“Kwa Nini Vitoto Vichanga Vinakufa?”
Hilo ndilo jambo ambalo familia iliyopoteza watoto wadogo wawili ilitaka kujua. Mwanamume kutoka Willowick, Ohio, U.S.A., alieleza hivi:
“Hivi karibuni, msiba ulitokea ndani ya familia yangu. Dada yangu wa kimwili alipoteza watoto wake wachanga wawili katika aksidenti mbaya sana ya gari. Bila shaka, familia nzima ilihuzunika sana. Mhubiri wao Mbaptisti hakutoa faraja yoyote ya Kimaandiko. Aliweza tu kusema, ‘Yalikuwa mapenzi ya Mungu’ na, ‘Mungu alihitaji malaika zaidi wawili.’
“Ingawa kulikuwa wakati mchache sana wa kufanya uchunguzi, nilirejezea kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko na kichwa chacho ‘Kwa Nini Vitoto Vichanga Vinakufa?’ Katika siku na majuma yaliyofuata, mke wangu nami tumeweza kushiriki pamoja na familia yangu majibu ya kikweli kwa mengi ya maswali yao, kama vile, ‘Kwa nini vitoto vichanga vinakufa?’ ‘Je! ni mapenzi ya Mungu kuchukua watoto kutoka kwa wazazi wao?’ na, la maana zaidi, ‘Kuna tumaini gani la kuona watoto hawa wazuri tena?’ Wazazi wangu wamesema wangependa kuja kwenye Jumba la Ufalme wakati ujao.”
Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko kina zaidi ya vichwa vya habari kuu 70. Vilivyotiwa ndani ni “Kifo,” “Motoni (Hell),” “Nafsi,” “Kuchukuliwa Kimwili Kutoka Duniani,” “Kuzaliwa Upya Katika Mwili Mwingine,” “Ngono,” “Kuwasiliana na Ulimwengu wa Roho,” na vingi zaidi. Faharisi yacho ya habari na maandiko yenye kurasa saba yaweza kukusaidia kupata majibu haraka. Ili kupokea nakala, tafadhali jaza na kupeleka kuponi hii.
Ningependa kupokea kile kitabu chenye jalada gumu cha kurasa 448 Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko.