Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 4/15 uku. 21
  • Kujua Yaliyo Katika Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujua Yaliyo Katika Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jeuri Iliyotabiriwa
  • Kuilipa Bei
  • “Mwanadamu wa Kwanza Alikuwa Mwanadamu”
  • Nyumba Iliyogawanyika—Jinsi Talaka Inavyowaathiri Vijana
    Amkeni!—2009
  • Kumwamini Mungu—Je! Kunatosha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Tembea Kama Ufundishwavyo na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • ‘Nyakati Zetu za Hatari’—Jamaa Yako Inahusikaje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 4/15 uku. 21

Kujua Yaliyo Katika Habari

Jeuri Iliyotabiriwa

“Vijana-wabalehe wanakuwa wenye jeuri zaidi ya walivyokuwa miaka iliyopita,” anataarifu James Fox, mchunguzi wa matendo ya uhalifu kwenye Chuo Kikuu cha Northeastern. “Mimi naona badiliko halisi katika namna ya kijana tunayekuwa naye,” anataarifu Faye Harrison, hakimu mmoja wa Michigan. “Aliye mgumu zaidi, mwepesi zaidi (kutenda jeuri), mwenye kuhusika kwa kina kirefu zaidi katika kutotii wakati wa umri wa mapema zaidi.” Kwa uhakika, vijana-matineja wenye kasirani kali ndio “wenye kusababisha visa 300 kwa mwaka vya wazazi kuuawa na vijana-wabalehe,” linaripoti Detroit Free Press.

Kwa sababu gani kuna ongezeko la jeuri miongoni mwa vijana wa leo? Fox anataja kuweza kupata silaha kwa urahisi zaidi, jeuri ya televisheni, na “kwa ujumla, upungufu wa kustahi mamlaka,” kulingana na USA Today. Akikaza fikira juu ya wazazi, David Ramirez, hakimu mmoja wa Denver, anaitikadi kwamba “maadili ya kimapokeo na mawazo ya staha hayapitishwi kwa watoto, na inaonekana wazazi wengi wana ukosefu wa kujikabidhi kwa vijana wao,” linataarifu The Denver Post.

Yaliyo ya wakati unaofaa kabisa ni maneno yaliyoandikwa na mtume Paulo wakati, karne nyingi zilizopita, alipotabiri “kwamba katika siku za mwisho nyakati za hatari zilizo ngumu kupambana nazo zitakuwa hapa. Kwa maana watu watakuwa wajipenda wenyewe, wapenda fedha, wenye kimbelembele, . . . wasiotii wazazi, .wasio na shauku ya asili,... bila kujiweza, wakali, bila upendo wa wema.” (2 Timotheo 3:1-3, NW) Wakristo wanaweza kujilinda dhidi ya mielekeo kama hiyo kwa kujenga mahusiano yenye upendo ya kijamaa, kama inavyoonyeshwa katika vifungu vya Biblia kama Kumbukumbu 6:4-9 na Wakolosai 3:12-14, 18-21.

Kuilipa Bei

“Sisi hatuisomi Biblia na hatujui yaliyomo,” anasema George Gallup, Jr., Mwamerika mtafuta maoni ya watu. “Sisi tunalipia jambo hilo na kutaabika katika kadiri ya talaka, kutendwa vibaya kwa watoto, matumizi mabaya ya dawa za kulevya, na kupunja na kukosa ufuataji haki katika viwango vyote vya jamii ya watu.” Kulingana na uchunguzi huo wa Gallup wa maoni ya watu, asilimia 40 ya Waamerika wanakuwa kanisani Jumapili na yapata asilimia 80 wanafunga ndoa kanisani, hata hivyo kadiri ya talaka imeongezeka mara tatu tangu 1960, hesabu ya wenzi wenye kuishi pamoja bila kufunga ndoa imeongezeka karibu mara tano, na kuzaa watoto haramu kumeongezeka karibu mara nne. Utoaji mimba uliongezeka mara tatu kati ya 1972 na 1979.

Akionyesha wazi kabisa shina la tatizo lenyewe, Gallup alionelea hivi: “Kwa uwazi makanisa hayapenyi mpaka kwenye msingi wa kukaza maadili kikiki. Sisi tunaishi kwa kufuata dini kijuu-juu sana. Hiyo haigeuzi maisha na kutoa upya mwelekezo. Wala hiyo haina msingi wa kibiblia.”

Hata hivyo Ukristo unapaswa kuwa wenye kugeuza maisha, kutoa upya mwelekezo na kutegemea msingi wa Biblia. Hapo awali ulikuwa hivyo. Wakristo wa mapema walifundishwa ‘kuondolea mbali utu wa zamani.’ Paulo aliandika hivi: “Wala waasherati, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wanaume wanaotunzwa kwa makusudi yasiyo ya asili, wala wanaume wanaolala na wanaume, wala wevi, wala watu wenye pupa . . . hawatarithi ufalme wa Mungu. Na hali hivyo ndivyo baadhi ya ninyi mlikuwa.”​—Waefeso 4:22; 1 Wakorintho 6:9-11, NW.

“Mwanadamu wa Kwanza Alikuwa Mwanadamu”

Wanamageuzi fulani wanadai kwamba mageuzi yanaitikadika kwa “asilimia ya mia kwa mia” na kwamba hiyo ni “nadharia ambayo mtu anaweza kuthibitisha katika maabara.” Lakini kwenye Kongamano la Pili la Kimataifa la Uchunguzi wa Visukuku vya Kibinadamu, lililofanywa hivi majuzi huko Turin, Italia, ilikuwa wazi kwamba bado wanasayansi wengi wana mashaka-mashaka juu ya jambo hilo.

Badala ya kuhakikisha kwamba mageuzi yanaitikadika kwa “asilimia ya mia kwa mia,” inaonekana kongamano hilo lilifichua mitofautiano mikubwa ya maoni kati ya wanasayansi kuhusu ni wakati gani na jinsi gani mwanadamu aligeuka-geuka. Mathalani, Mchunguzi wa Visukuku vya Kibinadamu, Bernard Vandermeersch, alikazia uhakika wa kwamba, kwa kadiri ambavyo asili za mwanadamu zinahusika, matokeo ya uchunguzi wa visukuku “yanapinganisha mambo ya uhakika yanatokezwa na tabia za urithi,” ambazo zinaonyesha kulikuwa na mzazi mmoja wa kale.

Hata hivyo, mipinganisho hiyo inapatikana miongoni tu mwa watu wanaoshindwa kukubali ule ukweli rahisi wa kwamba Mungu “alifanya kutoka katika mtu mmoja kila taifa la wanadamu, wapate kukaa juu ya uso wote wa dunia.” (Matendo 17:26, NW) Alifanya hivyo jinsi gani? Mwanzo 2:7 unatuambia kwamba “Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai,” akisababisha mwanadamu awe “nafsi hai.”

Haishangazi kwamba, mwana-bayolojia Giuseppe Sermonti, akieleza juu ya mashauri yaliyokatwa na kongamano hilo, alikiri kwamba “majaribio yote ya kufanya iwe kwamba sisi ni masokwe-watu walioshuka kwenye miti hayajatokeza matokeo yo yote ya kupendeza. Mwanadamu wa kwanza alikuwa mwanadamu.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki