Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 8/15 kur. 3-4
  • Kusema Katika Ndimi —Tukio Linaloongezeka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kusema Katika Ndimi —Tukio Linaloongezeka
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Kuna Ile Tamaa Leo ya Kupata Zawadi ya Ndimi?
  • Mtu Hupatwa na Nini?
  • Kusema kwa Lugha
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Kusema kwa Lugha?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Je! Zawadi ya Ndimi Ni Sehemu ya Ukristo wa Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Je! Kusema Katika Lugha Leo—Kunatoka kwa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 8/15 kur. 3-4

Kusema Katika Ndimi —Tukio Linaloongezeka

“NGUVU fulani ilikuwa imedhibiti ulimi wangu na maneno yalitiririka tu kama maji. Lilikuwa jambo la shangwe kama nini! Kulikuwako hisia ya usafi mwingi mno. Nimebadilika kabisa tangu wakati huo,” asema mtu mmoja aliyekuwa na lile ono lisilo la kawaida la kusema katika “ulimi usiojulikana.”

Hapo una ufafanuzi wa mtu kuhusu ono lake la kwanza la kusema katika “ulimi usiojulikana.” ‘Lakini hilo ni nini?’ wengine huenda wakauliza kwa kufaa. Hilo linarejezea lile zoea au imani katika baadhi ya makanisa ambapo wanaume na wanawake hudai kuwa wao husukumwa na roho ya Mungu kusema katika lugha za kigeni au ambazo hawajui.

Hilo ni tukio linaloongezeka. Kusema katika ndimi kulikoonwa wakati mmoja kuwa jambo lililotukia kwa waamini wa Upentekoste tu, kumevuka mipaka ya mafarakano ya zamani kama vile Wabaptisti, Waepiskopali, Walutheri, Wamethodisti, Wapresbiteria, na Wakatoliki wa Kiroma. Hali ya mtu akiwa anasema katika ndimi imeelezwa kuwa yenye msisimuko mwingi, yenye kichaa, ya kuona njozi, na iliyo kama usingizi. Kuna hali ya kifumbo na yenye uvutio mwingi inayoshirikishwa na kusema katika ndimi, au lugha.

Kwa Nini Kuna Ile Tamaa Leo ya Kupata Zawadi ya Ndimi?

Katika kitabu chake Tongues of the Spirit, Cyril G. Williams hudokeza kwamba huenda kukawa na “uhusiano kati ya hisia ya kutofaulu, na tamaa ya kusema katika ‘ndimi.’” Yeye hueleza jambo hilo kuwa njia ya kuondosha hisia mbaya iliyo na “thamani ya kitiba ikiwa yenye kupunguza mkazo” na “yenye kusuluhisha mapingano ya kindani.” Fadhaiko katika kazi ya kanisa, mikazo ya kihisiamoyo, kutofaulu katika kazi-maisha fulani, kufiwa, mikazo ya nyumbani, au ugonjwa katika familia vinatajwa kuwa visababishi vinavyochangia usemi huo wenye msisimuko mwingi.

Vivyo hivyo, katika The Psychology of Speaking in Tongues, John P. Kildahl husema kwamba “hangaiko ni jambo linalohitajiwa ili kusitawisha uwezo wa kusema katika ndimi.” Kupitia uchunguzi wa kibinafsi na mahoji ya uangalifu, ilipatikana kwamba “zaidi ya asilimia 85 ya wale wasemao katika ndimi wamepatwa na taabu dhahiri yenye kuhangaisha kabla ya kusema katika ndimi.” Kwa mfano, mama mmoja alitaka kusema katika ndimi ili aweze kumwombea mwana wake aliyekuwa na ugonjwa wa kansa. Mwanamume mmoja alianza kusema katika ndimi wakati wa kipindi ambacho alikuwa akisitasita kufanya uamuzi juu ya toleo la kupandishwa cheo kazini. Mwanamke mmoja alianza kusema katika ndimi katika juma moja baada ya mume wake kujiunga na shirika linalowasaidia walevi.

Mtu Hupatwa na Nini?

Mtu mwingine aliyekuwa amesema katika ndimi kwa mara ya kwanza aliripoti hivi: “Nilihisi kuwashwa kotekote mwilini, na kuhisi baridi na kutokwa jasho sana, kutetemeka na kudhoofika viungoni.” Mara nyingi kunakuwako tabia isiyo ya kawaida inayowaudhi wengine, ambayo hushirikishwa na ono la kusema katika ndimi. Kwa mfano, “msichana mmoja alikuwa karibu anyongwe kwa mate yake mwenyewe alipojinyoosha kwenye kiti, shingo yake ikiwa imeegama kwenye sehemu ya nyuma ya kiti, visigino vyake vikiwa sakafuni, miguu yake ikiwa migumu.” Wakati wa mkutano wa kundi moja “mwanamume mmoja alipindukapinduka kutoka upande mmoja wa kanisa hadi mwingine.”

“Kwa wengine,” aandika Profesa William J. Samarin, “kusema katika ndimi ni wonyesho wa kuwa na ubatizo katika Roho Takatifu.” Bila hilo “wao hufanywa wahisi kutokuwa kamili.” Kunaonwa pia “kuwa jibu la sala, uhakikisho wa upendo na kibali cha kimungu.” Wengine wamesema kwamba inawaacha wakiwa na hisia ya upatani wa kindani, shangwe, na amani, na wakiwa na “hisia ya kuwa na nguvu nyingi zaidi” na “hisia ya kutambuliwa yenye nguvu zaidi.”

Je! usemi wenye msisimuko mwingi kwa kweli ni ushuhuda wa utendaji wa roho takatifu? Je! ono hilo humtambulisha mtu kuwa Mkristo wa kweli? Je! kusema katika ndimi ni sehemu ya ibada inayokubaliwa leo? Maswali hayo yanastahili zaidi ya jibu la kijuujuu tu. Kwa nini? Kwa sababu tunataka ibada yetu iwe na kibali na baraka ya Mungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki