“Nilikuwa Nikiwaka Hasira”
Msichana wa miaka 15 kutoka Knoxville, Tennessee, aliandika hivi: “Nilitaka kutoa asante zangu kwenu kwa ajili ya kitabu chenu kipya Questions Young People Ask—Answers That Work. Nimeona shangwe sana kukisoma.”
Halafu anaeleza kilichofanya aandike barua yake: “Nilikuwa nikiwaka hasira juu ya ndugu yangu kwa sababu alinisema nilipokosa kufanya jambo fulani nililopaswa kulifanya nyumbani. Kwa kuwa sasa kimetokea, nahisi nikiwa mwenye hatia na nimepanda juu kwenye chumba changu kuwaandikia na kusoma ‘Kwa Nini Ni Vigumu Sana Kuchukuliana na Ndugu na Dada Yangu?’ (Sura ya 6) Najua kitasaidia katika kuelekeana na matatizo wakati ujao.”
Vijana wanaelekeana na maswali mengi yanayotaka uamuzi unaofaa: Je! mimi niko tayari kufanya urafiki na mvulana au msichana? Naweza kuponaje hisia zilizovunjika kwa kutompata mtu niliyetazamia awe mwenzangu? Namna gani ngono kabla ya ndoa? Najuaje kama ni upendo halisi? Ni kazi-maisha gani ninayopaswa kuchagua? Naweza kuelekeanaje na mkazo wa vijana wa umri wangu? Kwa maswali ya jinsi hiyo na mengine, vijana wanahitaji majibu yanayofanya kazi.
Sisi tunahisi kwamba utanufaika sana kutokana na kitabu Questions Young People Ask—Answers That Work, kilicho na sura moja juu ya kila moja la maswali haya. Unaweza kupokea nakala ya kichapo hiki chenye picha za kuvutia kwa kujaza na kupeleka hati hii yenye anwani.
Ningependa kupokea kile kitabu chenye jalada gumu cha kurasa 320 Questions Young People Ask—Answers That Work.