzo la kibinafsi litatokeza usitawisho wa ujitoaji kimungu, funzo hilo lapasa litie ndani nini?
Lengo la funzo la kibinafsi haliwezi kuwa kupitia kurasa kadhaa za habari na hivyo kujaza akili na habari. Badala ya hivyo, wakati wa kusoma kisehemu cha Neno la Mungu, lazima wakati utumiwe kufikiri juu ya habari, kuamua inalofundisha juu ya sifa na njia za Yehova ili mwanafunzi awe zaidi kama Yehova katika pande hizi.—3/1, ukurasa 13.
◻ Kwa nini funzo la Biblia la kibinafsi lapasa kutia ndani usomaji wa kawaida wa habari za Yesu katika Gospeli?
Kielelezo cha Yesu hutusaidia kusitawisha ujitoaji kimungu. Yesu alijua Baba yake vizuri zaidi kupita mtu mwingine yeyote, hivyo yeye angeweza kuiga njia na sifa za Yehova kwa ukaribu. Kwa sababu hiyo, yeye alituwekea kielelezo kikamilifu cha ujitoaji kimungu. (Yohana 1:18; 14:9; Warumi 13:14)—3/1, ukurasa 18.
◻ Katika kielezi cha Yesu cha talanta, ni nini kilichomaanishwa na kufanyiza kazi talanta hizo? (Mathayo 25:19-23)
Kufanyiza kazi talanta hizo kulimaanisha kutenda kiaminifu kama mabalozi wa Mungu, kufanya wanafunzi, na kutolea watu wa nyumba ya Mungu kweli za kiroho. (Mathayo 24:45; 28:19-20; 2 Wakorintho 5:20, NW)—3/15, ukurasa 13.
◻ Ni katika pande gani tatu Biblia haina kifani ikilinganishwa na vyanzo vingine vyote vya shauri?
Kwanza, shauri layo linanufaisha sikuzote. (Zaburi 93:5) Pili, Biblia imestahimili kutahiniwa na wakati. (Isaya 40:8; 1 Petro 1:25) Tatu, mweneo mkubwa wa shauri la Biblia haulinganiki. Hata tuwe tunaelekeana na tatizo au uamuzi gani, mna hekima ndani ya Biblia ambayo yaweza kutusaidia.—4/1, ukurasa 13.
◻ Ni zipi zile aina mbili za uthibitisho ambazo huonyesha kwamba Biblia ni Neno la Mungu, si la mwanadamu?
Ile hekima ya Biblia na uwezo wayo usiolinganika wa kubadili watu. (Mithali 2:1, 5, 6; Waebrania 4:12)—4/1, ukurasa 21.