Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 3/1 kur. 18-23
  • Fuata Kielelezo cha Yesu cha Ujitoaji Kimungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fuata Kielelezo cha Yesu cha Ujitoaji Kimungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kama Baba, Kama Mwana
  • Kuzoea Ujitoaji Kimungu Kuelekea Washirika wa Jamaa
  • “Kwa Kusudi Hili Mimi Nimetokea”
  • Tieni Ujitoaji Kimungu Katika Uvumilivu Wenu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Ongezeni Kwenye Uvumilivu Wenu Ujitoaji-kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Fuatieni Ujitoaji Kimungu Mkiwa Wakristo Waliobatizwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Karibu Kwenye “Ujitoaji Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 3/1 kur. 18-23

Fuata Kielelezo cha Yesu cha Ujitoaji Kimungu

“Siri takatifu ya huu ujitoaji kimungu yakiriwa wazi kuwa ni kubwa: ‘Yeye [Yesu] alidhihirishwa katika mnofu.’”—1 Timotheo 3:16, NW.

1. (a) Ni swali gani lililokaa bila kujibiwa kwa zaidi ya miaka 4,000? (b) Jibu lilitolewa wakati gani na jinsi gani?

NI SWALI lililokaa bila kujibiwa kwa miaka zaidi ya 4,000. Tangu wakati ule ule ambapo binadamu wa kwanza, Adamu, alishindwa kushika uaminifu wa kimaadili, swali lilikuwa: Ujitoaji kimungu udhihirishweje miongoni mwa ainabinadamu? Mwishowe, katika karne ya kwanza W.K., Mwana wa Mungu alipokuja duniani, jibu lilitolewa. Katika kila wazo, neno, na tendo, Yesu Kristo alionyesha kwamba alikuwa na ufungamano wa kibinafsi na Yehova. Hivyo aliondoa shela yenye kufunika ile ‘siri takatifu ya ujitoaji kimungu,’ akionyesha njia ya wanadamu waliojiweka wakfu ya kudumisha ujitoaji huo.—1 Timotheo 3:16.

2. Katika kufuatia ujitoaji kimungu, kwa nini tufikirie kwa ukaribu kielelezo cha Yesu?

2 Katika kufuatia ujitoaji kimungu tukiwa Wakristo waliojiweka wakfu na kubatizwa, yafaa ‘tufikirie kwa ukaribu’ kielelezo cha Yesu. (Waebrania 12:3, NW) Kwa nini? Kwa sababu mbili. Kwanza, kielelezo cha Yesu chaweza kutusaidia tusitawishe ujitoaji kimungu. Yesu alimjua Baba yake kuliko mtu mwingine yeyote. (Yohana 1:18) Na Yesu aliiga njia na sifa za Yehova kwa ukaribu sana hivi kwamba angeweza kusema hivi: “Aliyeniona mimi amemwona Baba [pia, NW].” (Yohana 14:9) Basi, kupitia maisha na huduma ya Yesu twaweza kupata uthamini wa kina kirefu zaidi kwa sifa nyororo za Yehova, hivyo tukiimarisha ufungamano wetu wa kibinafsi kwa Muumba wetu mwenye upendo. Pili, kielelezo cha Yesu chaweza kutusaidia kudhihirisha ujitoaji kimungu. Yeye aliweka kielelezo kilicho kikamilifu cha mwenendo unaodhihirisha ujitoaji kimungu. Hivyo ingefaa sisi tufikirie jinsi twaweza ‘kumvaa Kristo,’ yaani, tumchukue kuwa kigezo, tuige kielelezo chake.—Warumi 13:14.

3. Programu yetu ya funzo la Biblia la kibinafsi yapasa kuhusisha nini ndani, na kwa nini?

3 Si kila jambo ambalo Yesu alisema na kutenda lilihifadhiwa kwa namna ya maandishi. (Yohana 21:25) Kwa hiyo, mambo yaliyorekodiwa chini ya uvuvio wa kimungu yapasa yatupendeze sisi kihususa. Kwa hiyo programu ya funzo la Biblia la kibinafsi yapasa ihusishe ndani kusoma kwa ukawaida yale masimulizi ya Gospeli kuhusu maisha ya Yesu. Lakini ili usomaji huo utusaidie katika ufuatiaji wetu wa ujitoaji kimungu, ni lazima tuchukue wakati wa kufikiria kwa uthamini mambo tusomayo. Ni lazima pia tuwe chonjo kutazama ng’ambo ya mambo yale yenye kuonekana waziwazi.

Kama Baba, Kama Mwana

4. (a) Ni nini huonyesha kwamba Yesu alikuwa mtu mwenye uchangamfu na hisia ya kina kirefu? (b) Yesu alichukua hatua gani ya kwanza katika kushughulika na wengine?

4 Fikiria kielelezo. Yesu alikuwa mtu mwenye uchangamfu na hisia ya kina kirefu. Angalia kutokana na Marko 10:1, 10, 13, 17, ndiye aliyechukua hatua ya kwanza kuwafikia wenye kuhitaji msaada. Hivyo, twasoma kwamba alitupa jicho “akaona” mjane wa Naini ambaye mwana wake aliyekufa alikuwa akichukuliwa mbali. Ndipo yeye ‘akafikilia’ na kufufua mvulana huyo, na hakuna mtajo wowote kwamba kuna mtu yeyote aliyemwomba afanye hivyo. (Luka 7:13-15) Pia, bila kuombwa afanye hivyo, yeye alichukua hatua ya kwanza akaponya mwanamke kiwete na mwanamume mwenye ugonjwa wa kujazana maji mwilini.—Luka 13:11-13; 14:1-4.

5. Masimulizi haya ya huduma ya Yesu yatufundisha nini kuhusu sifa na njia za Yehova?

5 Usomapo kuhusu vituko hivyo, ngoja kidogo ujiulize hivi: ‘Kwa kuwa Yesu aliiga Baba yake kikamilifu, masimulizi haya yaniambia nini mimi kuhusu sifa na njia za Yehova?’ Hayo yapasa kutupa sisi uhakikishio wa kwamba Yehova ni Mungu mwenye uchangamfu na hisia ya kina kirefu. Uzidifu wa kupendezwa kwake daima na jamaa ya kibinadamu umemsukuma achukue hatua ya kwanza kushughulika nao. Haikuwa lazima ashurutike kutoa Mwana wake awe “ukombozi kwa watu wengi.” (Mathayo 20:28, ZSB; Yohana 3:16) Yeye hutafuta fursa za ‘kufungamana’ na wale ambao wataka kumtumikia kwa sababu ya upendo. (Kumbukumbu 10:15, NW) Kama vile Biblia isemavyo: “Macho ya Bwana [Yehova, NW] hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake.”—2 Nyakati 16:9.

6. Tokeo huwa nini tuonyeshapo uchangamfu na hisia ya kina kirefu kama vile Mwana wake alivyoweka kielelezo?

6 Kufikiria hivyo uchangamfu wa Yehova na hisia ya kina kirefu, kama ilivyoonyeshwa na kielelezo cha Mwana wake, kutagusa moyo wako, kuujaze uthamini mkubwa zaidi kwa sifa Zake nyororo na zenye kuvutia. Hilo, nalo, litakuvuta kwake. Utasukumwa na moyo umfikie kwa uhuru katika sala nyakati zote na chini ya hali zote. (Zaburi 65:2) Litaimarisha ufungamano wako wa kibinafsi kwake.

7. Baada ya kufikiria uchangamfu na hisia ya kina kirefu ya Yehova, wewe wapaswa kujiuliza nini, na kwa nini?

7 Ingawa hivyo, kumbuka kwamba ujitoaji kimungu wahusisha ndani mengi kuliko hisia ya kiibada tu. Kama vile mwanachuo wa Biblia R. Lenski aarifu, ‘wahusisha ndani mtazamo wetu wote wenye staha nyingi na ibada na vitendo vinavyotokana nao.” (Italiki ni zetu.) Kwa hiyo baada ya kufikiria uchangamfu wa Yehova na hisia ya kina kirefu kama ilivyoonyeshwa na kielelezo cha Yesu, jiulize hivi: ‘Ni jinsi gani mimi naweza kufanana zaidi na Yehova katika jambo hili? Je! wengine huniona mimi kuwa mwenye kufikilika?’ Ikiwa wewe ni mzazi, ni lazima uwe mwenye kukaribika kwa watoto wako. Na ikiwa wewe ni mzee wa kundi, hakika yakupasa uwe mwenye kukaribika. Basi, ni jambo gani litafanya uwe mwenye kufikilika zaidi? Ni uchangamfu na hisia ya kina kirefu. Ni lazima usitawishe upendezi wa kweli na wa moyo mweupe katika wengine. Ujalipo kweli kweli kuhusu wengine na uwapo na nia ya kujitoa uwatumikie, wao watahisi jambo hilo na kujisikia wakivutwa kwako.

8. (a) Wewe wapaswa kutunza nini akilini usomapo masimulizi ya Biblia kuhusu Yesu? (b) Sisi twajifunza nini kuhusu Yehova kutokana na masimulizi yaliyotajwa katika kielezochini?

8 Kwa hiyo usomapo masimulizi ya Biblia kuhusu Yesu, kumbuka kwamba waweza kujifunza mengi kuhusu Yehova akiwa mtu kutokana na mambo ambayo Yesu alisema na kutenda.” Na wakati uthamini wako kwa sifa za Mungu, kama zilivyoonyeshwa na Yesu,a ukusukumapo ujaribu kufanana Naye zaidi, hapo huwa unaonyesha uthibitisho wa kuwa kwako na ujitoaji kimungu.

Kuzoea Ujitoaji Kimungu Kuelekea Washirika wa Jamaa

9, 10. (a) Upendo na hangaiko la Yesu kwa mama yake, Mariamu, vilidhihirisha nini muda mfupi tu kabla yeye hajafa? (b) Yaonekana ni kwa nini Yesu aliaminisha utunzaji wa Mariamu mikononi mwa mtume Yohana wala si kwa mmoja wa ndugu zake mwenyewe za kimnofu?

9 Maisha na huduma ya Yesu Kristo yafunua mengi kuhusu jinsi ujitoaji kimungu wapasa kudhihirishwa. Kielelezo chenye kugusa moyo kimeandikwa kwenye Yohana 19:25-27 NW, ambapo twasoma hivi: “Hata hivyo, kando ya mti wa mateso wa Yesu walikuwapo wamesimama mama yake na dada ya mama yake; Mariamu mke wa Klopasi, na Mariamu Magdalene. Kwa hiyo Yesu, kwa kuona mama yake na yule mwanafunzi ambaye yeye alipenda [Yohana] wakiwa wamesimama kando hapo, alisema hivi kwa mama yake: ‘Mwanamke, ona! Mwana wako!’ Halafu akasema hivi kwa yule mwanafunzi: ‘Ona! Mama yako!’ Na tangu saa hiyo na kuendelea yule mwanafunzi akamchukua akampeleka kwenye nyumba yake mwenyewe.”

10 Wazia hilo! Dakika chache tu kabla yeye hajasalimisha uhai wake wa kidunia, upendo na hangaiko la Yesu lilimsukuma aaminishe utunzaji wa mama yake, Mariamu, (ambaye yaonekana kufikia sasa alikuwa mjane) mikononi mwa Yohana mtume mpendwa. Lakini kwa nini iwe Yohana na si mmoja wa ndugu za kimnofu za Yesu mwenyewe? Kwa sababu hangaikio kubwa zaidi la Yesu halikuwa mahitaji ya Mariamu ya kimwili tu, bali hali njema yake ya kiroho hasa. Na mtume Yohana (ambaye yawezekana alikuwa binamu ya Yesu) alikuwa amethibitisha imani yake, hali hakuna kionyeshi cha kwamba ndugu za Yesu za kimnofu walikuwa waamini kufikia hapo.—Mathayo 12:46-50; Yohana 7:5.

11. Kulingana na Paulo, Mkristo aweza kuzoeaje ujitoaji kimungu katika nyumba yake mwenyewe? (b) Kwa nini Mkristo aliye wa kweli hufanya uandalizi kwa ajili ya wazazi wazee-wazee?

11 Sasa, huu ulikuwaje udhihirisho wa ujitoaji kimungu? Mtume Paulo aeleza hivi: “Uwaheshimu wajane walio wajane kweli kweli. Lakini mjane akiwa ana watoto au wajukuu, na wajifunze kwanza kuyatenda yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe, na kuwalipa wazazi [na wazazi wa wazazi, NW] wao. Kwa kuwa hili lakubalika mbele za Mungu.” (1 Timotheo 5:3, 4) Kama vile asemavyo Paulo, kuheshimu wazazi kwa kuwaandalia riziki ya kimwili iwapo yahitajiwa kabisa ni wonyesho wa ujitoaji kimungu. Jinsi gani hivyo? Yehova, Mwanzishi wa mpango wa jamaa, aamuru watoto waheshimu wazazi wao. (Waefeso 3:14, 15; 6:1-3) Kwa sababu hiyo, Mkristo wa kweli hutambua kwamba kutunza daraka hilo la kijamaa hakuonyeshi upendo kwa wazazi wake tu bali hudhihirisha staha nyingi kwa Mungu pia na utii kwa amri zake.—Linganisha Wakolosai 3:20.

12. Wewe waweza kuzoeaje ujitoaji kimungu kuelekea wazazi wazee-wazee, na matilaba yapaswa kuwa

12 Basi, je! wewe waweza kuzoeaje ujitoaji kimungu kuelekea washirika wa jamaa? Hakika jambo hili lingehusisha ndani kupanga kutunza mahitaji ya kiroho na ya kimwili ya wazazi wazee-wazee, kama Yesu alivyofanya. Kutokufanya hivyo kungefunua ukosefu wa ujitoaji kimungu. (Linganisha 2 Timotheo 3:2, 3, 5.) Mkristo aliyejiweka wakfu huwaandalia riziki wazazi wahitaji, si ili aonyeshe fadhili tu au atimize wajibu bali kwa sababu yeye apenda jamaa yake na atambua maoni ya ustahifu mwingi ambayo Yehova huwa nayo kuhusu kutunza daraka hilo. Hivyo, kutunza kwake wazazi wazee-wazee ni wonyesho wa ujitoaji kimungu.b

13. Baba Mkristo aweza kuzoeaje ujitoaji kimungu kuelekea jamaa yake?

13 Ujitoaji kimungu waweza kuzoewa nyumbani kwa njia nyinginezo. Kwa kielelezo, baba Mkristo ana daraka la kuandalia jamaa yake kimwili, kihisia-moyo, na kiroho. Kwa hiyo, kuongezea kuandaa riziki ya kimwili, yeye hupanga kwa upendo kuwe na funzo la Biblia la jamaa lililo na ukawaida. Yeye huratibu wakati wa kushiriki kwa ukawaida katika huduma ya shambani pamoja na jamaa yake. Yeye ni mwenye usawaziko, akitambua uhitaji wao wa pumziko na tafrija pia. Na kwa hekima yeye huweka wazi mambo yapasayo kutangulizwa kwanza, bila kuruhusu utendaji wa kundi usababishe akose kuangalia jamaa yake. (1 Timotheo 3:5, 12) Kwa nini yeye hufanya yote haya? Si kwa sababu ya kuhisi akilazimika kutimiza wajibu tu bali kwa sababu ya kupenda jamaa yake. Yeye hutambua umaana ambao Yehova huweka juu ya mtu kutunza jamaa yake. Kwa kutimiza hivyo daraka lake akiwa mume na baba, yeye anakuwa akizoea ujitoaji kimungu.

14. Mke Mkristo aweza kudhihirishaje ujitoaji kimungu nyumbani?

14 Wake Wakristo pia wana daraka la kuzoea ujitoaji kimungu nyumbani. Jinsi gani? Biblia yasema kwamba mke apaswa “kuwa katika ujitiisho” kwa mume wake na apaswa kuwa na “staha ya kina kirefu” kwake. (Waefeso 5:22, 23, NW) Hata ikiwa mume wake si mwamini, mke apaswa “kuwa katika ujitiisho” kwake. (1 Petro 3:1, NW) Mwanamke Mkristo huonyesha unyenyekeo huo wa kimke kwa kuunga mkono mume wake katika maamuzi afanyayo maadamu hayagongani na sheria za Mungu. (Matendo 5:29) Na kwa nini mke hukubali fungu hili? Si kwa sababu ampenda tu mume wake bali hasa kwa sababu atambua kwamba ndivyo “ipendezavyo katika Bwana”—yaani, ni mpango wa Mungu kwa jamaa. (Wakolosai 3:18) Hivyo ujitiisho wake wenye nia kwa mume wake huwa ni wonyesho wa kwamba yeye ana ujitoaji kimungu.

“Kwa Kusudi Hili Mimi Nimetokea”

15. Yesu alidhihirisha ujitoaji kimungu kwa njia gani ya kutokeza?

15 Moja ya njia za kutokeza ambavyo Yesu alidhihirisha ujitoaji kimungu ilikuwa kwa ‘kujulisha wazi habari njema za ufalme wa Mungu.’ (Luka 4:43, NW) Baada ya ubatizo wake katika Yordani katika 29 W.K., Yesu alitumia miaka mitatu na nusu iliyofuata akishughulika sana sana na kazi hii iliyo ya maana kuliko zote. “Ni kwa kusudi hili kwamba mimi nimetokea,” yeye akaeleza. (Marko 1:38; Yohana 18:37, NW) Lakini huu ulikuwaje udhihirisho wa ujitoaji kimungu wake?

16, 17. (a) Ni nini kilichosukuma Yesu ashughulike sana sana kuhubiri na kufundisha? (b) Kwa nini huduma ya Yesu ya kuhubiri na kufundisha ilikuwa udhihirisho wa ujitoaji kimungu wake?

16 Kumbuka kwamba ujitoaji kimungu wahusisha ndani kuishi kwa njia yenye kufurahisha Mungu kwa sababu wewe wampenda na kuzithamini kwa kina kirefu sifa zake zenye kukuvuta umwonyeshe upenzi mwingi. Basi, je! ni kitu gani kilichosukuma Yesu atumie miaka yake ya mwisho duniani akishughulika sana sana na kazi ya kuhubiri na kufundisha? Je! ni hisia tu ya kiwajibu au faradhi fulani? Hakuna shaka kwamba Yesu alihangaikia watu. (Mathayo 9:35, 36) Naye aling’amua kikamili kwamba kupakwa kwake mafuta kwa roho takatifu kulimweka rasmi na kukampa utume wa kutekeleza huduma yake. (Luka 4:16-21) Hata hivyo, yeye alikuwa na matilaba ya kina kirefu zaidi.

17 “Nampenda Baba,” Yesu akawaeleza wazi mitume wake usiku wa mwisho wa maisha yake ya kidunia. (Yohana 14:31) Msingi wa upendo huo ni maarifa ya kuzijua sifa za Yehova kwa kina kirefu na kwa uhusiano wa ndani. (Luka 10:22) Kwa kusukumwa na moyo wenye kuchochewa na uthamini wa kina kirefu, Yesu alipata upendezo katika kufanya penzi la Mungu. (Zaburi 40:8) Hicho kilikuwa “chakula” chake—chenye kuhitajiwa sana kwa maisha, chenye ladha nzuri sana katika kaakaa lake. (Yohana 4:34) Yeye aliweka kielelezo kikamilifu cha ‘kutafuta kwanza ufalme’ badala ya kujitanguliza mwenyewe. (Mathayo 6:33) Kwa hiyo jambo lililofanya huduma yake ya kuhubiri na kufundisha iwe wonyesho wa kwamba alikuwa na ujitoaji kimungu si aliyofanya tu wala kadiri alivyofanya, bali ni sababu ya kuyafanya.

18. Kwa nini kuwa na ushiriki fulani katika huduma kwa lazima si udhihirisho wa ujitoaji kimungu?

18 Katika jambo hili, sisi twaweza kufuataje kielelezo cha “kigezo,” Yesu? (1 Petro 2:21, NW) Wote ambao huitikia mwaliko wa Yesu wa “kuja uwe mfuasi wangu” wana utume wa kimungu kuhubiri habari njema za Ufalme na kufanya wanafunzi. (Luka 18:22, NW; Mathayo 24:14; 28:19, 20) Je! hii yamaanisha kwamba kwa kuwa na ushiriki fulani katika kujulisha wazi habari njema, hapo sisi huwa tunafuatia ujitoaji kimungu? Si kwa lazima. Kama tungejihusisha katika huduma kivoloya au kwa jinsi ya kuonyesha kidogo, au ili tufurahishe tu wanajamaa au wengine, haingefikiriwa kuwa ‘tendo la ujitoaji kimungu.’—2 Petro 3:11, NW.

19. (a) Ni nini yapasa kuwa sababu ya msingi ya mambo tutendayo katika huduma? (b) Matokeo huwa nini tusukumwapo na upendo wenye mizizi ya kina kirefu kwa Mungu?

19 Kama Yesu, ni lazima matilaba yetu yawe ya kina kirefu zaidi. Yesu alisema: “Ni lazima wewe upende Yehova Mungu wako kwa moyo wako mzima [hisia za moyo, tamaa, na kuhisi kwa yule mtu wa ndani] na kwa nafsi yako nzima [uhai wako na kuwako kwako kote] na kwa akili yako nzima [uwezo wako wa weledi] na kwa imara yako nzima.” Mwandishi mmoja aliongezea jambo hilo kwa kusema: “Hilo . . . lazidi kwa mbali ustahiki wa matoleo na dhabihu zote.” (Marko 12:30, 33, 34, NW) Kwa hiyo la maana si yale tufanyayo tu, bali sababu ya sisi kuyafanya. Ni lazima sababu ya msingi ya sisi kufanya huduma yetu iwe upendo ulio na mizizi yenye kina kirefu kwa Mungu, ambao wahusisha ndani kila sehemu ya sisi. Iwapo hivyo, hatutatosheka kwa kuonyesha kidogo tu kuwa tunashiriki, bali tutasukumwa na nia ya kuonyesha tuna kina cha ujitoaji kimungu kwa kufanya yoteyote tuwezayo. (2 Timotheo 2:15) Wakati uleule, iwapo matilaba yetu ni upendo kwa Mungu, hatutakuwa wachambuzi, tukilinganisha huduma yetu na ile ya wengine.—Wagalatia 6:4.

20. Ni jinsi gani sisi twaweza kunufaika kikamili na kielelezo cha Yesu katika kufuatia ujitoaji kimungu?

20 Twaweza kuwa na shukrani kama nini kwamba Yehova ametufunulia siri takatifu ya ujitoaji kimungu! Kwa kujifunza kwa uangalifu mambo ambayo Yesu alisema na kutenda na kwa kujitahidi kumwiga yeye, sisi tutasaidiwa tusitawishe na pia tudhihirishe ujitoaji kimungu kwa kipimo kamili zaidi. Yehova atatubariki kwa wingi tufuatapo kielelezo cha Yesu katika kufuatia ujitoaji kimungu tukiwa Wakristo waliojiweka wakfu na kubatizwa.—1 Timotheo 4:7, 8.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa vielelezo zaidi, fikiria tujifunzavyo juu ya Yehova kutokana na masimulizi yanayofuata: Mathayo 8:2, 3; Marko 14:3-9; Luka 21:1-4; na Yohana 11:33-36

b Kwa mazungumzo kamili juu ya mambo yenye kuhusika katika kuzoea ujitoaji kimungu kuelekea wazazi wazee-wazee, ona Mnara wa Mlinzi, Juni 1, 1987, kurasa 13-18.

Je! Wewe Wakumbuka?

◻ Katika kufuatia ujitoaji kimungu, kwa nini tufikirie kielelezo cha Yesu?

◻ Twajifunza nini juu ya Yehova kutokana na uchangamfu na hisia ya kina kirefu iliyoonyeshwa na Yesu kwa kielelezo?

◻ Sisi twaweza kudhihirishaje ujitoaji kimungu kuelekea wanajamaa?

◻ Ili huduma yetu iwe wonyesho wa ujitoaji kimungu, ni lazima matilaba yetu iwe nini?

[Picha katika ukurasa wa 21]

Baba Mkristo ana daraka la kuandalia jamaa yake kimwili, kihisia-moyo, na kiroho

[Picha katika ukurasa wa 23]

“Lakini mjane akiwa ana watoto au wajukuu, na . . . [wayatende] yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe, na kuwalipa wazazi [na wazazi wa wazazi, NW] wao.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki