Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 6/15 kur. 3-4
  • Wapendwa Wako Waliokufa Wao Wako Wapi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wapendwa Wako Waliokufa Wao Wako Wapi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Inakuwaje kwa Wapendwa Wetu Waliokufa?
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Tumaini la Ufufuo Ni Hakika!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Sababu kwa Nini Waweza Kuamini Katika Ufufuo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Jizoeze Imani Ili Upate Uhai wa Milele
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 6/15 kur. 3-4

Wapendwa Wako Waliokufa Wao Wako Wapi?

ALEC alitamauka. Haipati juma moja, yeye alipoteza wawili kati ya rafiki zake. Mmoja wao, Nevil, alikufa kutokana na jeraha la risasi. Yule mwingine, Tony, aliuawa katika aksidenti ya gari. Maswali ambayo hayakuwa yamepata kumsumbua, sasa yalimhangaisha mvulana huyo wa miaka 14 wa Afrika Kusini. ‘Kwa nini watu hulazimika kufa? Na ni nini hutukia baada ya kifo?’ yeye akajiuliza-uliza.

Akiwa njiani kwenda kwenye maziko ya Nevil, Alec alitumaini kwa moyo mweupe kwamba angepata majibu kwa maswali haya. “Lakini,” yeye akumbuka, “kasisi alisoma tu kutoka kitabu fulani na kusema kwamba Nevil alikuwa ameenda mbinguni. Halafu, tukiwa kando ya kaburi, yeye alisema kwamba tungojee ufufuo. Nilivurugika. Ikiwa Nevil alikuwa mbinguni, yeye angewezaje kuwa akingojea ufufuo?”

Baadaye siku iyo hiyo, Alec alihudhuria maziko ya Tony. Ibada ya maziko ilifanywa kidesturi katika lugha ambayo hakuelewa. Lakini, tabia yenye hisia za kupita kiasi ya baadhi ya waombolezi ilimsadikisha Alec kwamba hawakupata faraja yoyote. “Usiku huo,” yeye aeleza, “niliudhika sana. Nilijihisi kuwa hoi na kuvurugika. Hakuna mtu ambaye angenipa majibu yenye kuridhisha kwa maswali yangu. Kwa mara ya kwanza maishani mwangu, nilijiuliza-uliza kama kweli kuna Mungu.”

Kila mwaka mamilioni, kama Alec, hupoteza wapendwa katika kifo. “Ulimwenguni pote,” chaeleza kitabu 1992 Britannica Book of the Year, “kulikuwa na vifo 50,418,000 katika 1991.” Na ni watu milioni ngapi zaidi wamekufa tangu wakati huo? Wazia yale machozi mengi sana yaliyotolewa na waokokaji waliofiwa! Jambo linaloongeza kihoro chao ni ule mvurugo unaoletwa na maoni yanayotofautiana juu ya kifo.

Hivyo wengi, kama vile Alec, hutamauka na kutia shaka kama kuna msingi wowote wa kuwa na tumaini katika uhai wa wakati ujao baada ya kifo. Kulingana na Encyclopedia of Religions, “katika enzi zote, watu wenye kufikiri wamekuwa na maoni tofauti na umati, . . . wakitilia shaka jinsi nafsi au uhai mzima waweza kuendelea kuishi ukiwa mbali na ubongo na mwili.”

Kwa kupendeza, ensaiklopidia iliyotajwa juu yakiri kwamba wazo la kidini juu ya nafsi isiyoweza kufa inayoendelea kuishi ikiwa mbali na mwili haiungwi mkono katika Biblia. Ni kweli, katika mahali pachache, Biblia hurejezea “nafsi” ya mtu kuwa ikiacha au hata kurudia mwili uliokufa, lakini katika pindi hizo “nafsi” yatumiwa katika maana ya “uhai,” uliopotezwa au uliopatikana tena. (Mwanzo 35:16-19; 1 Wafalme 17:17-23, New World Translation) Mara nyingi, neno “nafsi” hutumiwa katika Biblia kueleza juu ya viumbe vinavyoonekana vya mwili na damu, naam, viumbe vilivyo hai. (Mwanzo 1:20; 2:7) Kwa sababu hiyo, Biblia husema mara nyingi kwamba nafsi hufa. (Ezekieli 18:4, 20; Matendo 3:23; Ufunuo 16:3, NW) Neno la Mungu husema kwamba nafsi zikiisha kufa, hizo ‘hazijui neno lolote.’—Mhubiri 9:5, 10.

Kwa upande ule mwingine, Biblia ina masimulizi ya watu waliokufa nao wakarudishwa kwenye uhai. Katika kisa cha Lazaro, hilo lilitukia baada ya yeye kuwa amekufa kwa siku nne. (Yohana 11:39, 43, 44) Hata hivyo, ni nini kitakachowapata watu waliokufa mamia au maelfu ya miaka iliyopita? Je! mataraja yao ya uhai wa wakati ujao yamaanisha kwamba Mungu atafufua mwili uleule waliokuwa nao walipokufa?

La. Wazo kama hilo halipatani na yale yanayotukia kwa atomu zinazofanyiza mwili uliokufa. Baada ya muda, baadhi ya atomu hizohizo hufyonzwa na uoto ambao, nao, huliwa na viumbe wengine na kuwa sehemu ya miili yao.

Je! hilo lamaanisha kwamba hakuna tumaini kwa watu waliokufa zamani? La. Muumba wa ulimwengu wetu mzima ulio mkubwa ana kumbukumbu la kustaajabisha mno, lisilo na mipaka. Katika kumbukumbu lake lililo kamilifu, yeye ana uwezo wa kuhifadhi utu na tabia za urithi za binadamu yeyote aliyekufa ambaye yeye achagua kukumbuka. Isitoshe, Yehova Mungu ana uwezo wa kuumba tena mwili wa kibinadamu wenye msimbo-jeni (sheria za urithi) uleule hasa wa mtu aliyeishi hapo kwanza. Yeye pia aweza kutia ndani yao kumbukumbu na utu wa yule anayemkumbuka, kama vile Abrahamu.

Karibu miaka elfu mbili baada ya kifo cha Abrahamu, Yesu Kristo alitoa uhakikishio huu: “Ya kuwa wafu hufufuliwa, hata na Musa alionyesha katika sura ya Kijiti, hapo alipomtaja Bwana kuwa ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Naye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai; kwa kuwa wote huishi kwake.” (Luka 20:37, 38) Zaidi ya Abrahamu, Isaka, na Yakobo, mamilioni ya wanadamu wengine waliokufa wako hai katika kumbukumbu la Mungu, wakingojea ufufuo unaokuja. “Kutakuwa na ufufuo wa wafu, wenye haki na wasio haki pia,” Biblia huthibitisha.—Matendo 24:15.

Majuma machache baada ya kufiwa, Alec alipata majibu kwa maswali yake. Mmoja wa Mashahidi wa Yehova alimzuru nyumbani mwake na kumwonyesha yale ambayo Neno la Mungu husema juu ya kifo na juu ya ufufuo. Hilo lilimfariji Alec na kufanya maisha yake yawe na maana mpya.

Je! wewe pia ungependa kujifunza zaidi juu ya tumaini la ufufuo lenye msingi wa Biblia? Kwa kielelezo, je, ufufuo mwingi utatukia mbinguni au duniani? Na ni lazima mtu afanye nini ili apate kibali cha Mungu na kuona utimizo wa ahadi Yake nzuri ajabu la kwamba watu wataungana tena pamoja na wapendwa wao waliokufa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki