Muono-Ndani Juu ya Habari
Kuungama Hatia Yao ya Damu
“Sisi tuliita ile vita [Vita ya Ulimwengu 2] vita takatifu na tukapeleka watu kwenye nyanja za mapigano,” akakiri Shingen Hosokawa, katibu-mkuu wa Ofisi ya Hekalu la Farakano Otani la Kibuddha la Bara Safi la Kweli katika Japani. “Sisi hatuna la kufanya ili kuzidiwa na aibu mbele ya Buddha mtakatifu.” Kwenye “Ibada ya Ukumbusho wa Wafu wa Vita” hivi majuzi, miaka 45 baada ya kumalizika kwa Vita ya Ulimwengu 2, farakano hilo, lenye waamini zaidi ya milioni tano, lilikiri daraka lalo katika “kushirikiana kwa nia katika [jitihada za kivita za] Vita ya Ulimwengu 2.” “Mamlaka ya Kibuddha ya tangu zamani haijapata kutaarifu wazi hivyo daraka layo yenyewe la kivita kwenye ibada ya kidini,” likasema Asahi Shimbun.
Hata hivyo, je! dini nyingi zaidi hazipasi “kuzidiwa na aibu” kwa sababu zilihimiza vijana wengi wanaume waende vitani? Kulingana na Kodansha Encyclopedia of Japan, karibu madhehebu zote za Kibuddha, “za Kikristo,” na za Kishinto katika Japani zilifanyiza Ushirika wa Kidini katika 1941 “ili kuandaa kinga ya kiroho kwa ajili ya taifa wakati wa vita.”
Ni jambo lenye kutarajiwa kwamba, ikirejezea milki ya ulimwengu ya dini bandia kuwa “Babuloni Mkubwa,” Biblia husema: “Ndiyo, katika yeye ilipatikana damu . . . ya wale wote ambao wamechinjwa juu ya dunia.” (Ufunuo 18:2, 24, NW) Je! Yehova Mungu, Mpaji wa uhai wa kibinadamu, atataka hesabu kwa wanadini hao kwa sababu ya hatia yao ya damu? Sura iyo hiyo ya Ufunuo yaaridhia kwa udhahiri jambo litakalopata Babuloni Mkubwa, ikitaarifu hivi: “Malaika kabambe akainua juu jiwe kama jiwe kubwa la kusagia na kulivurumisha ndani ya bahari, akisema: ‘Hivyo kwa mtupo wa ghafula Babuloni jiji kubwa litavurumishwa chini, nalo halitapatikana kamwe tena.’”—Ufunuo 18:21, NW.
Ukosefu wa Makuhani
Mafarakano ya Kibuddha katika Japani husumbuliwa-sumbuliwa na tatizo la mahekalu yasiyo na watu. Majirani wa mahekalu wasio na makuhani walio wakaaji wa kwao wanakinza kuzurura kwa wahuni katika eneo la hekalu na pia hatari ya kufoka kwa moto. Farakano la Myoshinji la Ubuddha wa Zen liliamua kushughulika na tatizo hilo kwa kuondolea mbali mahekalu au kuyaunganisha na yale yaliyo karibu. Zaidi ya asilimia 20 ya mahekalu 3,500 ya farakano la Myoshinji kotekote katika Japani ama hayana kuhani wa eneo la kwao ama hutumikiwa na makuhani wa kutoka mahekalu ya karibu.
Kwa nini shida hiyo? “Farakano hilo linatatizwa kupata waandamizi wa makuhani wenye kustaafu,” laeleza The Daily Yomiuri, “na makuhani vijana wamekinza kupelekwa wakatumikie mahekalu katika maeneo yaliyopungua idadi ya watu.” Farakano hilo lilijaribu kuzoeza wafanya kazi waliostaafu wawe makuhani lakini tayari limeachilia mbali mpango huo. Ingawa wafuasi wa Myoshinji wasema kwamba “huu si muda ambapo idadi ya mahekalu ndiyo ithibati ya imara,” haiwezi kukanwa kwamba uvutano wao unapungua.
Kwa kupendeza, kitabu cha Biblia cha Ufunuo chatabiri kwamba maji ya Eufrati, ambayo mfumo wa kidini wa ulimwenguni pote—“Babuloni Mkubwa”—umeyakalia, ‘yatakauka kabisa.’ (Ufunuo 16:12; 18:2, 9, 11, NW) Maji hayo yawakilisha nini? “Maji ambayo wewe uliona . . . humaanisha vikundi vya watu na umati wa watu na mataifa na ndimi.” (Ufunuo 17:15, NW) Kukauka kabisa kwa “maji” hayo, au waungaji mkono, kwatukia wazi katika makao ya Mashariki ya Babuloni Mkubwa.
Utatuzi
Ulio Mkamilifu
“Matisho yanayoongezeka sana ambayo sasa twayakabili . . . yana nguvu nyingi sana hivi kwamba hatua isipoanza kuchukuliwa sasa ili kuyabadili, bila kuepukika yataongoza kwenye matokeo ya kiuchumi yenye gharama za kulemea kabisa na kuangamiza mashirika ya kijamii na ya kisiasa,” yataarifu Taasisi ya Worldwatch, yenye kituo katika Washington, D.C., U.S.A. Mwaka uliopita ripoti ya kila mwaka ya taasisi hiyo ilionya kwamba mawimbi ya joto yenye kuua, hali za ukavu, na mafuriko yalikuwa mwonjo wa kimbele tu wa balaa nzito zaidi ambazo bado zitaikumba dunia iliyopigwa dharuba kali. Maeneo yaliyolengwa katika ripoti hiyo kwamba yaangaliwe bila kukawia ni kutia ndani udhibiti wa idadi ya watu, kutumia nishati vizuri, kupanda upya misitu, na kuzuia njaa kuu. Hata hivyo, taasisi hiyo yasema kwamba ‘mpango wa bila kukawia wa hatua ya tufe lote’ na ‘mabadiliko yenye kina sana katika kigezo cha mwenendo wa binadamu’ yahitajiwa ili kupata matokeo chanya.
Je! twaweza kutarajia kuona mpango wa tufe lote ambao utaleta mabadiliko yenye kina sana wakati wetu? Ndiyo, lakini si kupitia jitihada za binadamu yeyote wala kikundi cha wanadamu. Kwa nini sivyo? Kwa sababu nabii Yeremia aliandika hivi karne zilizopita: “Njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.” Bali, Biblia yaahidi kwamba Yehova Mungu ‘atawaangamiza wale wanaoangamiza dunia’ na ‘atanyoosha mambo’ ili kunufaisha wakaaji wa dunia.—Yeremia 10:23, UV; Ufunuo 11:18; Mika 4:3, 4, NW.