Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 12/15 kur. 8-10
  • “Tafuteni Yehova, Ninyi Nyote Wasikivu”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Tafuteni Yehova, Ninyi Nyote Wasikivu”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Tutafute Usikivu?
  • Wale ‘Watafutao Usikivu’ Leo
  • Itikia kwa Usikivu
  • Tafuta Upole Umpendeze Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Kuendelea Kuwa na Kibali cha Mungu Hali Zinapobadilika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Mtafute Yehova Kabla ya Siku Yake ya Hasira
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
  • Mtafuteni Yehova Kabla ya Siku Yake ya Hasira
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 12/15 kur. 8-10

“Tafuteni Yehova, Ninyi Nyote Wasikivu”

“TAFUTENI Yehova, ninyi nyote wasikivu wa dunia, ambao mmezoea kufanya uamuzi wa hukumu Wake mwenyewe. Tafuteni uadilifu, tafuteni usikivu. Inaelekea huenda mkafichwa katika siku ya kasirani ya Yehova.”—Sefania 2:3, NW.

Nabii Sefania alielekeza maneno hayo kwa “wasikivu wa dunia,” na aliwahimiza ‘watafute usikivu’ ili walindwe katika “siku ya kasirani ya Yehova.” Hilo haliachi shaka lolote kwamba usikivu ni takwa linalohitajiwa ili kupata wokovu. Lakini kwa nini?

Kwa Nini Tutafute Usikivu?

Usikivu ni sifa ya kuwa mwenye hali ya upole, bila kiburi au kujiona. Unahusiana kwa ukaribu na sifa nyinginezo, kama vile unyenyekevu na upole. Kwa hiyo, watu wasikivu ni wenye kufundishika nao hukubali kwa utayari nidhamu itokayo mkononi mwa Mungu, hata ingawa huenda ikaonekana kuwa yenye kuhuzunisha kwa wakati huo.—Zaburi 25:9; Waebrania 12:4-11.

Usikivu wenyewe huenda usihusiane hata kidogo na elimu au cheo cha mtu maishani. Hata hivyo, wale wenye elimu ya juu au wenye mafanikio katika njia ya kilimwengu huelekea kuhisi kwamba wanastahili kujifanyia wenyewe maamuzi katika mambo yote, hata mambo yanayohusu ibada. Hilo laweza kuwazuia wasiruhusu mtu mwingine awafundishe jambo fulani au wasikubali shauri na kufanya mabadiliko ya lazima maishani mwao. Wengine walio matajiri kimwili huenda wakatumbukia katika hali ya kufikiri kimakosa kwamba usalama wao umo katika mali zao za kimwili. Kwa hiyo, hawahisi uhitaji wowote wa kupata utajiri wa kiroho kutoka katika Neno la Mungu, Biblia.—Mathayo 4:4; 5:3; 1 Timotheo 6:17.

Fikiria waandishi, Mafarisayo, na makuhani wakuu wa siku za Yesu. Katika pindi moja wakati wale maofisa waliotuma kumkamata Yesu waliporudi bila yeye, Mafarisayo walisema hivi: “Je! ninyi nanyi mmedanganyika? Ni nani katika wakuu amwaminiye, au katika Mafarisayo? Lakini makutano hawa wasioifahamu torati wamelaaniwa.” (Yohana 7:45-49) Yaani, kulingana nao, ni watu wasio na ujuzi na wasiopata elimu ambao wangekuwa wapumbavu vya kutosha kuwa na imani katika Yesu.

Hata hivyo, baadhi ya Mafarisayo walivutwa kwenye kweli, na hata walimtetea Yesu na Wakristo. Nikodemo na Gamalieli walikuwa miongoni mwa hao. (Yohana 7:50-52; Matendo 5:34-40) Baada ya kifo cha Yesu, “jamii kubwa ya makuhani wa[li]itii ile Imani.” (Matendo 6:7) Bila shaka kielelezo chenye kutokeza zaidi kilikuwa kile cha mtume Paulo. Yeye alielimishwa miguuni pa Gamalieli akawa wakili wa Dini ya Kiyahudi aliye stadi na mwenye kustahiwa sana. Hata hivyo, baadaye aliitikia kwa unyenyekevu wito wa Kristo Yesu akawa mfuasi wake mwenye bidii.—Matendo 22:3; 26:4, 5; Wagalatia 1:14-24; 1 Timotheo 1:12-16.

Hayo yote yaonyesha kwamba hata mtu awe na malezi gani au awe na hisi gani sasa juu ya ujumbe kutoka Biblia, maneno ya Sefania yangali yatumika. Ikiwa mtu ataka kukubaliwa na Mungu na kuongozwa na Neno lake, usikivu ni jambo la lazima.

Wale ‘Watafutao Usikivu’ Leo

Mamilioni ya watu kotekote ulimwenguni wanaitikia habari njema za Ufalme. Mashahidi wa Yehova wanaongoza mafunzo ya Biblia zaidi ya milioni nne kila juma katika nyumba za watu wa jinsi hiyo. Watu hao hutoka malezi mengi tofauti-tofauti na hali mbalimbali za kiuchumi na za kijamii. Lakini, jambo moja wanaloshiriki ni kwamba wana unyenyekevu kuweza kuukubali ujumbe wa Biblia ambao mtu fulani aliwatolea kwenye mlango wao wenyewe au kwingineko. Wengi wao wanafanya maendeleo mazuri kwa sababu wako tayari kujitahidi kushinda vizuizi vilivyo njiani mwao. Ndiyo, wamo miongoni mwa “wasikivu wa dunia” leo.

Chukua kielelezo cha Maria katika Meksiko. Yeye alijifunza uwakili kwenye chuo kikuu na alikuwa na usalama wa kifedha kwa sababu ya kurithi mali. Kwa sababu hiyo, alisitawisha mawazo fulani ya kujitegemea sana ambayo, kama alivyosema, yalimbadili, akawa mtu “mwasi, asiye na adabu, mfidhuli, na asiyeamini kuwako kwa Mungu. Nilianza kufikiri kwamba kila jambo lingeweza kusuluhishwa na fedha na kwamba Mungu hakuwa wa maana. Kwa kweli, nilihisi kwamba hata hakuwako,” Maria akakumbuka. “Kwangu kanisa lilikuwa jambo la kipumbavu na takwa la kijamii tu,” yeye akaongeza.

Baadaye, Maria aliona mabadiliko katika binamu yake baada ya yeye kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. “Alikuwa amekuwa mbaya sana, na sasa alikuwa mtu mwenye amani na mnyoofu sana,” Maria akaeleza. “Watu wa ukoo walisema kwamba alikuwa mhubiri na alisoma Biblia, na kwa sababu hiyo hakunywa kileo wala kufuatia wanawake tena. Kwa hiyo nilitaka aje anisomee Biblia kwa sababu nilifikiri kwamba kwa njia hiyo ningepata amani na utulivu nilizotaka sana.” Tokeo lilikuwa kwamba Maria alikubali funzo la Biblia pamoja na mume na mke Mashahidi.

Alikuwa na mambo mengi ya kushinda, na pia ilikuwa vigumu sana kwake kuikubali ile kanuni ya Biblia ya ukichwa ili awe katika ujitiisho kwa mume wake. Lakini alifanya mabadiliko makubwa katika maisha yake na katika mtazamo wake. Alikiri hivi: “Nafikiri kwamba tangu wakati ule akina ndugu walipotembelea nyumbani kwangu na kuleta pamoja nao msaada wa Yehova, kumekuwa na furaha, utulivu, na baraka ya Mungu zikikaa nyumbani mwangu.” Leo, Maria ni Shahidi wa Yehova aliyejiweka wakfu na kubatizwa.

Katika kufuatia ibada ya kweli, kuna sehemu nyingine ambayo katika hiyo usikivu, au ukosefu wao, unakuwa na daraka la maana. Mara nyingi sana, mke katika familia hukubali kweli na kutaka kumtumikia Mungu, lakini mume husitasita. Labda ni vigumu kwa waume fulani kukubali wazo la kwamba kuna mtu mwingine—Yehova Mungu—ambaye ni lazima wake zao wajitiishe kwake sasa. (1 Wakorintho 11:3) Mwanamke mmoja katika Chihuahua, Meksiko, aliomba funzo la Biblia, na hatimaye yeye na watoto wake saba walikubali kweli. Mwanzoni mume wake alipinga. Kwa nini? Kwa sababu hakutaka familia yake iende kuhubiri nyumba kwa nyumba, ikitoa fasihi ya Biblia. Yaonekana alihisi kwamba hilo lilikuwa ni kumvunjia heshima. Hata hivyo, familia yake ilisimama imara katika uamuzi wayo wa kumtumikia Mungu. Baadaye mume huyo alianza kuona thamani ya kukubali mpango wa Mungu. Lakini miaka 15 ilipita kabla ya yeye kujiweka wakfu kwa Yehova.

Kotekote Meksiko, bado kuna jumuiya nyingi zilizo mbali ambako wakazi wenyeji wana lugha na desturi zao za kienyeji za Kihindi. Ujumbe wa Biblia unawafikia watu hao na unawasaidia waboreshe kiwango cha maisha yao ya kitamaduni, wengine wanapojifunza kusoma na kuandika huku wakijifunza kweli. Hata hivyo, jambo la kwamba watu wana elimu ndogo au nyenzo chache za kimwili halimaanishi kwa lazima kwamba watakuwa wenye kuitikia zaidi. Kiburi kwa sababu ya rangi na kushikamana sana na mapokeo ya wazazi wa kale waliokufa nyakati nyingine hufanya iwe vigumu kwa wengine kuikubali kweli. Hilo pia hueleza ni kwa nini mara nyingi katika vijiji fulani vya Kihindi, wale wanaoikubali kweli husumbuliwa na wale wanakijiji wengine. Kwa hiyo usikivu una unamna-namna mwingi.

Itikia kwa Usikivu

Namna gani wewe binafsi? Je! unaitikia kweli ya Neno la Mungu? Au ni vigumu kwako kukubali kweli nyinginezo za Biblia? Labda ungetaka kujichunguza mwenyewe kuona lile linalokuzuia. Je! unahangaika kwa sababu watu wengi wanaovutwa kwenye kweli ni wenye malezi ya hali ya chini? Je! kiburi cha kibinafsi kingeweza kuwa chahusika katika kufikiri kwako? Ni vizuri kufikiria maneno haya ya mtume Paulo: “Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu; tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu.”—1 Wakorintho 1:27-29.

Je! ungekatalia mbali hazina kwa sababu tu uliipata katika chombo cha udongo chenye hali ya chini? Bila shaka la! Lakini, hiyo ndiyo njia ambayo Mungu achagua kututolea Neno lake la kweli lenye kuokoa uhai, kama vile mtume Paulo aelezavyo: “Tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu, wala si kutoka kwetu.” (2 Wakorintho 4:7) Usikivu na unyenyekevu utatuwezesha kuona thamani ya kweli ya hazina hiyo na si kuona tu vile “vyombo vya udongo,” au wawakilishi wa kibinadamu, wanaoileta kwetu. Kwa kufanya hivyo, tutaongeza pia uwezekano wa ‘kufichwa kwetu katika siku ya kasirani ya Yehova’ na kuwa miongoni mwa wale wasikivu ‘watakaoirithi dunia.’—Sefania 2:3; Mathayo 5:5, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki