Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 4/15 kur. 15-20
  • Fanya Yehova Awe Itibari Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fanya Yehova Awe Itibari Yako
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uko Wapi Ule Upendo wa Kidugu?
  • Kuokoka kwa Kuitibari Katika Yehova
  • Wakati Ujao Mwangavu
  • Yehova Hutegemeza Watumishi Wake
  • Mtumaini Yehova kwa Moyo Wako Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • “Ee Yehova, . . . Nimekutegemea Wewe”
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
  • Kuwatumaini Wengine Ni Muhimu kwa Maisha Yenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Unaweza Kuwatumaini Ndugu Zako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 4/15 kur. 15-20

Fanya Yehova Awe Itibari Yako

“Itibari katika Yehova na ufanye mema;... uwe na upendezo mzuri sana katika Yehova.”​—ZABURI 37:3,4, NW.

1, 2. (a) Ni jambo gani lililotukia kwa wale ambao hawakuitibari katika Yehova katika karne ya kwanza, na kwa wale ambao waliitibari? (b) Ni maswali gani ambayo huenda yakaulizwa juu ya dini katika wakati wetu?

KATIKA karne ya kwanza ya Wakati wa Kawaida wetu, viongozi wa kidini Wayahudi walidai kuwa waliabudu Mungu. Lakini wao hawakuitibari katika yeye. Wao walivunja amri zake na kunyanyasa wawakilishi wake. (Mathayo 15:3; Yohana 15:20) Tokeo ni kwamba, ‘nyumba yao iliachiwa hali ya ukiwa’ na Yehova. (Mathayo 23:38) Katika 70 W.K., majeshi ya Kiroma yaliteketeza Yerusalemu na hekalu lao, kukiwa na upotezo mkubwa wa uhai kwa viongozi wa kidini na wafuasi wao. Lakini wale ambao waliitibari katika Yehova walipewa himaya, kwa maana walikuwa wametii maonyo ya wanenaji wake na kukimbilia usalama.​—Mathayo 24:15-22; Luka 21:20-24.

2 Katika hizi siku za mwisho za mfumo huu wa mambo, je! dini za ulimwengu huu zinaitibari katika Mungu wa kweli, Yehova? Je! zinatii amri zake na kutenda mapenzi yake, au zinaiga viongozi wa kidini wa karne ya kwanza ambao Mungu aliachia hali ya ukiwa? Ni zipi kati ya dini za leo ambazo zinaweza kutazamia kupewa himaya na Yehova kwa sababu ‘zinaitibari katika Yehova na kutenda mema’?​—Zaburi 37:3, NW.

Uko Wapi Ule Upendo wa Kidugu?

3. Kwa sababu gani jitihada za kidini kuleta amani zimeshindwa?

3 Hivi majuzi, Papa John Paul wa 2 alionya kwamba “wanadamu wote walielekeana na matisho makubwa kuhusu kuokoka kwao.” Yeye alikazia kwamba “matisho hayo yangezuiwa kwa njia nzuri zaidi kupitia jitihada za ushirika miongoni mwa vikundi mbalimbali vya kidini.” Ni mapenzi ya Mungu, yeye akasema, kwamba viongozi wa kidini ‘wafanye kazi pamoja’ ili walete “amani na mapatano.” Hata hivyo, ikiwa hayo ni mapenzi ya Mungu, basi mbona Mungu hajabariki jitihada ambazo zimefanywa muda wa karne hizo kuelekea jambo hilo? Yeye hajafanya hivyo kwa sababu dini hizi hazijaitibari katika njia ya Mungu ya kuleta amani kupitia Ufalme wake wa kimbingu. (Mathayo 6:9, 10) Badala yake, wao wametegemeza siasa na vita vya mataifa. Tokeo ni kwamba, katika wakati wa vita, wanadini wa taifa moja wameua wanadini wa taifa jingine, hata kuua watu wa dini yao wenyewe. Mkatoliki ameua Mkatoliki, Mprotestanti ameua Mprotestanti, na dini nyingine zimefanya hivyo hivyo. Lakini je! ndugu za kiroho walio wa kweli wanauana huku wakidai kuwa wanatumikia Mungu?

4. Yesu alisema ni nini kiwango kwa dini ya kweli, na kwa sababu gani hiyo ilikuwa “amri mpya”?

4 Yesu aliweka kiwango kwa dini ya kweli alipoambia wafuasi wake hivi: “Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.” (Yohana 13:34, 35) Kwa hiyo wale wanaozoea dini ya kweli lazima wapendane wao kwa wao. Hii ilikuwa “amri mpya” kwa sababu Yesu alisema: “Kama vile nilivyowapenda ninyi, . . . mpendane vivyo hivyo.” Yeye alikuwa na nia ya kutoa uhai wake kwa ajili ya wafuasi wake. Lazima wao wawe na nia ya kufanya hivyo hivyo—hapa. na, si kuchukua uhai wa waitikadi wenzao bali kutoa uhai wao wenyewe ikihitajiwa kabisa. Hilo lilikuwa jambo jipya, kwa maana halikuwa limetakwa na Sheria ya Musa.

5. Ni jinsi gani Neno la Mungu linavyokazia kwa kani nyingi uhitaji wa upendo na umoja miongoni mwa waabudu wake wa kweli?

5 Neno la Mungu linataarifu hivi: “Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona. Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.” (1 Yohana 4:20, 21) Kwa upendo huu, wale wanaoitibari katika Yehova wanadumisha umoja wa kweli wa kimataifa. Mtume Paulo anasema hivi kwenye 1 Wakorintho 1:10: “Basi ndugu nawasihi, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mnene mamoja; wala pasiwe kwenu faraka, bali mhitimu katika nia moja na shauri moja.”​—Ona pia 1 Yohana 3:10-12.

6. Kwa sababu gani Mashahidi wa Yehova wanaweza kusema kwamba wao ‘hawana hatia kwa damu ya mtu awaye yote’?

6 The World Book Encyclopedia chasema kwamba watu milioni 55 waliuawa katika Vita ya Ulimwengu ya Pili. Wao waliuawa na watu wa kila dini iliyo kubwa isipokuwa Mashahidi wa Yehova. Hakuna hata kimoja cha vifo hivyo ambacho kilisababishwa na shahidi wa Yehova, kwa kuwa wao walitii amri ya kupendana na wakakataa kuhusika katika vita vya mataifa. Ingawa mashahidi wengi waliuawa kwa sababu ya msimamo wao wa kutokuwamo, wao wangeweza kusema kama alivyofanya mtume Paulo: “Mimi sina hatia kwa damu ya mtu awaye yote.”​—Matendo 20:26.

7, 8. Ni jinsi gani wanakanisa fulani wanavyokiri hatia yao ya damu?

7 Hivi majuzi kasisi Mkatoliki aliyekuwa akitumikia wanajeshi wa angani walioangusha makombora ya atomi juu ya Japani katika 1945 alitaarifu hivi: “Kwa miaka 1,700 iliyopita kanisa limekuwa likifanya vita iwe yenye kustahika. Limekuwa likishawishi watu waitikadi kwamba ni kazi ya Kikristo inayoheshimika. Jambo hilo si kweli. Sisi tumesafishwa ubongo. . . . Ile gospeli ya Vita ya Haki ni gospeli ambayo Yesu hakufundisha kamwe. Hakuna jambo lo lote katika maisha au fundisho la Yesu ambalo linaweza kudokeza kwamba ingawa ni jambo lisilo halali kuchoma watu kwa baruti ya nyukilia mpaka wawe majivu, ni jambo halali kuchoma watu kwa kumimina petroli inayowaka moto au kwa kutumia silaha inayomimina miali ya moto.”

8 Catholic Herald ya London ilitaarifu hivi: “Wakristo wa kwanza . . . walilifuata neno Lake Yesu na wakakataa kuandikwa katika jeshi la Kiroma hata kama adhabu ilikuwa kifo. Je! historia yote ingekuwa tofauti kama kanisa lingeshikilia msimamo walo wa kwanza? . . . Ikiwa makanisa ya leo yangelaumu vita kwa kushirikiana, jambo ambalo lingemaanisha kwamba kila mshiriki angefungwa na dhamiri yake awe mkataa vita kama Wakristo hao, huenda amani ikahakikishwa kweli kweli. Lakini tunajua kwamba jambo hilo halitatukia kamwe.”

9 Kwa sababu gani sisi tunakata shauri kwamba Yehova ameziachia ukiwa dini za ulimwengu huu?

9 Hivyo, dini za ulimwengu zimejiletea msiba kwa kuacha msimamo wa kufuata sheria za Mungu. Wao wanafanya sawasawa tu na walivyofanya Mafarisayo kwa kutomwitibari. “Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai.” (Tito 1:16) Tokeo ni kwamba, Mungu ameziachia ukiwa dini za ulimwengu huu kama vile kwa uhakika alivyoiachia ukiwa dini ya kinafiki ya Wayahudi katika karne ya kwanza.​—Mathayo 15:9, 14.

Kuokoka kwa Kuitibari Katika Yehova

10, 11. Mfalme Hezekia alifanya nini wakati Ashuru ilipodai Yerusalemu usalimu amri kwa ushinde, na mnenaji wa Senakeribu alikuwa akidhihaki nani vikali?

10 Usitie itibari yako katika matatuzi ya kibinadamu kwa matatizo ya ulimwengu huu. Badala ya hivyo, mwitibari yule Mmoja ambaye anaweza kutimiza ahadi zake. (Yoshua 23:14) Kama kielelezo, angalia lililotukia katika karne ya nane kabla ya Kristo, katika siku za Mfalme Hezekia wa Yuda. Biblia inasema hivi juu yake: “Yeye aliendelea kufanya yaliyokuwa ya kufaa katika macho ya Yehova.” (2 Wafalme 18:3, NW) Wakati wa utawala wake, ile serikali kubwa ya ulimwengu ya Ashuru yenye uweza ilikuja dhidi ya Yerusalemu. Mnenaji wa mfalme Mwashuri Senakeribu alidai kwamba Yerusalemu usalimu amri kwa ushinde, akisema: “Hivi ndivyo mfalme amesema, ‘Msiache Hezekia adanganye ninyi watu, kwa maana yeye hawezi kukomboa ninyi kutoka mkono wangu. Na msiache Hezekia asababishe ninyi kuitibari katika Yehova.’”​—2 Wafalme 18:29,30, NW.

11 Hezekia alifanya nini? Biblia inataarifu hivi: “Hezekia akaanza kusali mbele za Yehova na kusema: ‘O Yehova Mungu wa Israeli, unayeketi juu ya makerubi, wewe peke yako ndiwe Mungu wa kweli wa falme zote za dunia. Wewe mwenyewe umezifanya mbingu na dunia. Inamiza sikio lako, O Yehova, na usikie. Fungua macho yako, O Yehova, na uone, na usikie maneno ya Senakeribu ambayo amepeleka kudhihaki vikali Mungu aliye hai. . . . O Yehova Mungu wetu, tuokoe, tafadhali, kutoka mkono wake, kwamba falme zote za dunia zipate kujua kwamba wewe, O Yehova, ndiwe Mungu peke yako.’”​—2 Wafalme 19:15-19, NW.

12. Yehova alijibu sala ya Hezekia jinsi gani?

12 Yehova alisikia sala hiyo na akapeleka nabii Isaya akaambie Hezekia: “Hivi ndivyo Yehova amesema kuhusu mfalme wa Ashuru: ‘Yeye hatakuja ndani ya jiji hili wala yeye hatapiga mshale humo wala kuukabili kwa ngao wala kukupusha boma la mazingiwa dhidi yalo.’ “Je! Hezekia alipaswa kupinga Ashuru kwa kutumia jeshi? Hapana, yeye alipaswa kuitibari katika Yehova, na alifanya hivyo. Tokeo lilikuwa nini? “Malaika wa Yehova aliendelea na kwenda nje na kudhurubu chini mia moja themanini na tano elfu katika kambi ya Waashuri.” Senakeribu mwenyewe alilipa kwa kudhihaki vikali Yehova na watumishi wa Yehova, kwa maana wanaye mwenyewe walimuua. Kulingana na neno la Yehova, hakuna hata silaha moja iliyokuja dhidi ya Yerusalemu.​—2 Wafalme 19:32-37, NW.

13, 14. Ni juu ya msingi gani watu wa kutoka mataifa yote wataokoka mwisho wa mfumo wa mambo uliopo?

13 Katika siku yetu jambo la hali moja na hilo litatukia. Wale wanaoitibari katika Yehova wataokoka dhihaka kali za ulimwengu huu na mwisho wa ulimwengu huu. “Wale wanaojua jina lako wataitibari katika wewe, kwa maana wewe kwa uhakika hutaacha wale wanaokutafuta wewe, O Yehova.” (Zaburi 9:10, NW) Lakini kabla Yehova hajafisha ulimwengu huu wenye hatia ya damu, yeye anaalika wenye moyo wa kufuata haki wamjie yeye kupata usalama. Hao wanakuwa ndio “mkutano mkubwa” kutoka mataifa yote, ambao “wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu.” Wao wanaokoka mwisho wa mfumo huu kwa sababu wanaitibari katika Yehova na kutumikia yeye “mchana na usiku.”​—Ufunuo 7:9-15.

14 Hawa wanajibu mwito ambao sasa unaenda nje ukiwa na kani iliyoongezeka ulimwenguni pote, kama ilivyotabiriwa kwenye Isaya 2:2, 3, NW: “Na lazima itukie katika sehemu ya mwisho ya zile siku kwamba mlima wa nyumba ya Yehova [ibada yake ya kweli] utakuwa uliosimamishwa kwa uthabiti . . . jamii nyingi za watu kwa uhakika zitaenda na kusema: ‘Njoni, ninyi watu, na acheni twende juu kwenye mlima wa Yehova, . . . na yeye atatuagiza juu ya njia zake, na sisi tutatembea katika vijia vyake.’” Mstari wa 4 unasema: “Na wao watapaswa kufua panga zao ziwe majembe ya plau na mikuki yao iwe makasi ya kupogolea. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa, wala wao hawatajifunza vita tena.”

15. Ni nani wanaotimiza unabii wa Isaya 2:2-4, na jinsi gani?

15 Ni nani, katika wakati wetu, ambao ‘wanageuza panga zao ziwe majembe ya plau’? Ni nani ambao ‘hawajifunzi vita tena’? Ni nani ambao wana upendo usiovunjika kwa ajili ya ndugu na dada zao wa kiroho katika sehemu zote za dunia na wana umoja pamoja nao? Ni nani ambao wanaitibari kweli kweli katika Yehova na kualika wengine wafanye hivyo hivyo? Mambo ya uhakika ya wakati wetu yanaonyesha kwamba jibu linaweza kuwa tu: Mashahidi wa Yehova. Wao, kama Hezekia, wanaitibari katika Yehova kwa moyo wao wote na kuonyesha hivyo kwa kushika amri zake.

Wakati Ujao Mwangavu

16, 17. Ni wakati ujao gani ulio mwangavu ambao Yehova anatolea wale wanaoitibari katika yeye?

16 Kwa wale ambao wanaitibari katika yeye, Yehova anatoa wakati ujao ulio mwangavu kuliko nyakati zote zinazoweza kuwaziwa, wakati atakapobadilisha jamii ya ulimwengu wa zamani kwa kuweka yake iliyo mpya. Katika ule ulimwengu mpya hapa duniani, hakutakuwa na hofu wala kutoitibariana, wala umaskini, ukosefu wa haki, wala uhalifu. Watu hawatauawa tena katika vita au kwa kutolewa mimba. Ufunuo 21:4 hata unaahidi kwamba “mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena.”

17 Baada ya muda fulani, dunia itakuwa paradiso kama Yesu alivyoahidi. (Luka 23:43, ZSB) Na kwa kuwa hata kifo kitaondolewa kabisa, wale wanaoitibari katika Yehova wataweza kuishi milele katika Paradiso. Itakayotimizwa kabisa ni Mika 4:4: “Bali wataketi kila mtu chini ya mzabibu wake, na chini ya mtini wake; wala hapana mtu atakayewatia hofu.” Ebu wazia kuishi katika jamii ambamo kila mtu unayekutana naye ni mtu unayeweza kuitibari! Kwa sababu gani itakuwa hivyo? Kwa sababu, kama Isaya 54:13 inavyosema: “Watoto wako wote watafundishwa na BWANA [Yehova, NW]; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi.”

18. Ni manufaa gani ambazo wale wanaoitibari katika Yehova wanavuna hata sasa?

18 Lakini, hata sasa mamilioni ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote wanavuna manufaa kwa kuitibari katika Yehova. Mathalani, kwa sababu ya kutii sheria na kanuni za Yehova, watumishi wa Yehova wako huru na kansa ya mapafu inayosababishwa na kuvuta tumbako. Kwa sababu ya kuishi katika mazingira yenye usafi kiadili, kwa ujumla wao hawahatarishwi na ambukizo kubwa la ulimwenguni pote la magonjwa yanayopitishwa kwa kufanya ngono, kutia na UKIMWI. Kutotumia vibaya dawa za kulevya kunawalinda dhidi ya magonjwa yenye kuharibu ubongo na yenye kufisha ambayo watu wengi wanaotumia vibaya dawa za kulevya wanayo. Na kwa kuwa wao hawatiwi damu mishipani, hawapatwi na magonjwa mengi yenye kufisha yanayoambukizwa kupitia damu, kutia na ugonjwa wa kufura ini, unaoua au kuwatia dhara la daima wapokeaji elfu kumi wa damu kila mwaka katika United States tu.

19. Ni jinsi gani Yehova atakavyoponyosha wale wanaomtukia hata wakifa sasa?

19 Hata ikiwa watu fulani kati ya wale wanaoitibari sasa katika Yehova watapaswa kufa kwa sababu ya uzee, ugonjwa, au aksidenti, Yehova atawaponyosha. Atawarudisha kwa njia ya ufufuo. Hivyo, mtume Paulo alitutia moyo ‘tuwe na itibari yetu, si katika sisi wenyewe, bali katika Mungu ambaye huinua wafu.’​—2 Wakorintho 1:9, NW.

Yehova Hutegemeza Watumishi Wake

20, 21. (a) Ni upinzani gani ambao sisi tunaweza kutazamia, kama inavyothibitiwa na lililotukia kwa Yesu? (b) Ni jinsi gani Yehova anavyothibitisha watu wake kuwa ni wa kweli, kama alivyofanyia Yesu?

20 Kumbuka kwamba “ulimwengu mzima umo katika uwezo wa yule mwovu,” Shetani Ibilisi. (1 Yohana 5:19, NW) Kwa hiyo ikiwa wewe unaitibari katika Mungu, utapingwa na Shetani na ulimwengu wake. Wao watajaribu kuharibu itibari yako kwa dhihaka au mnyanyaso, kama ilivyokuwa kwa habari ya Yesu. Baada ya yeye kupigiliwa misumari kwenye mti wa mateso, “wapita-njiani walianza kunena juu yake kwa kutukana, wakitikisa-tikisa vichwa vyao na kusema: . . . ‘Kama wewe ni mwana wa Mungu, shuka chini kutoka mti wa mateso!’ Kwa jinsi ile ile wakuu wa makuhani pia pamoja na waandishi na wanaume wazee wakaanza kumfanyia mzaha na kusema: ‘Wengine aliokoa; yeye mwenyewe hawezi kujiokoa!’ . . . Yeye ameweka itibari yake katika Mungu; acha Huyo amponyoshe sasa ikiwa Yeye anamtaka.’”​—Mathayo 27:39-43, NW.

21 Siku tatu baadaye, Mungu hakika alimponyosha Yesu kwa kumfufua kutoka kwa wafu. Hata hivyo, kizazi hicho cha wafanya mzaha kiliuawa au kikatiwa utumwani na majeshi ya Kiroma. Kwa kuwa Kristo aliye Mfalme wa Ufalme wa kimbingu ndiye atasimamia ufufuo, ikiwa wafanya mzaha hao watarudi kutoka kwa wafu, watalazimika kujinyenyekeza chini ya Yule waliyemfanyia mzaha miaka elfu mbili iliyopita! Ndiyo, Yehova anawathibitisha watumishi wake kuwa ni wa kweli, ambao wanasema: “Mimi nimetia itibari yangu katika Mungu. Mimi sitaogopa. Mwanadamu wa dunia anaweza kunitenda nini?” —Zaburi 56:11, NW.

22. Yehova anatangaza nini kuhusu wale wanaoitibari katika yeye, na wale wasiofanya hivyo?

22 Kuhusu watumishi wake, Yehova anatangaza hivi: “Mbarikiwa ni mwanamume kakawana ambaye anatia itibari yake katika Yehova, na ambaye Yehova amekuwa uhakika wake. Na yeye kwa uhakika atakuwa kama mti uliopandwa kandokando ya mafungu ya maji, ambao unapeleka nje mizizi yao pa]e pale kandokando ya mtaro wa maji; na yeye hataona wakati joto linapokuja, bali majani yake kwa kweli yatathibitika kuwa yenye kusitawi sana. Na katika mwaka wa ukame yeye hatakuwa mwenye sumbuko, wala yeye hatafanya likizo la kuacha kutokeza tunda.” Lakini Yehova anatangaza hivi pia: “Mlaaniwa ni mwanamume kakawana ye yote ambaye anatia itibari yake katika mwanadamu wa dunia na kwa kweli anafanya mkono wake uwe wa mnofu, na ambaye moyo wake unageukia mbali kutoka kwa Yehova mwenyewe. Na yeye kwa uhakika atakuwa kama mti wa upweke katika uwanda wa jangwa naye hataona wakati mema yajapo.”​—Yeremia 17 5-8, NW.

23. Ni lazima tufanye nini ikiwa tunataka uhai wa milele?

23 Hivyo, katika nyakati hizi za hatari, “itibari katika Yehova na ufanye mema; kaa katika dunia, na ushughulike pamoja na uaminifu. Pia uwe na upendezo mzuri sana katika Yehova, na yeye atakupa wewe maombi ya moyo wako.” (Zaburi 37:3, 4, AW) Maombi yako yenye kutimizwa na yatie ndani ile zawadi ya uhai wa milele katika ulimwengu mpya wenye uadilifu, ulioahidiwa na Mungu tunayeitibari.

Maswali kwa Ajili ya Kupitia

◻ Ni kiwango gani ambacho lazima kishikwe na wale wanaoitibari katika Yehova?

◻ Je! dini za ulimwengu huu zinafunza itibari katika Yehova?

◻ Itibari ya Mfalme Hezekia ilithibitishwa kuwa kweli jinsi gani?

◻ Katika siku yetu, unabii wa Isaya 2:2-4 unatimizwa jinsi gani?

◻ Ni wakati ujao gani utapatwa na wale wanaoitibari katika Yehova?

[Picha katika ukurasa wa 17]

Mnenaji wa mfalme wa Ashuru alimdhihaki vikali Yehova na kudai Yerusalemu usalimu amri kwa ushinde

[Picha katika ukurasa wa 18]

Katika ulimwengu mpya, wale wanaoitibari katika Yehova watafurahia amani na usalama kamili

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki