Je! Wewe Ungekaribisha Ziara?
Mmoja wa Mashahidi wa Yehova angependa kukuzuru wewe na kukusaidia uongeze maarifa yako juu ya Mungu, Ufalme wake, na makusudi yake, kama yalivyorekodiwa katika Biblia. Sisi tuna uhakika kwamba habari hizi zitakusaidia, kwa maana zitaandaa majibu ya kutegemeka kwa matatizo ambayo sisi sote twakabili leo. Mashahidi wa Yehova huandaa maagizo ya kibinafsi na ya kikundi katika Biblia bila malipo.
Hivyo basi ikiwa ungependa mtu mwenye kustahili akuzuru katika nyumba yako, au mahali fulani pafaapo, sisi tutaterema kukupangia hilo. Utasaidiwa upate si majibu tu kwa maswali yako ya Biblia bali pia majibu kwa matatizo ya leo yawezayo kutatuliwa kwa kutumia kanuni za Biblia. Ili ujipatie utumishi huu, kwa usahili jaza habari zenye kuombwa chini na uzipeleke kwenye anwani iliyo hapa chini.
Mimi ningependa kujua mengi zaidi juu ya Biblia. Tafadhali pangeni mtu fulani anitembelee.