Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 7/1 uku. 31
  • Walimtumaini Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Walimtumaini Yehova
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Kutembea kwa Nafsi Yote katika Njia ya Uzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Fanya Yehova Awe Itibari Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Je! Waweza Kumtumikia Yehova Ukiwa Painia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 7/1 uku. 31

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

Walimtumaini Yehova

MASHAHIDI WA YEHOVA wanaamriwa na Yehova kuhubiri habari njema ya Ufalme katika ulimwengu wote ili watu wa mataifa yote wawe na nafasi ya kujua juu ya ulimwengu mpya wa Mungu. Katika nchi nyinginezo, mara nyingi kwa kichocheo cha makasisi wa Jumuiya ya Wakristo, kazi yetu imezuiwa. Hiyo ndiyo hali katika nchi fulani katika Afrika. Lakini Mashahidi wa Yehova huko hufanya kama alivyofanya Mfalme Daudi. Alisema hivi: “Nimemtumaini Mungu, sitaogopa.” (Zaburi 56:11) Mambo yaliyoonwa na ndugu zetu katika bara hilo yanaonyesha kwamba walimtumaini Yehova na kuendelea na kazi yake ya maana.

Shahidi anayefanya kazi akiwa mwalimu mkuu katika shule alisisitiza juu ya kutii “Mungu kuliko wanadamu,” akitangaza rasmi kutokuwamo kwake kuelekea mambo ya Serikali. (Matendo 5:29) Alipigwa vibaya na kutazamiwa kupata hukumu ya kuwa msaliti. Kila mtu alifikiri kwamba angeuawa. Hata hivyo, Shahidi huyo alimtumaini Yehova. Alibaki mwaminifu akaeleza sababu zake za kidhamiri za msimamo wake. Tokeo? Aliachiliwa na kurudishwa mji wa nyumbani kwake, ambapo wajumbe wa Serikali waliompiga walimwomba radhi. Shahidi huyo mwaminifu alichukuliwa tena katika kazi ya kufundisha na kuongezwa cheo kuwa inspekta wa shule!

Mratibu wa shule moja alimfuta kazi mwalimu Shahidi. Mwezi mmoja baadaye mratibu huyo alikubali kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani kutoka kwa painia wa pekee akakubali funzo la Biblia. Baada ya kumaliza sura ya 6, alijiuzulu kuwa mratibu wa shule hiyo, naye na mke wake wakaanza kuhudhuria mikutano yote ya Mashahidi wa Yehova. Asubuhi ya Jumapili moja mwalimu aliyefutwa kazi alipata mshangao wa kupendeza kukutana na mtu huyo aliyemfuta kazi na kupata kwamba yeye alikuwa njiani kuwa ndugu wa kiroho.

Jambo jingine lililoonwa kutoka nchi iyo hiyo linatoa kielezi cha jinsi Mashahidi wa Yehova hukazia heshima kwa mipango ya Yehova na kufanya bidii kuendeleza usafi wa tengenezo. Painia wa pekee aliyekuwa akifanya kazi kwenye eneo lililo pekee alipata upinzani mwingi. Kwa kuwa alitoka kabila na eneo jingine, adui za kweli walitaka kumwondosha kijijini. Hata hivyo, chifu wa kijiji alielekeza kwenye mwenendo wake mzuri na matokeo mazuri ya huduma yake naye hakuruhusu kuondoshwa kwake. Chifu alikuwa ameona kwamba tangu kufika kwa painia wa pekee huyo, watu walikuwa wakiheshimu mamlaka zenye kutawala kwa kulipa kodi zao na kufanya kazi ya barabara ya jumuiya mara moja kila juma.—Warumi 13:1, 7.

Halafu, usiku mmoja Shahidi mwingine alikamatwa katika tendo la uzinzi pamoja na mwanamke asiye Shahidi. Kulikuwako machongezi, na painia wa pekee akaitwa mbele ya chifu, ambaye alimkaripia, akisema hivi: “Ndiye huyu ndugu yako aliyekamatwa katika tendo la uzinzi. Nyinyi Mashahidi wa Yehova hamko tofauti na dini nyingine.” Hata hivyo, painia wa pekee huyo alieleza hivi: “Ingawa sisi sio wakamilifu, tuko tofauti na dini nyingine kwa sababu hatuachilii matendo ya wale ambao hutenda dhambi mbaya sana.”

Shahidi mwenye kufanya uzinzi alitumika kwa muda gerezani na kulipa faini. Zaidi ya hiyo, alitengwa na ushirika kutoka kundi akiwa mtenda mabaya asiyetubu. Kitendo hicho kilimvutia chifu na kufunga midomo ya wale waliodhihaki Mashahidi wa Yehova. Chifu huyo alisema hivi: “Msinene vibaya juu ya Mashahidi wa Yehova. Wao ndio wenye kweli. Kitendo kama hicho hakichukuliwi na dini nyingine.”

Mashahidi waaminifu katika bara hilo hufuata himizo la Zaburi 37:3: “Umtumaini BWANA [Yehova, NW] ukatende mema, ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu.” Je! sisi tutamtumaini Yehova kama Wakristo hao wanavyofanya?y

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki