Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 3/1 kur. 10-14
  • Fuatieni Ujitoaji Kimungu Mkiwa Wakristo Waliobatizwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fuatieni Ujitoaji Kimungu Mkiwa Wakristo Waliobatizwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Maana ya Ujitoaji Kimungu
  • Jitihada ya Kujikakamua Yahitajiwa
  • Kusitawisha Ujitoaji Kimungu
  • Tieni Ujitoaji Kimungu Katika Uvumilivu Wenu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Ongezeni Kwenye Uvumilivu Wenu Ujitoaji-kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Fuata Kielelezo cha Yesu cha Ujitoaji Kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Ujitoaji-Kimungu
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 3/1 kur. 10-14

Fuatieni Ujitoaji Kimungu Mkiwa Wakristo Waliobatizwa

“Hata hivyo, wewe, O mtu wa Mungu, . . . fuatia uadilifu, ujitoaji kimungu.”—1 TIMOTHEO 6:11, NW.

1. Wewe ungelijibuje swali, Ni nini siku iliyo ya maana zaidi katika maisha yako? Kwa nini wajibu hivyo?

NI SIKU gani iliyo ya maana zaidi maishani mwako? Ikiwa wewe ni Shahidi wa Yehova aliyebatizwa, bila shaka utajibu, ‘Ala, ni siku ile niliyobatizwa!’ Kwa uhakika, ubatizo ni hatua ya maana sana katika maisha yako. Ni kifananisho cha nje kwamba wewe umefanya wakfu kamili usiolimbika kwa Yehova ufanye penzi lake. Ubatizo wako hutia alama tarehe ya kuagizwa kwako rasmi kuwa mhudumu (minista) wa Mungu Aliye Juu Zaidi, Yehova.

2. (a) Kungeweza kutolewa kielezi gani kwamba ubatizo siyo hatua ya mwisho ambayo wewe wachukua katika mwendo wako wa Kikristo? (b) Ni hatua gani za utangulizi zilizo za maana ambazo ulichukua kabla ya kubatizwa?

2 Ingawa hivyo, je! ubatizo ndiyo hatua ya mwisho ambayo wewe huchukua katika mwendo wako wa Kikristo? Sivyo hata kidogo! Kwa kutoa kielezi: Katika mabara mengi sherehe ya arusi huwa ndiyo alama ya mwisho wa kipindi cha kupanga na kujitayarisha (na kwa kawaida mwisho wa uchumba). Wakati ule uje, huwa ndiyo alama ya mwanzo wa maisha pamoja mkiwa watu wawili waliofunga ndoa. Vivyo hivyo, ubatizo wako ndio upeo wa kipindi cha matayarisho ambapo wewe ulichukua hatua kadhaa za utangulizi. Ulipata maarifa kuhusu Mungu na Kristo. (Yohana 17:3) Ulianza kujizoeza imani katika Yehova kuwa ndiye Mungu wa kweli, katika Kristo kuwa Mwokozi wako, na katika Biblia kuwa ndilo Neno la Mungu. (Matendo 4:12; 1 Wathesalonike 2:13; Waebrania 11:6) Ulionyesha imani hiyo kwa kutubu kuhusu mwendo wa vitendo vyako vya zamani na kugeukia mwendo wa uadilifu. (Matendo 3:19) Ndipo ulipofanya uamuzi wa kujiweka wakfu kwa Yehova ili ufanye penzi lake. (Mathayo 16:24) Mwishowe, ukabatizwa.—Mathayo 28:19, 20.

3. (a) Twaweza kuonyeshaje kwamba ubatizo wetu hutia alama mwanzo wa maisha ya utumishi wa kujiweka wakfu kwa Mungu? (b) Ni maswali gani yatokea, na kwa nini twapaswa kupendezwa sana na majibu?

3 Ingawa hivyo, ubatizo wako sio mwisho bali ndio mwanzo wa maisha ya utumishi mtakatifu ulio wakfu kwa Mungu. Kama vile mwanachuo mmoja wa Biblia alivyoarifu, ni lazima maisha ya Kikristo yasiwe ‘mpindano wa mwanzoni tu ukifuatwa na utuli uliosedeka.’ Basi, wewe waweza kuonyeshaje kwamba katika kisa chako, ubatizo hauwakilishi ‘mpindano wa mwanzoni tu’? Ni kwa kufuatia mwendo wa ujitoaji kimungu muda wa maisha yote. Huu ujitoaji kimungu ni nini? Kwa nini yahitajiwa kabisa kuufuatia? Waweza kuusitawishaje kikamili zaidi katika maisha yako? Twapaswa kupendezwa sana na majibu, kwa maana ni lazima sisi tuwe watu wenye kutambulishwa kwa “matendo ya ujitoaji kimungu” ikiwa tutaokoka siku inayokaribia ya hukumu ya Yehova.—2 Petro 3:11, 12, NW.

Maana ya Ujitoaji Kimungu

4. Paulo alimshauri Timotheo afanye nini, na ilikuwaje kuhusu Timotheo wakati huu?

4 Wakati fulani kati ya 61 na 64 W.K., mtume Paulo alimwandikia Timotheo mwanafunzi Mkristo barua yake ya kwanza yenye uvuvio. Baada ya kuaridhia hatari ambazo zaweza kuletwa na kupenda pesa, Paulo aliandika hivi: “Hata hivyo, wewe, O mtu wa Mungu, kimbia vitu hivi. Lakini fuatia . . . ujitoaji kimungu.” (1 Timotheo 6:9-11, NW) Kwa kupendeza, wakati huu labda Timotheo alikuwa katika miaka yake ya mapema ya 30 na kitu. Alikuwa tayari amesafiri mapana na marefu pamoja na mtume Paulo na akawa amepewa mamlaka ya kuweka rasmi waangalizi na watumishi wa huduma katika makundi. (Matendo 16:3; 1 Timotheo 5:22) Hata hivyo, Paulo aliusia mwanamume huyu mkomavu wa Kikristo, aliyejiweka wakfu na kubatizwa, afuatie ujitoaji kimungu.

5. Ni nini maana ya usemi “ujitoaji kimungu”?

5 Paulo alimaanisha nini kwa usemi “ujitoaji kimungu”? Neno la awali la Kigiriki (eu·seʹbei·a) laweza kutafsiriwa kihalisi kuwa “kustahi kwema sana.” Kuhusu linachomaanisha, twasoma hivi: “Neno eusebeia hutukia pindi kwa pindi katika maana yenye kudokeza ujitoaji wa kibinafsi kuhusiana na dini katika maandishi ya kipindi hicho . . . lakini maana ya ujumla zaidi ya neno hilo katika Kigiriki kile cha watu wengi wa kipindi cha Waroma ilikuwa ‘uaminifu-mshikamanifu.’ . . . Kwa Wakristo neno eusebeia ni ujitoaji kwa Mungu ulio wa aina ya juu kabisa.” (Christian Words, cha Nigel Turner) Kwa hiyo kama vile utumiwavyo katika Maandiko, usemi “ujitoaji kimungu” hurejezea staha nyingi au ujitoaji wenye uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova Mungu binafsi.

6. Mkristo hutoaje ushuhuda juu ya ujitoaji kimungu wake?

6 Ingawa hivyo, huu ujitoaji kimungu si hisia ya kiibada tu. Sawa na vile “imani pasipo matendo imekufa,” vivyo, pia, ni lazima ujitoaji kimungu upate wonyesho katika maisha ya mtu. (Yakobo 2:26) Katika New Testament Words, William Barclay aliandika hivi: “Si kwamba [neno eu·seʹbei·a na maneno yenye kuhusiana nalo] yaonyesha hisia hiyo ya kicho na staha nyingi, bali pia yadokeza maana ya ibada inayojuzu kicho hicho, na maisha ya utii amilifu unaojuzu staha nyingi hiyo.” Neno eu·seʹbei·a laendelea kufasiliwa kuwa ni “umaizi wa kimatendo hasa wa Mungu katika kila upande wa maisha.” (The Second Epistle General of Peter and the General Epistle of Jude, cha Michael Green) Basi, ni lazima Mkristo aonyeshe kithibitisho cha kwamba ana ufungamano wa kibinafsi na Yehova kwa njia ambayo yeye huishi maisha yake.—1 Timotheo 2:2; 2 Petro 3:11.

Jitihada ya Kujikakamua Yahitajiwa

7. Paulo alimaanisha nini alipohimiza Timotheo, ingawa alikuwa amebatizwa, ‘afuatie’ ujitoaji kimungu?

7 Ingawa hivyo, ni nini kinachohusishwa katika kukuza na kudhihirisha ujitoaji kimungu? Je! ni shauri la kubatizwa tu? Kumbuka kwamba ingawa Timotheo alikuwa amebatizwa, yeye alihimizwa “kuufuatia [kwa uhalisi, ‘wewe uwe ukifuatia’]” huo.a (1 Timotheo 6:11, Kingdom Interlinear) Ni wazi kwamba Paulo hakuwa akidokeza kwamba mwanafunzi Timotheo hakuwa na ujitoaji kimungu. Bali, alikuwa akimkazia uhitaji wa kuendelea kuufuatia bila kufanya mchezo na juhudi. (Linganisha Wafilipi 3:14.) Kwa uwazi, huu ungekuwa ufuatiaji wa maisha yote. Timotheo, kama Wakristo wote waliobatizwa, angeweza kuendelea kufanya maendeleo katika kudhihirisha ujitoaji kimungu.

8. Petro alionyeshaje kwamba jitihada ya kujikakamua yahitajiwa kwa Mkristo aliyejiweka wakfu na kubatizwa ili afuatie ujitoaji kimungu?

8 Jitihada ya kujikakamua yahitajiwa ili Mkristo aliyejiweka wakfu na kubatizwa afuatie ujitoaji kimungu. Akiandikia Wakristo waliobatizwa waliokuwa na tazamio la ‘kuwa washiriki katika asili ya kimungu,’ mtume Petro alisema hivi: “Ndiyo, kwa sababu hii hii, kwa kuchanga kwenu jitihada yote isiyo ya mchezo kwa kuitikia, gaweni kwenye imani yenu nguvu ya wema, kwenye nguvu yenu ya wema maarifa, kwenye maarifa yenu kujidhibiti, kwenye kujidhibiti kwenu uvumilivu, kwenye uvumilivu wenu ujitoaji kimungu.” (2 Petro 1:4-6, NW) Kwa uwazi, kadiri fulani ya imani yahitajiwa ndiyo tujitoe kwa ajili ya ubatizo. Hata hivyo, baada ya ubatizo hatuwezi kuambaa-ambaa tu, huku tukitosheka na Ukristo kidogo tu wa kuonyesha. Bali, tufanyapo maendeleo katika maisha ya Kikristo, twahitaji kuendelea kukuza sifa nyingine nzuri, kutia na ujitoaji kimungu, ambazo zaweza kugawiwa imani yetu. Petro asema kwamba hilo huhitaji jitihada isiyo ya mchezo upande wetu.

9. (a) Neno la Kigiriki kwa “gaweni” latoaje kielezi cha kadiri ya jitihada ambayo yahitajiwa ili kusitawisha ujitoaji kimungu? (b) Petro anatuhimiza tufanye nini?

9 Neno la Kigiriki ambalo Petro atumia kwa “gaweni” (e·pi·kho·re·geʹo) lina asili ya kupendeza na hutoa kielezi cha kadiri ya jitihada inayohitajiwa kabisa. Latokana na nomino (jina, kho·re·gosʹ) ambayo kwa uhalisi yamaanisha “kiongozi wa korasi.” Ilirejezea mtu fulani aliyelipa gharama zote za kuzoeza na kuendeleza korasi katika kufanya tamthilia jukwaani. Watu wa jinsi hiyo walitwaa daraka hili kwa kujitolea kwa sababu ya kupenda jiji lao na ndio waliolipia gharama zile kutoka mifuko yao wenyewe. Watu hao walijivunia fahari ya kutumia pesa nyingi kuandaa mambo yote yaliyohitajiwa kwa ajili ya mcharazo bora. Neno hilo lilikua likaja kumaanisha “kugawilia, andalia kwa wingi sana.” (Linganisha 2 Petro 1:11.) Kwa hiyo Petro atuhimiza tujigawie, si kipimo fulani tu cha ujitoaji kimungu, bali wonyesho ulio kamili kabisa unaowezekana wa sifa hii yenye thamani kubwa.

10, 11. (a) Kwa nini jitihada yahitajiwa ili kusitawisha na kudhihirisha ujitoaji kimungu? (b) Twaweza kushindaje mng’ang’ano?

10 Ingawa hivyo, kwa nini jitihada hiyo yahitajiwa ili kusitawisha na kudhihirisha ujitoaji kimungu? Kwanza, kuna ule mng’ang’ano ambao ni dhidi ya mnofu wenye dhambi. Kwa kuwa “mbetuko wa moyo wa mwanadamu ni mbaya tangu ujana wake na kuendelea,” si rahisi kufuatia maisha ya kutii wenye utendaji kwa Mungu. (Mwanzo 8:21, NW; Warumi 7.21-23) “Wote wale wanaotamani kuishi kwa ujitoaji kimungu kwa kushirikiana na Kristo Yesu watanyanyaswa pia,” asema mtume Paulo. (2 Timotheo 3:12, NW) Ndiyo, ni lazima Mkristo ambaye hujitahidi kuishi kwa njia yenye kupendeza Mungu awe tofauti na ulimwengu. Yeye ana fungu la viwango vilivyo tofauti na shabaha zilizo tofauti. Kama Yesu alivyoonya, hii huamsha chuki ya ulimwengu mwovu huu.—Yohana 15:19; 1 Petro 4:4.

11 Hata hivyo, twaweza kushinda mng’ang’ano huo, kwa maana “Yehova ajua jinsi ya kukomboa watu wenye ujitoaji kimungu kutoka katika jaribu.” (2 Petro 2:9, NW) Ingawa hivyo, ni lazima sisi tufanye sehemu yetu kwa kuendelea kufuatia ujitoaji kimungu.

Kusitawisha Ujitoaji Kimungu

12. Petro aonyeshaje kinachohitajiwa ili kusitawisha ujitoaji kimungu kwa kipimo kamili zaidi?

12 Basi, je! wewe waweza kusitawishaje huu ujitoaji kimungu kwa kipimo kamili zaidi? Mtume Petro aandaa kidokezi. Kwenye 2 Petro 1:5, 6, wakati anapoorodhesha sifa ambazo ni lazima zigawiwe imani yetu, yeye aorodhesha maarifa kabla ya ujitoaji kimungu. Mapema zaidi katika sura ile ile, yeye aliandika hivi: “Nguvu zake za kimungu zimetupa sisi kwa uhuru mambo yote yahusuyo maisha na ujitoaji kimungu, kupitia maarifa sahihi ya mmoja aliyetuita sisi.” (2 Petro 1:3, NW) Hivyo Petro ashirikisha ujitoaji kimungu pamoja na maarifa sahihi kuhusu Yehova.

13. Kwa nini maarifa sahihi yahitajiwa sana katika kusitawisha ujitoaji kimungu?

13 Kwa uhakika, haiwezekani kusitawisha ujitoaji kimungu bila maarifa sahihi. Kwa nini? Basi, kumbuka kwamba ujitoaji kimungu ni kuelekea Yehova binafsi na huthibitishwa kwa njia ambayo sisi huishi maisha zetu. Hivyo maarifa sahihi kuhusu Yehova yahitajiwa sana, kwa kuwa yahusisha ndani kupata kumjua yeye kibinafsi, kwa uhusiano wa ndani, kujua sifa na njia zake kikamili. Zaidi ya hilo, yahusisha ndani kujitahidi kumwiga yeye. (Waefeso 5:1) Kadiri tufanyavyo maendeleo katika kujifunza kuhusu Yehova na katika kuonyesha njia na sifa zake katika maisha zetu, ndivyo tupatavyo kumjua vizuri zaidi. (2 Wakorintho 3:18; linganisha 1 Yohana 2:3-6.) Jambo hilo, nalo, huwa na tokeo la kuzithamini kwa kina kirefu zaidi sifa za Yehova zilizo za bei kubwa sana, likitokeza kipimo kamili zaidi cha ujitoaji kimungu.

14. Ili kupata maarifa sahihi, programu yetu ya funzo la kibinafsi yapasa kuhusisha nini, na kwa nini?

14 Wapataje maarifa sahihi hayo? Hakuna njia za mkato. Ili tupate maarifa sahihi, ni lazima tuwe na bidii yenye uendelevu wa kujifunza Neno la Mungu na vichapo vyenye msingi wa Biblia. Funzo hilo la kibinafsi lapasa kutia ndani programu yenye ukawaida wa kusoma Biblia, kama ile iliyoratibiwa kuhusiana na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. (Zaburi 1:2) Kwa kuwa Biblia ni zawadi kutoka kwa Yehova, yale tufanyayo kuhusiana na funzo la kibinafsi la Biblia ni wonyesho wa kadiri ambavyo sisi twathamini zawadi hiyo. Tabia zako za funzo la kibinafsi zafunua nini kuhusu kina cha uthamini wako wa maandalizi ya kiroho ya Yehova?—Zaburi 119:97.

15, 16. (a) Ni nini chaweza kutusaidia tusitawishe hamu ya kiroho kwa funzo la kibinafsi la Biblia? (b) Ili funzo la kibinafsi la Biblia liwe na tokeo la kufanya tusitawishe ujitoaji kimungu, jambo gani lifanywe wakati wa kusoma kisehemu cha Neno la Mungu?

15 Yakubalika kwamba, kusoma na kujifunza si mambo rahisi kwa watu fulani. Lakini muda fulani upitapo na jitihada ifanywapo, wewe waweza kukuza hamu ya kiroho ya kutaka kuwa na funzo la kibinafsi la Biblia. (1 Petro 2:2) Ufikiripo kwa kuthamini mambo yote ambayo Yehova Mungu amefanya, anafanya, na bado atafanya kwa ajili yako, moyo wako utakusukuma ujifunze yote uwezayo kuhusu yeye.—Zaburi 25:4.

16 Lakini ili funzo hilo la kibinafsi la Biblia liwe na tokeo la kukufanya ukuze ujitoaji kimungu, huwezi kuwa na lengo la kumaliza tu kusoma kurasa za habari fulani au kujaza habari tu katika akili yako. Badala ya hivyo, usomapo kisehemu cha Neno la Mungu, ni lazima uchukue wakati wa kufikiria habari zile, ukijiuliza maswali kama haya: ‘Jambo hili lanifundisha nini kuhusu sifa na njia nyororo za Yehova? Ni jinsi gani mimi naweza kufanana zaidi na Yehova katika mambo haya?’

17. (a) Twajifunza nini kuhusu rehema ya Yehova kutokana na kitabu cha Hosea? (b) Kufikiria rehema ya Yehova kutuathirije?

17 Fikiria kielelezo. Wakati fulani uliopita usomaji wa Biblia tuliogawiwa kufanya katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ulitupitisha katika kitabu cha Hosea. Baada ya kumaliza kusoma kitabu hiki cha Biblia, ungeweza kujiuliza hivi: ‘Mimi najifunza nini kuhusu Yehova akiwa Mtu—sifa zake na njia zake—kutokana na kitabu hiki?’ Jinsi kitumiwavyo na waandikaji wa baadaye wa Biblia yaonyesha kwamba twajifunza mengi kuhusu rehema nyororo ya Yehova kutokana na kitabu cha Hosea. (Linganisha Mathayo 9:13 pamoja na Hosea 6:6; Warumi 9:22-26 pamoja na Hosea 1:10 na 2:21-23.) Nia ya Yehova kuwaonyesha Israeli rehema ilifanyiwa kielezi na mishughuliko ya Hosea pamoja na mke wake, Gomeri. (Hosea 1:2; 3:1-5) Ingawa umwagaji damu, uibaji, uasherati, na ibada ya sanamu vilienea sana katika Israeli, Yehova ‘alisema na Israeli kwa maneno ya kumtuliza moyo.’ (Hosea 2:13, 14; 4:2) Yehova hakuwa na wajibu wa kuonyesha rehema hiyo lakini angefanya hivyo kwa ‘hiari yake mwenyewe,’ mradi Waisraeli wangedhihirisha toba yenye kuhisiwa moyoni na wageuke kutoka kwenye mwendo wao wa dhambi. (Hosea 14:4; linganisha Hosea 3:3.) Wewe ufikiripo hivyo kuhusu rehema ya Yehova isiyo ya kikawaida, itachochea moyo wako, iimarishe ufungamano wako wa kibinafsi kwake.

18. Baada ya kufikiria rehema ya Yehova kama vile yakaziwa katika Hosea, ungeweza kujiuliza nini?

18 Ingawa hivyo, mengi zaidi yahitajiwa kabisa. “Wenye furaha ni wenye rehema, kwa kuwa wao wataonyeshwa rehema,” akasema Yesu. (Mathayo 5:7, NW) Kwa hiyo, baada ya kufikiria rehema ya Yehova kama vile yakaziwa katika kitabu cha Hosea, jiulize hivi: ‘Mimi naweza kuigaje rehema ya Yehova kwa njia nzuri zaidi katika mishughuliko yangu pamoja na wengine? Ikiwa ndugu au dada ambaye ametenda dhambi dhidi yangu au akanikosea aomba msamaha, je! mimi husamehe “kwa uchangamfu”?’ (Warumi 12:8; Waefeso 4:32) Ikiwa wewe hutumikia katika kundi ukiwa mzee aliyewekwa rasmi, ungeweza kujiuliza hivi: ‘Ninaposhughulikia mambo ya hukumu, ni jinsi gani mimi naweza kumwiga vizuri zaidi Yehova, ambaye huwa “tayari kusamehe,” hususa iwapo mtenda kosa aonyesha ushuhuda wa kweli wa toba yenye kuhisiwa moyoni?’ (Zaburi 86:5; Mithali 28:13) ‘Nitafute nini kuwa msingi wa kutanua rehema?’—Linganisha Hosea 5:4 na 7:14.

19, 20. (a) Tokeo huwa nini funzo la Biblia likifanywa kikamili? (b) Ni nini msaada zaidi katika kusitawisha ujitoaji kimungu, na makala ifuatayo itazungumzia nini?

19 Lo, funzo lako la Biblia la kibinafsi huthawabisha kama nini lifanywapo kwa njia hiyo ya ukamili! Moyo wako utafurikwa na uthamini wa sifa za Yehova zilizo za thamani kubwa. Na kwa kuendelea kujitahidi kuiga sifa hizi maishani mwako, wewe utaimarisha ufungamano wako wa kibinafsi kwake. Kwa njia hiyo utakuwa ukifuatia ujitoaji kimungu ukiwa mtumishi wa Yehova aliyejiweka wakfu na kubatizwa.—1 Timotheo 6:11.

20 Msaada zaidi katika kusitawisha sifa hii yenye thamani kubwa waweza kupatikana katika Yesu Kristo—aliye kielelezo kikamilifu cha ujitoaji kimungu. Kufuata kielelezo cha Yesu kutakusaidiaje katika kusitawisha na pia kudhihirisha ujitoaji kimungu? Makala inayofuata itazungumzia swali hilo na maswali yenye kuhusiana nalo.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa habari ya neno la Kigiriki di·oʹko (“fuatia”), The New International Dictionary of New Testament Theology yafafanua kwamba katika maandishi sanifu, neno hilo “[kihalisi] lamaanisha kufukuza [kitu] mbio, kufuatia, kukimbia kwa kufuata, . . . na [kitamathali] lamaanisha kufuatia kitu fulani kwa bidii, kujaribu kufikia kitu fulani, kujaribu kupata.”

Wewe Ungejibuje?

◻ Kwa nini ubatizo siyo hatua ya mwisho ambayo wewe huchukua katika mwendo wako wa Kikristo?

◻ Ni nini maana ya “ujitoaji kimungu,” nawe waonyeshaje uthibitisho wa kwamba unao?

◻ Kwa nini jitihada ya kujikakamua yahitajiwa ili kukuza ujitoaji kimungu?

◻ Ni jinsi gani wewe waweza kusitawisha ujitoaji kimungu katika kipimo kamili zaidi?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki